Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MKUU wa Wilaya ya Tunduru Juma Homera amekabidhi meza na viti 70 kwa shule mpya ya Sekondari ya Muhewesi iliyosajiliwa mwaka 2019 na hiyo kumaliza changamoto hiyo ambayo ilikuwepo shuleni hapo. 

Homera amekabidhi viti na meza hivyo kwa Ofisa Elimu Sekondari katika wilaya hiyo Selestine Kahangwa kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru. 

Shule hiyo ipo kwenye kijiji na kata ya Muhuwesi ambapo moja ya changamoto kubwa ilikuwa ni ukosefu wa viti na meza kwa ajili ya wanafunzi wanaosoma shuleni hapo. 

Akizungumzia vifaa hivyo ,Homera ameiambia Mchuzi Blog kuwa thamani ya vifaa vyote hivyo ni Sh.5,000,000 na kwamba amewashukuru wadau walioshiriki kuchangia meza na viti hivyo.Amewataja baadhi ya wadau hao ni Kampuni ya Jafu Investment iliyochangia meza 40 na viti 40, Jitegemee Ranchi iliyochangia meza 15 na viti 15, Lupondo amechangia meza 5 na viti 5,na Mataka amechangia meza 10 na viti 10. 

Hata hivyo, Homera amesema anatarajia kukabidhi meza 200 na viti 200 vingine kwa ajili ya shule mbalimbali za sekondari wilayani humo huku akisisitiza kuwa "Tukutane site#Tukutane Kazini.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...