Baadhi ya watumishi wa Idara ya uhamiaji ,Wahifadhi pamoja na watumishi wa Mega Group wakiwa kwenye eneo la hifadhi ya Tarangire wakati walipotembelea hifadhi hiyo kuhamasisha utalii wa ndani


Na Vero Ignatus,Arusha.

Katika kuhamasisha utalii wa ndani nchini Idara ya Uhamiaji mkoa wa Arusha imeshiriki kutembelea hifadhi hifadhi ya Taifa ya Tarangire ambapo wamejionea vivutio mbalimbali ikiwemo makundi makubwa ya tembo,twiga,pundamilia na vivutio vingine.

Naibu Kamishna Abdallah Towo ni Afisa wa Uhamiaji Mkoa wa Arusha, amesema kuwa wameamua kutembelea hifadhi ikiwa ni moja kati ya njia za kuhamasisha Taasisi nyingine za serikali kujenga utamaduni wa kutembelea hifadhi wakiwa na wafanyakazi wao lengo ikiwa ni kuhimiza ufanisi kazini na kujenga mahusiano bora kazini.

Issa Mlweta ni Mrakibu wa Uhamiaji amesema kuwa Uhamiaji ni wadau wakubwa wa utalii kwani wanawakaribisha watalii wanapoingia na kutoka katika mipaka ikiwa ni pamoja na kuhamasisha utalii na kutangaza vivutio muhimu tulivyonavyo.

Harieli Msaki ni Mhifadhi Mwandamizi Ujirani Mwema hifadhi ya Tarangire ,amesema kuwa hifadhi hiyo inatembelewa na watalii laki moja kila mwaka kutoka nchi za nje huku utalii wa ndani ukiwa chini hivyo ameipongeza uhamiaji na kuzitaka Taasisi nyingine ziige mfano wake.

Hikloch Ogola ni Mkurugenzi wa tafiti na Maendeleo kutoka Mega Media Group ,ambao ni waandaaji wa ziara hiyo amesema kuwa wameanzisha program maalumu ya kuhamasisha taasisi za umma na binafsi kutembelea vivutio vya utalii ili kuinua mapato ya utalii wa ndani na vile vile kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya utalii..

Utalii ni moja kati ya sekta ambazo zinaongoza kwa kuliingizia taifa fedha za geni na kuchangia kiasi cha asilimia 17% katika pato la taifa hivyo juhudi endelevu zinahitajika katika kuhamasisha utalii wa ndani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...