Na.Khadija seif, Michuzi TV
TAMTHIlIA pendwa ya wildflower msimu wa pili inarudi tena kwa kishindo kuanzia Octoba 14 mwaka huu.

Tamthilia hiyo itarushwa moja kwa moja kupitia King'amuzi cha startimes chaneli ya ST swahili saa 4 usiku kila siku ya jumatatu hadi ijumaa.

Maudhui ya tamthilia hiyo inamzungumzia mwanadada lily cruz ambae anarejea poblacion ardiente ili kulipiza kisasi cha wazazi wake ambao ni Dante na calmia ambao waliuawa na familia ya Julia Ardiente.

"Baada ya kunusurika kifo lily akutana na mwanamke tajiri prianka baada ya kufanikiwa na kuachiwa na wauaji, prianka akamchukua lily na kumbadilisha kila kitu kuhusu yeye na kuwa na utambulisho mpya wa ivy Kama vile mtoto wake.

Baada ya miaka kumi na tatu ivy anagundua kuwa mama yake hakuuwawa,baada ya msako mkali ivy alifanikiwa kumuona mama yake, lakini mama yake anagundua kuwa ana matatizo ya kupoteza kumbukumbu ambapo ivy alifanikiwa kumchukua na kumsaidia kurudisha kumbukumbu zake.

Huku ivy alikua kijana machachari na kufanikiwa kumteka kimapenzi kijana arnado,arnado alichanganyikiwa na penzi la ivy lakini lengo la ivy lilikua ni kuanika maovu ya arnado na asiweze kuolewa nae.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...