Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa
na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akizungumza na viongozi wa Mkoa wa
Manyara katika mkutano wa Mkuu wa Mkoa huo Mhe.Alexandar Mnyeti
uliokuwa na lengo la kuboresha Sekta ya elimu mkoani hapo wakati Waziri
alipokua kwenye ziara ya kukagua mitambo ya usikivu ya TBC iliyopo
Mkoani hapo eneo la Gitsimii pamoja na kuzungumza na wadau wa tasnia ya
habari Januari 23,2020.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara
Mhe.Alexandar Mnyeti akizungumza na viongozi wa Mkoa huo katika kikao
cha kujadili maendeleo ya elimu na namna ya kuboresha ufaulu wa
wanafunzi wa mkoa huo uliofanyika Januari 23,2020.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa
na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa
Manyara Mhe.Alexandar Mnyeti alopokua akiwasilisha taarifa ya mkoa
kuhusu usikivu wa TBC katika ziara yake ya kukagua mitambo ya usikivu
iliyopo Gitsmii pamoja na kuzungumza na wadau wa tasnia ya habari mkoani
hapo Januari 23,2020.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la
Utangazaji Tanzania (TBC) akizungumza na wadau wa tasnia ya habari wa
Mkoa wa Manyara(hawapo pichani) katika kikao cha Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe(kushoto)
kilichokua na lengo la kusikiliza na kutatua changamoto wanazokutana
nazo katika kutekeleza majukumu yao. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa
Idara ya Habari –MAELEZO Bw.Rodney Thadeus.
……
Na Shamimu Nyaki –WHUSM,Manyara.
Serikali imeanza kuhamisha mitambo
ya Usikivu ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kutoka katika jengo
la Mkoa wa Manyara kupeleka katika eneo la Gitsmii ambalo lina mwinuko
utakaosaidia kuimarisha usikivu katika mkoa huo.
Hayo yamesemwa na Waziri wa
Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo alipofanya ziara katika mkoa huo jana
Januari 23,2020 ya kukagua mitambo hiyo ambayo imekua na changamoto ya
kutosikika vizuri katika maeneo mengi ndani ya mkoa huo.
“Tunafahamu changamoto ya usikivu
wa TBC hapa Manyara ndio maana nimekuja pamoja na wataalam kuona namna
ya kutatua changamoto hiyo na tayari tumeshaanza mpango wa kuhamisha
mitambo kupeleka eneo waliloshauri wataalam wetu kwamba litaimarisha
usikivu katika mkoa huu”alisema Dkt.Mwakyembe.
Awali Mkurugenzi Mkuu wa Shirika
hilo Dkt.Ayoub Ryoba amesema kuwa tayari ofisi imeagiza mtambo wa “Wats”
2000 ambao ndio unaotakiwa kuwekwa katika eneo hilo ili matangazo ya
TBC yawafikie watu wengi wa mkoa wa manyara na maeneo jirani.
“TBC ni chombo cha umma lazima
kiwafikie wananchi wote ndio maana tunaendelea kuimarisha usikivu katika
maeneo mbalimbali na mpaka sasa tumeshafikia asilimia zaidi ya
70”alisema Dkt Ryoba.
Wakati huo huo.Dkt Mwakyembe
ameuagiza Mkoa huo kushirikiana na TANROADS pamoja na TANESCO
kutengeneza barabara inayoelekea sehemu iliyosimikwa mitambo hiyo pamoja
na umeme na maji kwakua ni miundombinu muhimu inayohitajika katika
eneo hilo.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Manyara
Mhe.Alexandar Mnyeti amesema kuwa wananchi wamekua wakilalamika kukosa
matangazo ya TBC lakini Serikali imatambua hilo na imeanza kulifanyia
kazi.
“Katika Sekta ya Utamaduni na
Michezo Mkoa huu unafanya vizuri sana hasa katika michezo ya riadha na
uhifadhi wa mila na desturi changamoto kubwa ni usikivu wa TBC redio ni
hafifu mno tunaamini ujio huu utaleta matokeo mazuri hivi
karibuni”alisema Mhe.Mnyeti.
Katika hatua nyingine Waziri
Mwakyembe amewasisitiza waandishi wa habari wa mkoa huo kufanya kazi yao
kwa weledi na uadilifu kuzingatia Sheria ya Huduma za Habari na Sheria
ya upatikanaji wa habari,ambapo amewasisitiza kuwa mwisho wa uandishi wa
mtaani ni Desema 2021.
Mhe.Waziri ameongeza kuwa kazi ya
uandishi wa habari ni taaluma kama taaluma nyingine hivyo wanapaswa
kuhakikisha wanafuata misingi ya taaluma hiyo ikiwemo kutoa habari kwa
usahihi na kwa wakati sahihi pamoja na kutumia vyanzo sahihi.
Hata hivyo Mhe.Waziri alipata
nafasi ya kuzungumza na viongozi wa Mkoa huo katika kikao
kilichoandaliwa na Mkuu wa Mkoa Mhe.Alexandar Mnyeti kilichokua na lengo
la kuimarisha sekta ya elimu pamoja na ufaulu wa wanafunzi wa mkoa huo
ambapo amewataka viongozi hao kutorudi nyuma katika kuendeleza elimu kwa
vijana walioko shuleni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...