Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imevunja mkataba wa ujenzi wa mradi mkubwa wa Maji maarufu kama mradi wa Maji Sawala katika Kata ya Mtwango wenye thamani ya shilingi Bilioni 1.8 uliyokuwa ukitekelezwa kwa pamoja na Kampuni za Siha Enterprise Co. LTD na Mavonda Co. LTD za Jijini Dar Es Salaam.

Halmashauri imelazimika kuvunja mkataba huo baada ya Mkandarasi kuonesha uwezo mdogo wa kutekeleza kazi hiyo, kwani tangu asaini Kandarasi ya ujenzi mnamo mwezi Januari 2018, katika hali ya kusikitisha ametekeleza jukumu hilo kwa asilimia 30 pekee licha ya kulipwa Fedha ya awali zaidi ya shilingi Milioni 270.

Aidha, Mkandarasi huyo anatakiwa kuilipa Halmashauri kiasi cha shilingi Milioni 413, ambapo kati ya hizo shilingi Milioni 254 ni faini wakati Milioni 159 ni bakaa ya Fedha ya utangulizi ambayo alilipwa baada ya kusaini mkataba.

Uongozi wa Halmashauri unaomba radhi kwa wananchi wa Kata ya Mtwango kwa kutopata huduma muhimu ya Maji kwa wakati, hata hivyo, uongozi unawahakikishia kuwa mradi utatekelezwa kama ilivyokusudiwa kwani taratibu za kumpata Mkandarasi mwenye uwezo na utashi wa kuujenga zimeanza.

Mnamo mwaka 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ilitiliana saini na Kampuni za Siha Enterprise Co. LTD pamoja na Mavonda Co. LTD kwa kandarasi ya miezi 12 ya kujenga na kuyafikisha Maji katika makazi ya watu kwenye Vijiji nne vya Sawala, Mtwango, Lufuna na Kibao kwa shabaha ya kuhudumia watu elfu 14.

Netho Ndilito
Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...