.Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC) Dkt.Sarah Urasa akizungumza na waandishi wa habari na Timu ya Maafisa Habari na Uhusiano wa Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto waliotembelea hospitali hiyo kuangalia mafanikio ya miaka ya minne ya serikali ya awamu ya tano ikiwa ni Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya .
 Mkuu wa Msafara na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Gelald Chami akitoa maelezo kuhusiana na Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya kutembelea kuona mafanikio ya miaka minne ya serikali ya awamu ya tano.
 Daktari Bingwa wa Uzazi wa  Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC ) Benjamin Shayo akieleza kuhusiana uhifadhi ya mbegu za kiume kwa ajili ya watu wenye tatizo la uzazi namna walivyofanikiwa mara baada ya kuuza kutoa huduma hiyo.

 Sehemu ya Mitungi ya Gesi  ya Oksijeni ambayo inazalishwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC).

 Fundi wa Vifaa vya Tiba Dustan Kanza akizungumza na waandishi wa habari namna wanavyofua hewa ya oksijen katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC)

 Fundi wa Viti Mwendo  wa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC) Prosper Kaaya akionesha namna wanavyotengeza viti vya magarudumu matatu kwa ajili ya watu wenye ulemavu.

 Mtaalam wa Afya wa Viungo Bandia wa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC) Sunday Agger  akionesha namna wanavyounda viungo Bandia katika hospitali hiyo.

 Mfamasia wa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC) Faustine Sasi akionesha waandishi wa habari namana wanavyongeza maji tiba katika hospitali hiyo.
.Moja ya Viungo Bandia vinavyozalishwa na hospatali  Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC).

picha ya mtoto aliyeunganishiwa mguu wa bandia ulioundwa na Hospitali ya Rufaa kanda ya Kaskazini (KCMC)
 Picha ya pamoja ya waandishi habari na Timu ya Maafisa Habari na Uhusiano wa Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto watendaji Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC).



*KCMC wanazalisha Hewa ya Oksjeni  kwa watu wenye matatizo ya kupumua
 
Na Chalila Kibuda Globu ya Jamii, Kilimanjaro

Katika kipindi cha Miaka Minne ya utawala wa Rais Dkt.John Pombe Magufuli Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC) imefanya hospitali hiyo kuwa Hospitali ya Viwanda kwa kuzalisha Vifaa tiba na Dawa kutokana uwekezaji wa miundombinu.

Katika Miaka Minne hiyo wameweza kufanikiwa katika kuabzisha Kinu cha kufua hewa ya Oksijen na Nitrojen,Mafuta ya Ngozi kwa watu  wenye Ualbinino,Huduma ya magonjwa ya moja na kuunda baskeli ya magurudumu Matatu, Kutengeneza maji tiba ‘DRIP’pamoja  kuunda viungo bandia bandia.

 Kinu cha kuzalisha Oksijeni na Naitrojeni  kinauwezo wa kufua hewa ya oksijeni ambayo kwa kiwango kikubwa hutumika kuwasaidia watu wenye matatizo ya kupumua ambapo kwa siku wanazalisha mitungi 400 hufuliwa katika kinu hicho.

Akizungumza  na waandishi wa habari na Timu ya Maafisa Habari na Uhusiano wa Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  , Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC) , Dkt. Sarah Urasa amesema kuwa mafanikio walioyapata hayo wameweza kutoa huduma kwa bora za matibabu kwa wananchi.
 
Amesema hospitali hiyo ni  ya kwanza kuwa na kinu ya kufua hewa ya oksijeni na Nitrogen  hapa nchini,hewa ya oksijeni pia inatumika kwa wale wagonjwa wanaopewa dawa za usingizi kwaajili ya upasuaji ,hewa ya nitrogen inatumika kuhifadhi sampuli kutoka kwa wagonjwa,tiba kwa magonjwa ya ngozi vile vile hutumika kukata matokeo kwenye ngozi au kwenye viungo vya uzazi"alisema.
  
 Dkt.Urasa  amesema ununuzi wa mitungi ya gesi ya oksijeni pekee ulikuwa inaigharimu Hospitali  zaidi ya sh. milioni tatu kwa wiki hatua ambayo imeokoa gaharama za uendeshaji hospitalini hapo na fedha iliyookolewa inafanya masuala mengine ya hospitali na kuongeza kuwa  kadiri uzalishaji unavyoongezeka katika kinu hicho wataanza kutumia mfumo wa kuunganisha gesi moja kwa moja hadi kwenda  kitanda cha mgonjwa.

Amesema  wameanza kuhifadhi mbegu za kiume kwa watu wenye matatizo ya uzazi ambayo huwahudumia wagonjwa kwa wiki mara moja  ambapo huwahudumia watu 10 mpaka 12 kwa siku na wajo mbioni kuanzisha kliniki kwa wiki mara mmoja kwa watu wenye matatizo hayo.

Dkt.Urasa  alisema katika Utawala wa Rais Dkt.John Magufuli wamefanikiwa kuanza kutengeneza maji tiba 'dripu' kwaajili ya kuwasaidia wagonjwa ndani na nje ya hospitali na kusaidia kiwango kikubwa hata hospitali zingine zimekuwa zikifika hapa kwaajili ua kujifunza namna ya kutengeneza maji tiba

Pia amesema KCMC ndio kituo pekee inayotambulika kimaitafa kutoa mafunzo ya magonjwa ya ngozi na zinaa kwa nchi zote za Afrika Mashariki ambapo KCMC ndio Kituo hikinachozalisha mafuta ya ngozi kwaajili ya watu wenye ualbino na tayari wameingia makubaliano na Bohari kuu ya Dawa (MSD) kwaajili ya kusambaza mafuta hayo tayari wamefikia mikoa 25 kwa kutumia mfumo wetu wa usambazaji na sasa MSD watatuongezea nguvu ili kusambazwa nchi mzima "alisema

Akizungumzia matumizi ya mitungi ya gesi kwa mgonjwa Mhandisi KCMC  Dustan Kanza alisema kwa wa mgonjwa mmoja hutumia mtungi mmoja lengo kuepukana na maambukizi na kuongeza kuwa kinu hicho kwa saa 24 inauwezo wa kuzalisha mitungi 400 na mpaka sasa tayari zaidi ya mitungi 600 imezalishwa tangu kuanza kufanya kazi kwa kinu hicho januari mwaka huu. 

Kwa upande wake Meneja Uzalishaji kitengo Idara ya ngozi Ebeneza Fabian alisema wanawafikia watu 6500 wenye mahitaji ya dawa za ngozi huku idadi ya watu wenye ualbino ikiwa takriban 25,000 akitaja changamoto kuwa ni upatikaji wa malighafi ya kutengenezea mafuta hayo na Mafunzo ya ufuaji wa gesi hizo zimesimamiwa na mtaalamu kutoka Nchini India ikiwa ndio wauzaji wa mitambo hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...