Na.Khadija seif, Michuzi tv
MKONGWE wa Tasnia ya filamu Mohammed Fungafunga a.k.a Jengua aamrekana wazi wazi kushuka kwa soko la filamu nchini..
Jengua amesema soko bado lipo ila linakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo swala la filamu kubeba dhima moja inajirudia mara kwa mara ya Mapenzi na kutoleta utofauti katika utunzi wa kazi za Sanaa.
" Wasanii wazuri wapo na kazi za sanaa zipo zinafanya vizuri kutokana na kupata wadau wapya wanaipeleka tasnia hi kimataifa Kama kuwepo kwa tuzo za sinema zetu pamoja na tuzo mbalimbali zinazotambua mchango wa tasnia ya filamu,"
Aidha, ameeleza kuwa ili tufike mbali ni lazima soko liboreshwe kuanzia kuboreshwa kwa uvaaji wa uhusika (acting) pamoja na utungaji wa miongozo (script) pamoja kuhariri picha jongefu.
Pia amesema ni wakati wa wasanii kujitambua na kuiheshimu tasnia ya filamu kwani walikuepo waasisi ambao ndio waliofanya baadhi ya wasanii wasasa kufata nyayo zao.
"Mama Ambiliki,Mzee pwagu,kipara wametangulia mbele ya haki lakini ni baadhi ya watu ambao waliheshimu Sanaa hii na kutupa hamasa wakina sisi kuingia kwenye kazi hiyo,"
Jengua amewataka wasanii chipukizi na waliobobea kuacha kujiona kwani imekua ngumu kwao wakongwe wa tasnia hi hasa wazee kutoa maarifa au kutoa ushauri katika kutengeneza kitu kizuri kutokana na kuonekana hawana jipya kwa sasa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...