Meneja wa Mauzo ya Reja Reja wa Benki ya Azania, Jackson Lohay (katikati) akiongea kwa njia ya simu na mmoja wa washindi wa promosheni ya ‘Amsha Ndoto’ katika droo iliyofanyika katika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam. Jumla ya Sh. 8,000,000/- ilitolewa kwa washindi watatu walioshiriki katika promosheni hiyo.
Benki ya Azania (ABL) leo imewatangaza washindi wa promosheni yake ya ‘Amsha Ndoto’ ambayo ina lengo la kuwahamasisha wateja wake na umma wawatanzania kujenga utamaduni wa kuweka akiba itakayowasaidia kuwa na maisha ya baadaye yaliyo imara kifedha.

Promosheni hii ambayo ni ya mizezi mitatu ilianza rasmi tarehe 27/06/2019 na inatarajia kufikiatamati tarehe 27/09/2019 huku ikihusisha wateja wa Azania Benki wa zamani na wale wapya naimejikita zaidi katika bidhaa mbili kuu za uwekaji akiba, ambazo ni: Ziada Akaunti pamoja naWatoto Akaunti.

Akitangaza washindi kwenye droo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam, Meneja wa Mauzo ya RejaReja wa Benki ya Azania, Jackson Lohay, amesema benki imetimiza ahadi ya kuwapatia zawadiwashindi walioshoriki kwenye promosheni na kwamba zawadi wanazopewa zitawasaidiakutimiza ndoto zao.

Kwa mujibu wa Lohay, washindi wa mwezi Julai wa promosheni hii ambao wamepatikana baadaya droo kufanyika ni;

1. Barakaeli Mmari amejishindia kiasi cha TZS 2,000,000/- (Arusha)
2. Rose Anaeli amejishindia kiasi cha TZS 3,000,000/- (Dar es Salaam)
3. Ketus Isack Malekamo amejishindia kiasi cha TZS 3,000,000/- (Tunduma)

Lohay ameongeza kuwa ili mtu aweze kushiriki kwenye promosheni ya Amsha Ndoto ni lazimakwanza awe mteja wa Azania Benki mwenye akiba ya kiasi kisichopungua TZS 1,000,000 ambayeanapewa tokeni zinazomwezesha kufuzu kwa ajili ya droo ya mwisho inayowapata washindi.

Wanaobahatika kushinda watafurahia riba ya 6% katika kipindi chote cha kampeni na mwakamzima.Akitoa pongezi kwa washindi wa promosheni, Lohay amewahasa wateja wa ABL kushiriki kwawingi na kwamba wana nafasi kubwa ya kujishindia zawadi lukuki katika droo zinazofuata hukuwakijahakikishia kuwa na akiba ya kutosha kwenye akaunti zao kwa ajili ya matumizi yao ya sikuza usoni.

“Tunawahamasisha wazazi wote na walezi kuwafungulia Watoto wao ‘Watoto Akaunti’ ili kuwana uhakika wa maisha yao ya baadaye yaliyo salama. Kwa namna hii hawatahangaika kutafutanamna gani ya kuwaandaa watoto wao kwa maisha ya baadaye kwani akaunti hii inaweka msingiwa kuwaandaa watoto kujifunza namna ya kuweka akiba kuanzia kwenye umri mdogo”,amesema Lohay.

Promosheni hii, yenye kaulimbiu: ‘Weka Akiba Ushinde Tumuwezeshe ada ya shule’,inawasilishwa kupitia mitandao ya kijamii na tovuti za ndani za benki. Benki pia imetengenezatovuti ndogo, maalumu kwa wateja wapya kujiunga na inaweza kupatikana kupitiaamshandoto.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...