Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi
Joseph Sokoine akifungua semina iliyoandaliwa na Ofisi hiyo kwa wajumbe
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira leo
Januari 25, 2020 jijini Dodoma ya kuwajengea uwezo kuhusu mada
mbalimbali zikiwemo Umuhimu wa uhandisi jeni katika kuongeza tija katika
kilimo, Fursa za teknolojia ya kisasa kwenye afya, Usimamizi wa
matumizi salama ya bioteknolojia ya kisasa na Matumizi ya bioteknolojia
ya kisasa kwa maendeleo ya mifugo na afya, fursa na changamoto zake.
Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira katika Ofisi hiyo, Faraja
Ngerageza.
Mhadhiri Idara ya Biolojia ya
Molekyuli na Bayoteknolojia Ndaki ya Sayansi Asilia na Tumizi ya Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Daniel Maeda akiwasilisha mada Matumizi ya
bioteknolojia ya kisasa kwa maendeleo ya mifugo na afya, fursa na
changamoto zake katika semina kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya bunge
ya Viwanda, Biashara na Mazingira iliyofanyika leo jijini Dodoma na
kuandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais.
Afisa Mazingira Mwandamizi Ofisi
ya Makamu wa Rais, Thomas Chali akitoa mada kuhusu Usimamizi wa matumizi
salama ya biotechnolojia ya kisasa katika semina kwa wajumbe wa Kamati
ya Kudumu ya bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira iliyofanyika leo
jijini Dodoma na kuandaliwa na Ofisi hiyo.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira wakiwa katika semina kuhusu
Umuhimu wa uhandisi jeni katika kuongeza tija katika kilimo, Fursa za
teknolojia ya kisasa kwenye afya, Usimamizi wa matumizi salama ya
biotechnolojia ya kisasa na Matumizi ya bioteknolojia ya kisasa kwa
maendeleo ya mifugo na afya, fursa na changamoto zake kilkiyofanyika
jijini Dodoma na kuandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais.
Sehemu hiya wataalamu kutoka Ofisi
ya Makamu wa Rais wakifuatilia semina iliyoandaliwa kwa wajumbe wa
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira. (PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...