Ikiwa zimebaki siku chache kuelekea katika sherehe za ufunguzi wa Reli ya kutoka Tanga kwenda Kilimanjaro, Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mh Kissa Kasongwa akiwa katika mkutano na wananchi wa Kata ya Magila gereza amelazimika kusimamisha mkutano na kushuhudia majaribio ya Treni ya mizigo iliyokuwa ikifanya safari zake katika reli ya kutoka Tanga kwenda Kilimanjaro ambayo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi ifikapo julai 20-2019 wilayani Moshi.

Dc Kissa amesema kuwa ni bahati kubwa kwa wanakorogwe kuhushudia majaribio hayo ya Treni ya mizigo ikifanya safari katika reli ambayo inapita wilayani Korogwe ikitokea Tanga na kwamba nao wameshiriki kwa namna moja au nyingine katika shagwe za sherehe hizo za uzinduzi ambapo ni utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi kwa maana iliahidi na sasa imetekeleza.
Kufunguliwa kwa Reli hii ya kupitisha treni za mizigo kutoka Tanga kwenda Kilimanjaro kutasaidia sana kukuza uchumi katika mikoa hii miwili inayounganishwa na reli pamoja na Taifa kwa ujumla.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...