Banki ya CRDB leo imekutana na baadhi ya Watoa huduma ya Uwakala wa Benki hiyo na kufanya  nao kongamano lililoambatana na hafla fupi ikiwa ni muendelezo wa kuadhimisha Mwezi wa Huduma kwa wateja. Pichani ni baadhi wa Mawakala wa Benki hiyo, wakikata keki kama ishara ya kujipongeza kwa huduma bora za kifedha zinazotolewa na mawakala hao, wanaoshuhudia ni Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, Cornell Meseyeck (kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Uwanala wa Kibenki wa Benki ya CRDB, Ericky Willy (katikati) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Yolanda Uriyo (kulia).
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, Cornell Meseyeck akizungumza katika hafla fupi iliyoandaliwa maalum kwa baadhi ya Mawakala wa Benki ya CRDB, ikiwa ni muendelezo wa kuadhimisha Mwezi wa Huduma kwa wateja, iliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Uwakala wa Kibenki wa Benki ya CRDB, Ericky Willyakizungumza katika hafla fupi iliyoandaliwa maalum kwa baadhi ya Mawakala wa Benki ya CRDB, ikiwa ni muendelezo wa kuadhimisha Mwezi wa Huduma kwa wateja, iliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Yolanda Uriyo akizungumza katika hafla hiyo.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...