Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe katikati akikagua baadhi ya malighafi ambazo zimekwishawasili zitakazotumika katika ujenzi wa kivuko kipya kitakachotoa huduma kati ya Mafia na Nyamisati. Ujenzi huo utagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 5.3 za kitanzania na unatarajiwa kukamilika ifikaapo mwezi Februari mwaka 2020.






Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe katikati akisistiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari, wafanyakazi wa kampuni ya Ms. Songoro Marine pamoja na TEMESA alipokuwa akifanya ukaguzi wa eneo la mradi wa ujenzi wa kivuko kipya ambacho kinatarajiwa kutoa huduma kati ya Nyamisati na Mafia. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Mhandisi Japhet Maselle na kulia ni Mbunge wa Mafia Mh. Mbaraka Dau.


Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Mhandisi Japhet Maselle akisoma taarifa fupi ya mradi wa ujenzi wa kivuko kipya cha Mafia Nyamisati iliyowasilishwa kwa Waziri wa Ujenzi Mh. Isack Kamwelwe wa pili kulia alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa kivuko hicho utakaofanyika katika eneo la Kigamboni. Kulia ni Mbunge wa Mafia Mh. Mbaraka Dau.


Mbunge wa Mafia Mh. Mbaraka Dau aliyenyoosha mkono akimuonyesha Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe katikati michoro itakayotumika katika ujenzi wa kivuko kipya cha Mafia Nyamisati wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa eneo la mradi wa ujenzi huo ambao utagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 5.3 za kitanzania, kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Mhandisi Japhet Maselle. Zoezi hili limefanyika katika eneo la Kigamboni Dar es Salaam.

PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO (TEMESA)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...