Naibu Gavana wa benki kuu Tanzania (BoT) Dr.Bernard Kibesse amezitaka taasisi za kifedha kuzingatia uwadilifu katika utoaji wa huduma za kifedha hasa katika zama hizi za kidigitali ili kuwahahikishia wateja wao usalama wa fedha zao.
Akizungumza katika kongamano la Taasisi za kifedha za Afrika Mashariki linaloendelea jijini Arusha ,Naibu Gavana amesema kuwa licha ya changamoto za wizi kwa njia za mitandao bado taasisi hizo zina jukumu la kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu Mkubwa kwani ndio nguzo kuu ya huduma hizo.
Aidha amesema kuwa serikali haitasita kuwachukulia hatua taasisi za kifedha zinazokiuka sheria ,maadali na tararibu za utoaji wa huduma ikiwemo kuzinyang'anya leseni .
Nae Mkurugenzi mtendaji wa Tanzania institute of bankers,
Patrick Mwisusa amesema kuwa kongamano hilo linalenga kuangalia maswala ya nafasi ya maadili katika utoaji wa huduma za kifedha na kuhimiza suala la uadilifu katika kulinda tasnia ya fedha Katika nchi za Afrika Mashariki
Mshiriki wa kongamano ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi za Kifedha nchini Kenya, Gilbert Allela amesema kuwa taasisi za fedha zina nafasi kubwa ya kulinda na kutunza uaminifu wa wateja wao kwa kujifunza mbinu za kisasa za kukabiliana na wizi wa kimtandao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...