Timu ya Gwambina ya Misungwi ya Mwanza imejigamba kuifunga timu ya AFC ya Arusha kwenye mapambano mkali wa ligi daraja la kwanza utakaofanyika leo jumamosi ya Januari 18 kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. 

Kocha wa Gwambina, Fulgence Novatus alisema wamejiandaa ipasavyo kuifunga AFC kama walivyowafunga mabao 3-0 walipocheza nao Mwanza. 

Novatus alisema Gwambina imeshazifunga timu kwao baadhi ya timu hivyo AFC watarajie kipigo jijini Arusha japokuwa hawajawahi kufungwa au kutoka sare jijini Arusha. 

"Timu za Mashujaa na Rhino zilikuwa hazijawahi kufungwa nyumbani kwao lakini sisi Gwambina tuliwafunga kwao hivyo AFC atarajie kipigo tena nyumbani kwao," alisema Novatus. 

Alisema vijana wake wana morali ya hali ya juu katika mpambano huo hivyo wanatarajia ushindi tuu bila wasiwasi wowote ule. 

Hata hivyo, kocha wa timu ya AFC Ulimboka Mwakingwe alisema anatarajia watashinda mpambano huo ili kulipiza kisasi kwa timu hiyo. 

Mwakingwe alisema AFC ya sasa siyo ile iliyofungwa mabao 3-0 na Gwambina kwenye mchezo wao wa awali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...