Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto anayeshugulikia Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu akizungumza na wadau wa Sekta ya ajira kutoka Sekata za umma, binafsi na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali wakati akifungua jukwaa la majadiliano la wadau kuhusu utekelezaji wa dhana ya uanagenzi  leo jijini Mbeya.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya Mariam Mtunguja akiwasisitiza waajiri wa mkoa wa Mbeya na Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kuwapokea wanafunzi na wahitimu wa vyuo vikuu kwa mafunzo ya uanagenzi wakati wa jukwaa la majadiliano la wadau kuhusu utekelezaji wa dhana ya uanagenzi liliofanyika leo jijini Mbeya.
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Patrick Golwike akifafanua jambo katika jukwaa la majadiliano la wadau kuhusu utekelezaji wa dhana ya uanagenzi  lililofanyika leo jijini Mbeya.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Juma Mnwele akichangia mada katika jukwaa la majadiliano la wadau kuhusu utekelezaji wa dhana ya uanagenzi  liliofanyika leo jijini Mbeya.
Baadhi ya waajiri kutoka Sekta ya Umma, Binafsi na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kutoka mikoa ya Nyanda za Juu Kusini wakisikiliza mada mbalimbali zilizokuwa zinazatolewa katika jukwaa la majadiliano la wadau kuhusu utekelezaji wa dhana ya uanagenzi  liliofanyika leo jijini Mbeya.
Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW
*********************************
Na Mwandishi Wetu Mbeya
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto anayeshugulikia Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu amesema kuwa dhana  Uanagenzi ni suluhisho la kuhakikisha mifumo yetu ya elimu inazalisha wataalamu mahiri wenye ujuzi au stadi zinazohitajika katika soko la ajira kwenye uchumi wa viwanda.
Dkt. Jingu amesema hayo leo jiji ni Mbeya wakati wa akifungua Jukwaa la majadiliano la wadau kuhusu utekelezaji wa dhana ya uanagenzi lililofanyika katika ukumbi wa Benjamin Mkapa mkoani Mbeya.  
Dkt. Jingu amesema kuwa Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Joseph Pombe Magufuli imedhamiria kuwa na nchi yenye uchumi wa kati wa viwanda kufikia mwaka 2025 na ujenzi wa Tanzania ya viwanda unahitaji waajiriwa wenye stadi zinazohitajika na soko la ajira kwenye sekta isiyo rasmi na rasmi.
“Hali ilivyo sasa kuna tofauti kubwa kati elimu wanayopatiwa wahitimu wa fani mbali mbali nchini na ujuzi au stadi zinazohitajika na soko la ajira alisema Dkt. Jingu
Ameongeza kuwa Serikali imeona umuhimu wa kushughulikia changamoto ya kuzalisha wahitimu wasioajirika kwenye sekta rasmi na isiyo rasmi kwa kuanzisha dhana ya uanagenzi kwenye Taasisi na vyuo vya Maendeleo ya Jamii itakayosaidia kupata wataalam wenye ubora unaohitajika.
Dkt. Jingu amesisitiza kupitia Mifano ya nchi za Ujerumani na Rwanda ikionesha kuwa uanagenzi umewezesha kutoa matokeo chanya na Ujerumani waliingiza dhana hii katika mfumo wa elimu ambapo imesaidia asilimia 60 ya wanafunzi wanaomaliza vyuo kuweza kujiajiri wenyewe kutokana na ujuzi na uzoefu wa kazi wanaoupata wakiwa masomoni kwa kupitia njia hiyo.
Akielezea dhumuni la Jukwaa la majadiliano la wadau kuhusu utekelezaji wa dhana ya uanagenzi Mkurugenzi Msaidizi Vyuo vya Maendeleo ya Jami Neema Ndoboka amesema kuwa lengo kuu ni kuangalia namna ya kuboresha mafunzo kwa vitendo na utekelezaji wa dhana ya uanagenzi katika kuhakikisha wanafunzi na wahitimu wanapata stadi zinazohitajika katika soko la ajira.
Ameongeza kuwa katika kuelekea katika uchumi wa kati wahitimu wa vyuo wanahitajika kama nguvu kazi katika kufikia hilo hivyo Serikali kwa kushirikiana na wadau wa ajira wanajukumu kubwa la kuandaa nguvu kazi hiyo iliyo na weledi na ufanisi katika kutekeleza majukumu yao.
Akitoa salamu za mkoa wa Mbeya, Katibu Tawala wa Mkoa huo Mariam Mtunguja amewasisitiza waajiri wa mkoa huo na Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kuwapokea wanafunzi na wahitimu wa vyuo vikuu hasa vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini ili waweze kupata ujuzi utakaowasaidia kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi pale watakapoajiriwa na kujiajiri.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Juma Mnwele amesema kuwa msisitizo uwekwe kwa Serikali kutoa muongozo kwa Taasisi za Serikali kuwapokea wanafunzi kwa mafunzo kwa vitendo hasa ya uanagenzi katika Taasisi za Serikali.
Naye Mwakilishi wa Shirika la TAHEA Petre Mapunda amesema kuwa Shirkla lake linatekeleza dhana ya uanagenzi kwa kuwapokea wanafunzi na wahitimu wa vyuo mbalimbali katika Shirika lao kwa kufanya kazi kwa muda mrefu na kuwezesha kupata ujuzi na kupata fursa za kuajiriwa na kujiajiri kutokana na ujuzi walioupata.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...