Waziri wa Elimu sayansi mafunzo na ufundi profesa Joyce ndalichako


Na. Vero Ignatus Arusha

Waziri wa Elimu sayansi mafunzo na ufundi profesa Joyce ndalichako amewasimamisha kazi watumishi sita wa chuo cha ualimu Patandi kwa tuhuma ya ubadhirifu wa fedha

Profesa Ndalichako amesema kuwa zaidi ya shilingi milioni 2.5 zilizotengwa na serikali kwaajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya chuo hicho imetumika visivyo.Waliosimamishwa kazi ni pamoja Israel Mayage kutoka chuo kikuu cha sayansi na teknonojia mbeya ambae awali alikuwa msimamizi wa mradi shule hiyo, mhasulibu Rose Kijaka na mwenyekiti wa kamati ya mapokezi Peter Mosha

Wengine ni kaimu chuo cha Patandi Isaac myovela, Ofisa manunuzi na ugavi Charles Njarabi na Hendry Malei ambaye alihamishiwa chuo cha Monduli, pia ameagiza mkuu chuo cha Patandi Janesi Mmbaje abadilishiwe majukumu kwasababu za kiafya

Waziri Ndalichako amechukua hatua hiyo mara baada ya kutembelea shuleni hapo kukagua mradi wa majengo licha ya taarifa kuonyesha umechelewa kukamilika bila Sababu ya msingi huku.thamani ya fedha inapingana na hali halisi na pia ubora wake.Amemuagiza Katibu mkuu wa wizara hiyo Dkt. Leonard Akwilapo Kupeleka watendaji wengine wakati uchunguzi ukiendelea kufanyika naendapo ikithibitika sheria itachukua mkondo wake

Mimi ninachotaka kujua hayo malori 170 yalimwagwa wapi na hiyo mifuko ya saruji 6520 ipo wapi na hadi sasa imetumikaje. Aliuliza profesa NdalichakoAmesema katika ziara yake amebaini fedha zilizotumika katika ujenzi huo ni shilingi milioni 990 ambapo amesisitiza kuwa fedha hiyo ni nyingi kuliko hali halisi ya ujenzi

Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro amewataka wale wote waliopo kwenye kamati ya ujenzi ukiondoa wale ambao wameondolewa wanakutana leo kupitia mambo yote yaliyosalia ili waweze kuwapokea wanafunzi tarehe 7 feb 2019 
.
Shule ya sekondari ni Patandi ni ya wanafunzi wenye ulemavu mbalimbali nchi nzima ikimalizika itachukua watoto 640 na itakuwa na vifaa vya kisasa ambavyo watavitumia kwaajili ya kujifunzia

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...