Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
Ni ukweli usiopingika kuwa mpira wa miguu ndio mchezo wenye mashabiki wengi zaidi ukilinganisha na michezo mingine,  na hiyo imepelekea uwekezaji mkubwa katika sekta hiyo ambayo vijana wanapata ajira kwa kiasi kikubwa.

Katika sekta hiyo ya mpira wa miguu kwa mujibu wa jarida la Daily Mail viwanja vikubwa vitatu vilivyotajwa ni pamoja na;

1. Uwanja Rungrado May 

Huu ni uwanja wa mpira wa miguu mkubwa zaidi duniani, unapatikana Pyongyang Korea Kaskazini, na una uwezo wa kubeba watazamaji 114,000 na ujenzi wake ulikamilika mwaka 1989 na mathalani hutumika kwa kucheza mechi kubwa za watu wengi pamoja na matukio makubwa, paa ya uwanja huo una mita 197 kutoka ardhini.

2. Uwanja wa Camp Nou

Uwanja huu unapatikana Barcelona Spain ukiwa ni uwanja wa pili kwa ukubwa duniani, tangu mwaka 1957 uwanja huo umekuwa umekuwa ukitumika kama uwanja wa nyumbani kwa timu ya Barcelona, uwanja huo unauwezo wa kubeba watazamaji 99,354 huku ukiwa uwanja mkubwa zaidi katika bara la Ulaya. Unatumika katika michezo mbalimbali ikiwemo mashindano ya Olympiki ya mwaka 1992 pamoja na fainali za UEFA, uwanja huu ulichukua takribani miaka mitatu katika ujenzi wake huku ikieleza kuwa umegharimu zaidi ya shilingi milioni 288.

3. Uwanja wa FNB Soccer City

Uwanja huu unapatikana Johannesburgy nchini Afrika Kusini ukiwa ni uwanja mkubwa zaidi Afrika huku ukishika nafasi ya tatu kwa ukubwa duniani, uwanja huu una uwezo wa kubeba mashabiki 94,736 na unapatikana  jirani na makao makuu ya shirikisho la mpira wa mguu nchini humo.

Uwanja wa FBN ulitangazwa zaidi katika uzinduzi wa fainali za kombe la duniani mwaka 2010 ambapo timu za Netherlands na Spain zilicheza kubwa zaidi mwaka 1990 uwanja huo ulitumiwa na aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Nelson Mandela kuhutubia wananchi kwa mara ya kwanza mara tu alipoteka jela.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...