Timu
ya Gwambina ya Misungwi ya Mwanza imejigamba kuifunga timu ya AFC ya
Arusha kwenye mapambano mkali wa ligi daraja la kwanza utakaofanyika leo
jumamosi ya Januari 18 kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini
Arusha.
Kocha wa
Gwambina, Fulgence Novatus alisema wamejiandaa ipasavyo kuifunga AFC
kama walivyowafunga mabao 3-0 walipocheza nao Mwanza.
Novatus
alisema Gwambina imeshazifunga timu kwao baadhi ya timu hivyo AFC
watarajie kipigo jijini Arusha japokuwa hawajawahi kufungwa au kutoka
sare jijini Arusha.
"Timu
za Mashujaa na Rhino zilikuwa hazijawahi kufungwa nyumbani kwao lakini
sisi Gwambina tuliwafunga kwao hivyo AFC atarajie kipigo tena nyumbani
kwao," alisema Novatus.
Alisema vijana wake wana morali ya hali ya juu katika mpambano huo hivyo wanatarajia ushindi tuu bila wasiwasi wowote ule.
Hata
hivyo, kocha wa timu ya AFC Ulimboka Mwakingwe alisema anatarajia
watashinda mpambano huo ili kulipiza kisasi kwa timu hiyo.
Mwakingwe alisema AFC ya sasa siyo ile iliyofungwa mabao 3-0 na Gwambina kwenye mchezo wao wa awali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...