Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amesema kuwa, ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania ( ATCL), Bombardier Q400 iliyokuwa iwasili nchini hivi karibuni, inashikiliwa nchini Canada na kesi ipo mahakamani.
Akizungumza jijini Dodoma wakati wa hafla ya kuwaapisha Mabalozi mbalimbali, Waziri Kabudi amesema kuwa, ndege hiyo inashikiliwa baada ya kufunguliwa kwa kesi mpya, kesi ambayo imefunguliwa na Mkulima aliyeshindwa Kesi aliyoifungua nchini Afrika Kusini.
Profesa Kabudi ameongeza kuwa, Serikali imekasirishwa na vitendo vya ndege zake kushikiliwa nchini Canada, na kwamba tayari amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Canada hapa nchini kumueleza kuhusu jambo hilo.
Waziri Kabudi pia ametumia hafla hiyo kuwataka Mabalozi hao wanaokwenda kuiwakilisha Tanzania kwenye Mataifa mbalimbali, kwenda kusimamia vizuri matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali, kwa kuwa kumekua na matumizi mabaya ya fedha kwenye Ofisi za Ubalozi.
Ametolea mfano Ubalozi wa Tanzania huko Addis Ababa - Ethiopia ambapo kumekua na ubadhirifu mkubwa na fedha na kuongeza kuwa kwa sasa Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) inaendelea na uchunguzi.
Katika hafla hiyo, Rais John Magufuli amewaapisha Mabalozi Watano ambao wanakwenda kuiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...