Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania(TAEC) Profesa Lazaro Busagala akibadilishana mkataba wa muendelezo wa ujenzi wa awamu ya pili ya ujenzi wa maabara ya TAEC, ujenzi wenye thamani ya shilingi Bilioni 10,447,749,433.24 na Mkurugenzi wa Kampuni ya M/S LI JUN DEVELOPMENT COMPANY LTD. maabara hiyo itajengwa kwenye makao makuu ya TAEC yaliyopo Njiro jijini Arusha 


Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) imesaini mkataba wa shilingi bilioni 10,447,749,423.24 na kampuni ya ujenzi ya M/S LI JUN DEVELOPMENT CONSTRUCTION LTD kwa ajili ya ujenzi wa awamu ya pili maabara ya kisasa. 

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) Profesa Lazaro Busagala ameitaka kampuni hiyo kuhakikisha inajenga maabara hiyo kwa kiwango cha hali ya juu kulingana na makubaliano ya mkataba husika. 

Maabara hiyo ni mwendelezo wa maabara ya awamu ya kwanza iliyozinduliwa mwezi April mwaka huu na Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa. Ujenzi huu wa maabara ni juhudi zingine za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kuendelea kuleta maendeleo nchini. 

Imetolewana; 

Peter G. Ngamilo 
Mkuuwa Kitengo cha Mawasiliano 
Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...