Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally atakuwa na ziara ya kikazi ya siku tatu Mkoani Kigoma kuanzia leo Januari 17 - 19, 2020.

Leo Januari 17 ,2020, Katibu Mkuu anatarajiwa kuwasili Uwanja wa ndege Kigoma Mjini kuelekea moja kwa moja wilayani Uvinza kata ya Kazuramimba ambapo atazungumza na wajumbe wote wa mkutano Mkuu wilaya ya Uvinza, Wazee, mabalozi, viongozi wa kata na matawi pamoja na mabaraza ya jumuiya zote wilayani hapo.

Aidha hapo kesho Januari 18,2020 Katibu Mkuu anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Mkutano Mkuu maalum wa kupokea taarifa ya kazi za Mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini wilayani Kigoma.

Atamalizia kwa kikao cha mabalozi wote wilaya ya Kigoma kesho kutwa tarehe 19 Januari, ambapo Katibu Mkuu atagawa vitambulisho kwa mabalozi wa wilaya hiyo ikiwa ni mfano kwa mabalozi wote nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...