KENYA imechaguliwa rasmi kuwa mwakilishi wa bara la Afrika kwenye baraza la ulinzi na usalama la UN kwa mwaka 2020/2021.

Rais waKenya Uhuru Kenyatta amepokea taarifa hiyo kutoka UN kwa nchi hiyo kuwa sehemu baraza la ulinzi la UN kwa kushirikiana na kuziwakilisha nchi za bara la Afrika.

Kenyatta amesema kuwa umoja wa nchi za Afrika ni alama inayoonesha imani kwa nchi hiyo katika uwezo wao wa kuliwakilisha bara la Afrika kimataifa.

Kenya imeshinda imeshinda uwakilishi huo kwa kupata kura 37 dhidi ya kura 13 walizopata Djibouti's uchaguzi uliofanywa na wanachama na wawakilishi wa umoja wa Afrika leo mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Rais Kenyatta ameeleza kufurahishwa na ushindi huo kwa mwaka 2020/2021 na kuahidi kushirikiana katika kudumisha amani na ulinzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...