NA MWAMVUA MWINYI, BAGAMOYO
SHIRIKA linalosaidia watu wenye maisha duni na kuleta mabadiliko chanya katika jamii (WHO IS HUSSAIN?), tawi la Dar es salaam kwa kushirikiana na diwani wa kata ya Vigwaza Mohsin Bharwani ,limetoa msaada wa vyakula kwa kaya 200 zilizopo kwenye kata hiyo,uliogharimu sh.milioni kumi.

Kila kaya kati ya hizo imepatiwa box lenye vitu vilivyogharimu sh. 50,000 ,ikiwemo mchele kilo 3, maharage kilo tatu, sukari kilo 3, majani ya chai, tende na tambi ili kuwasaidia katika mwezi mtukufu wa Ramadan.

Akikabidhi msaada huo, mratibu msaidizi wa shirika la Who is Hussain?, tawi la Dar es salaam Meesam Bandali amesema,walengwa ni watu wasio na uwezo wakiwemo wenye ulemavu,wazee katika kaya 200 kata ya Vigwaza.
Awali diwani wa kata ya Vigwaza, Mohsin Bharwani, amelishukuru shirika hilo kwa kumfuata kumuomba kupeleka msaada kwa kaya zinazoishi kwenye mazingira magumu.

Nae msemaji mkuu wa who is Hussain? Iffet Thawer ameeleza Hussain ni mjukuu wa mtume Mohammad S.W.A. ambae alipinga dhuluma hivyo kuwa chanzo cha wao kuhamasika kufanya shughuli za kusaidia jamii ikiwa sasa ni miaka kumi .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...