Mratibu na Msimamizi Mkuu wa miradi ya ujenzi ambayo inatekelezwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi jijini Dodoma, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP Costantine Kiwone, akimweleza Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Ramadhani Kailima (katikati) na Maofisa wengine hatua mbalimbali za ujenzi wa nyumba za askari, Makao Makuu ya Polisi na makazi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) jijini Dodoma jana.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima (katikati), akitoa maelekezo kwa Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Mbaraka Semwanza (kulia) na Mkurugenzi wa Utawala na Rasirimali Watu, Emmanuel Kayuni (wa pili kulia) baada ya kufanya ukaguzi katika ujenzi wa majengo ya jeshi hilo jijini Dodoma jana.  Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Kushughulikia Malalamiko, CP Albert Nyamhanga.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima (kulia), akiwa na Wakurugenzi na Maofisa wa Wizara hiyo akisisitiza jambo kwa Maofisa wa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Mkoa wa Dodoma, alipofanya ziara ili kuangalia utendaji kazi na huduma zinavyotolewa kwa wananchi. 

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima, akisalimiana na baadhi ya Maofisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, kabla ya kukagua ujenzi wa Makao Makuu ya Jeshi hilo ambao unaendelea jijini Dodoma.

PICHA NA VERONICA MWAFISI-MOHA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...