Rais mpya wa chama cha wanasheria nchini TLS Dkt. Rugemeleza Nshala
Rais TLS aliyemaliza muda wake Fatma Karume akitoa neno la shukrani leo Jjini Arusha
Dkt. Rugemeleza Nshala kabla ya matokeo ya uchaguzi wa kuwa Rais wa TLS
Dkt.Rugememelela Nshala mara baada ya kutangazwa mshindi wa kiti cha urais wa TLS leo Jijini Arusha katika ukumbi wa AICC.




NA:Vero Ignatus , Arusha

Wanachama wa chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS) wamewataka viongozi wapya watakao kiongoza chama hicho kutoa fursa sawa kwa mawakili walemavu ili kuweza kuhudumia vyema jamii Katika masuala ya kisheria na kuondokana na fikra potofu dhidi ya Watu walemavu.

Wakizungumza Mara baada ya kupiga kura baadhi ya mawakili ambao ni wanachama wa chama hicho wamesema ni vyema kwa viongozi kushirikiana na mawakili walemavu ili kutoa hamasa Katika jamii.

Elibariki Maeda ni Mwenyekiti wa chama chama mawakili wa kujitegemea Kanda ya Arusha amesema Ulemavu sio Sababu ya kushindwa kutekeleza majukumu yao Huku Rais wa chama hicho anaemaliza muda wake Fatma Karume akatoa neno kwa viongozi wajao.

Kwa upande wake Rais aliemaliza muda wake Fatma Karume amesema kuchaguliwa kwa Dkt Rugemeleza Nshala kuongoza chama hicho anaamini chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS) iko Katika mikono salama.

Katika hatua nyengine bi Fatma Karume ametumia fursa hiyo kuwashukuru wanachama waliompa dhamana ya kuongoza kwa kipindi alicho kuwa madarakani hivyo ni wakati muafaka kwa wanasheria kumpa ushirikiano chanya Rais Mpya wa TLS.

Matokeo ya uchaguzi huo yametoka kutangazwa jioni ambao Katika Nafasi ya wagombea urais ilikuwa ikigombewa na Godfrey wasong, Gaspar Nicodemas,Godwin Simba,Rugemeleza Nshala na John seka ambapo Dkt Rugemeleza Nshala ameobuka kidedea.


MATOKEO YA RAIS 2019/2020 (TLS)

Jumala ya Kura zilizo poigwa na wanachama wa TLS Ni 1217.

1-Dkt Rugemeleza Nshala kura 647.
2-Godwin Simba kura 354
3-Godfrey Wasonga kura 123
4-58 Gaspar Nicodemas kura 58
5-John Seka kura 29

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...