Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv

Timu ya KCCA imefanikiwa kunyakua ubingwa wa Kagame Cup baada ya kuifunga Azam Fc mchezo uliomalizika kwa ushindi wa goli 1-0.

Mchezo huo wa fainali ulichezwa majira ya saa 11 jioni kwa saa za Rwanda na Saa 12 jioni kwa saa za Tanzania.Azam waliokuwa mabingwa watetezi walikubali kuuvua ubingwa huo walioushikilia kwa miaka miwili mfululizo. 
Kwa upande wa KCCA wanalichukua Kombe la Kagame kwa mara ya pili baada ya miaka 41 kupita toka walivyolichukua kwa mara ya kwanza.

Kocha wa Azam Etienne Ndayiragije amewapongeza KCCA kwa kuweza kushinda mchezo huo na kuchukua ubingwa na mpira ni mchezo wa makosa walipata nafasi wakashindwa kuzitumia KCCA walipata na wakaandika goli lililowapa ubingwa.

Ndayiragije amesema, timu yake imecheza vizuri na anawapongeza kwa hatua walioyofikia kwani siku zote mshindi ni mmoja.

Azam wamecheza fainali ya tatu mfululizo na kufanikiwa kulichukua kombe hilo mara mbili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...