Kaimu Msajili wa Jumuiya za Kijamii na Taasisi za Kidini kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Jesca Shengena akitoa maelekezo kwa Makamu Mwenyekiti wa Kanisa la Mungu Mfalme, Makange Kitua (kushoto), wakati wa zoezi la Uhakiki  wa  Jumuiya  za  Kijamii na Taasisi za Kidini linaloendelea katika Ofisi Ndogo ya wizara hiyo jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Afisa  wa  Kitengo  cha  Jumuiya  za  Kijamii  na  Taasisi  za  Kidini kutoka Wizara  ya  Mambo  ya  Ndani ya Nchi, Neema Ngalawa akihakiki taarifa za Taasisi ya Kidini ya Peaceful Life Ministries wakati wa zoezi hilo linaloendelea Ofisi  Ndogo  ya  wizara  hiyo  jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mchungaji Msaidizi  wa  Kanisa  hilo, Paskazia Makofi.
 Makamu Mwenyekiti wa Kanisa la Mungu Mfalme, Makange Kitua akitoa maelezo ya  taasisi  yake  kwa  Afisa wa Kitengo cha Jumuiya za Kijamii na Taasisi za Kidini kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Neema Ngalawa (kulia),  wakati  wa  zoezi la uhakiki linalofanyika Ofisi Ndogo ya wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Afisa  wa  Kitengo  cha  Jumuiya  za  Kijamii  na  Taasisi  za  Kidini kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Thomas Sanira akimsikiliza  Katibu Mtendaji  wa  Jumuiya  ya  Istiqama, Issa  Suleiman(kulia), wakati wa zoezi la uhakiki wa taasisi hizo linaloendelea Ofisi Ndogo ya wizara hiyo jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Imekuwa ni mchezo wa watu wengi hasa wanaojiita wakristo kuanzisha makanisa ya uongo na kweli kwa manufaa yao. Unakuta wanawatumia vibaya watu masikini na wao wanatajirika mpaka wananunua ndege. Serikali ingekontro utitiri wa makanisa yanayoanziskwa bila mipangilio badala ya kuanza kuhakiki.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...