Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv
Klabu ya Simba Imefanikiwa kuanza vyema msimu wake mpya baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Power Dynamos ya Zambia katika mchezo wa kirafiki kwenye tamasha la Simba Day usiku wa leo Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.
Klabu ya Simba Imefanikiwa kuanza vyema msimu wake mpya baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Power Dynamos ya Zambia katika mchezo wa kirafiki kwenye tamasha la Simba Day usiku wa leo Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.
Katika mchezo huo uliokusanya umati wa mashabiki waliosheheni Uwanja wa
Taifa, shujaa wa Simba SC alikuwa ni mshambuliaji wake wa kimataifa wa
Rwanda, Meddie Kagere aliyefunga mabao yote matatu ya timu yake.
Katika mchezo huo ulioanza majira ya saa 12 jioni ilichukua dakika tatu ya mchezo kwa Mshambuliaji wa Kimataifa Meddie Kagere kuifungia timu yake goli la kuongoza akimalizia pasi ya kiungo Mzambia, Clatous Chama.
Katika mchezo huo ulioanza majira ya saa 12 jioni ilichukua dakika tatu ya mchezo kwa Mshambuliaji wa Kimataifa Meddie Kagere kuifungia timu yake goli la kuongoza akimalizia pasi ya kiungo Mzambia, Clatous Chama.
Dakika ya 23, Jimmy Dlingai anaisawazishia Power Dynamos kwa kichwa
akimalizia kona iliyopigwa na Larry Bwalya kumtungua kipa Beno
Kakolanya.
Mpaka mapumziko timu hizo zimeenda zikiwa zimefungana 1-1. Kipindi cha pili ilifanikiwa kupata mabao mawili zaidi, yote yakifungwa na Kagere
Mpaka mapumziko timu hizo zimeenda zikiwa zimefungana 1-1. Kipindi cha pili ilifanikiwa kupata mabao mawili zaidi, yote yakifungwa na Kagere
Kwenye dakika ya 58 kwa kichwa akimalizia pasi ya winga mpya, Deo Kanda
aliyesajiliwa kutoka TP Mazembe na dakika ya 73 akiandika bao la tatu.
Baada ya mchezo huo, Simba watasafiri kwenda Msumbiji kwa ajili ya mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji, UD do Songo Jumamosi, kabla ya kurejea nyumbani kwa mchezo wa marudiano kati ya Agosti 23 na 25.
Baada ya mchezo huo, Simba watasafiri kwenda Msumbiji kwa ajili ya mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji, UD do Songo Jumamosi, kabla ya kurejea nyumbani kwa mchezo wa marudiano kati ya Agosti 23 na 25.
Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Beno Kakolanya, Mohammed Hussein
‘Tshabalala’, Shomary Kapombe/Said Ndemla dk85, Tairon Santos Da
Silva/Kennedy Juma dk87, Pascal Wawa, Muzamil Yassin, Deo Kanda/Rashid
Juma dk75, Sharaf Eldin Shaibob/Gerson Fraga ‘Viera’ dk49, Meddie
Kagere, Clatous Chama na Francis Kahata/Miraj Athumani ‘Madenge’ dk61.
Power Dynamos; Lawrence Mulenga, Larry Bwalya, Raphael Makubuli, Jimmy
Dlingai, John Soico/Clifford Saudi dk75, White Mwamambaba, Benson
Sakala, Kondwani Chiboni/Faustin Bakodica dk51, Christian Ntouba/Judo
Bolondio dk59, Fredrick Mulamba/Jackob Phiri dk54 na Kassimu
Titus/Lameck Kafwaya dk 67.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...