Mkurugenzi wa taasisi ya sekta binafsi tanzania (tpsf) godfrey simbeye amesema kufuatia nchi kukabiliwa na changamoto ya vijana kukosa ajira kwasababu ya kukosa sifa kiushindani hivi sasa kunaanzishwa mabaraza ya ujuzi ya kisekta yenye lengo la kuhakikisha suala la ujuzi linakuzwa kiufasaha kuanzia elimu ya vyuoni pamoja na kuwezeshwa kwa vijana wabunifu nchini.

Simbeye amesema hayo mjini Morogoro wakati warsha ya kuandaa wajumbe wa mabaraza ya kisekta yenye nia ya kuwafanya kujua majukumu yao.Amesema kuwa Tpsf ni moja ya watekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kukuza ujuzi, na Tpsf ndio inayohusika na kipengele cha kuunda mabaraza ya ujuzi katika sekta sita ambazo ni muhimu kiuchumi ikiwemo Kilimo biashara, Utalii, Nishati, Ujenzi, Tehama, na Usafirishaji na zote zitakuwa na mabaraza ya ujuzi.

“mabaraza yatatakiwa kwenda na spidi ya teknolojia na mabadiliko yaliyobadilika kwenye viwanda vinavyoendelea na vinavyoanzishwa nchini, mabaraza yanatakiwa kutafanya tafiti kwa lengo la kuwafikia vijana wenye vumbuzi mbalimbali” alisema Simbeye.
Pia amesema katika mkakati huo wa kukuza ujuzi Tanzania TPSF lilidhamilia kuunda baraza la ujuzi la taifa, na nchi kama Tanzania imechukua hatua nyingine tofauti na imekuwa nchi ya pili kwa bara la Afrika ambayo imekuwa na mfumo huo wa mabaraza.
Juni 22 mwaka huu waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako anatarajiwa kuzindua mabaraza ya kisekta jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi wa taasisi ya sekta binafsi tanzania (tpsf) godfrey simbeye wapili kutoka kulia kwa walioketi pamoja na wadau wakati warsha ya kuandaa wajumbe wa mabaraza ya kisekta yenye nia ya kuwafanya kujua majuku

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...