Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (kulia) akizungumza na Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Joaquine De Mello alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
 Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai akisalimiana na Viongozi wa Taasisi ya Vyombo vya habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISA TAN) kabla ya kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Kikao hicho kilihusu ushirikiano wa pamoja kati ya Ofisi ya katibu wa Bunge na MISA TAN
 Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai akizungumza na Viongozi wa Taasisi ya Vyombo vya habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISA TAN) katika kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Kikao hicho kilihusu ushirikiano wa pamoja kati ya Ofisi ya katibu wa Bunge na MISA TAN
Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (katikati) katika picha ya pamoja na Viongozi wa Taasisi ya Vyombo vya habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISA TAN) baada ya kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Kikao hicho kilihusu ushirikiano wa pamoja kati ya Ofisi ya katibu wa Bunge na MISA TAN, ugeni huo ulioongozwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Vyombo vya habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania, Ndg. Gasirigwa Sengiyumva (wa pili kulia)

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...