Mabingwa wa soka katika michuano ya Ligi Kuu ya Hispania, LaLiga, timu ya Sevilla Fútbol Club  maarufu kama Sevilla FC inatarajiwa kuwasili nchini leo kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya  Simba ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya  kwa timu hiyo kucheza nchini  Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana, timu hiyo ambayo iliundwa January 25, 1890 (ina umri wa miaka 129 sasa)  hiyo inatarajiwa kuwasili jioni hii katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius  Nyerere jijini Dar es salaam.

Kulingana na taarifa hiyo mechi hiyo itakuwa ni maalum kwa vinara hao wa LaLiga ambao wanadhaminiwa na  SportPesa na akaongeza  kwamba ziara itahusisha matukio kadhaa ya   jamii na michezo ikiwemo kliniki namafunzo mbalimbali.

 "Kama ushindani wa kimataifa unakutana na dhamira ya LaLiga kuwa karibu na mashabiki wake. Kwa kweli kwamba mashabiki wetu wa Tanzania wataweza kupata furasa ya  kuangalia karibu  klabu kubwa kama Sevilla FC inamaanisha kuwa ni fursa kubwa kwa kila mtu," alisema Mkurugenzi wa Maendeleo ya Kimataifa katika Ligi ya La Liga, Oscar Mayo.

  Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Utawala na Utekelezaji wa SportPesa, Tarimba Abbas, kampuni yao  imeshirikiana na baadhi ya taasisi za soka za kubwa  ulimwenguni  baada ya kuna kuna haja ya  kuleta uzoefu  huu mkubwa  kwa Tanzania.

 "Ili kufurahia kuona moja ya klabu  kubwa za  mpira wa miguu  Ulaya, Sevilla FC. Kwa makubaliano yetu na LaLiga ambayo ni ligi bora duniani, tutaweza kuonyesha vipaji vyetu  na kuboresha kiwango cha soka  nchini ", alisema Talimba.

 Alisema kwamba mechi hiyo ni sehemu ya mradi wa 'LaLiga duniani  ambao unalenga kueneza soka  la  Hispania kimataifa na  kueneza pia sera ya 'Marca España', kuleta karibu mashabiki wa  LaLiga na  kukuza klabu nje ya nchi yetu.

Hii itakuwa ni klabu ya pili Ulaya kufanya ziara Afrika Mashariki, baada ya mwaka 2017 Everton FC kucheza  na  Gor Mahia  nchini  Kenya, ingawa  sio mara ya lkwanza kwa  Sevilla kutua katika bara hili kwani  mwaka  2015  ilikuwa nchinbi  Morocco ambao ilicheza mechi ya kuajindaa na  LaLiga dhidi ya timu ya   Hassania Union Sport d'Agadir.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...