Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

MSANII wa filamu na vichekesho nchini Tabu Mtingita amewashauri wasanii kuwa na uthubutu katika kazi zao ili waweze kufikia malengo yao na hiyo ni pamoja na kujituma kwa kufanya kazi kwa bidii.

Akizungumza na blogu ya jamii Tabu amesema kuwa kupitia sanaa ya uigizaji aliyoifanya wa muda mrefu amejifunza zaidi kuthamini kile anachokifaanya na kujenga maudhui ambayo yanasaidia jamii kitu ambacho kimempa umaarufu zaidi.

Amesema kuwa kabla ya kuanza kufanya sanaa ya uigizaji Ndumbagwe Misayo maarufu kama Thea alimvutia sana kupitia uigizaji wake wa kubadilika na kujenga uhalisia na kufanya sanaa ya uigizaji kabla ya kuanza kujihusisha na sanaa ya vichekesho ambayo imezidi kumpa umaarufu.

Tabu amewataka wasanii kuwa na subira na uvumilivu pamoja na kufanya kazi zenye manufaa na zenye kubadilisha na kujenga zaidi jamii zao huku akisisitiza wazazi na walezi kuichukulia sanaa kama kazi nyingine.
Msanii wa filamu na vichekesho nchini,Tabu Mtingita akizungumza na Michuzi Tv leo jijini Dare es Salaam kuhusu soko la filamu ambapo amesema wasanii watengeneze kazi zenye tija kwa jamii.(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...