Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii
MSANII Godfrey Tumaini alimaarufu kama Dudubaya, amefutiwa usajili wa kutojuhusisha
na shughuli zozote za sanaa hapa nchini kuanzia leo (Januari 7, 2020).
Hayo yameelewa katika taarifa iliyotolewa na katibu mtendaji wa Baraza la
sanaa la Taifa(BASATA), Godfrey Mngereza leo jijini Dar es Salaam.
Hatua hiyo imechukuliwa na Baraza la sanaa la Taifa (BASATA) baada ya kukataa wito ambao baraza hilo
lilimtaka kufika katika ofisi zake zilizopo Ilala Sharif Shamba jijijini Dar es
Salaam.
Msaanii huyo aliitwa na BASATA kutokana na alichokizungumza kuhusiana na
wasanii na sekta ya sanaa kupitia mitandao ya kijamii kwa makusudi amekaidi
wito huo.
Hata hivyo BASATA imesema kuwa haiwezi kuvumilia wasanii wachache wanaotaka
kuigeuza sekta ya sanaa, kwa kutumia maneno yasiyo ya staha na Lugha chafu
mbele ya jamii.
“BASATA haita kuvumilia wasanii wachache wanaotaka kuigeuza sekta ya sanaa
kwa kutumia maneno yasiyo na staha na Lugha chafu mbele kwa jamii.”
BASATA imetoa onyo kwa taasisi, kampuni na mtu yeyote kutokufanya kazi na
msaanii huyo kwani amekaidi agizo la baraza linaloshughulikia masuala ya sanaa
na wasanii hapa nchini.
Baraza linawakumbusha wasanii na wadau wote wa sanaa nchini kufanya kazi
kwa weredi kwa kuzingatia sheria, kanuni taratibu na miongozo inayosimamia
sekta ya sanaa nchini pamoja na kuzingatia sheria za nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...