Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu wa
Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Bw. Matias Haule akitoa
ufafanuzi kuhusu maambukizi ya mapya ya UKIMWI kwa wanafunzi wa Shule ya
Msingi Mininngani iliyoko Kondoa Mjini Mkoani Dodoma.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi
Miningani iliyoko nje kidogo ya mji wa Kondoa wakisiliza kwa amakini
mafunzo ya maambukizi ya UKIMWI kwa Vijana jana Kondoa Mkoani Dodoma.
*******************************
Na mwandishi wetu Kondoa
Wazee Wilayani
Kondoa wameiomba Serikali kudhibiti picha zenye maudhui ya ngono katika
mitandao ya Kijamii kwa lengo la kusaidia kupunguza maambukizi mapya ya
UKIMWI kwani picha hizo zisizo kuwa na maadili zinawachochea
vijana kujiingiza katika matendo yanayosababisha maambukizi ya UKIMWI.
Wazee hao
waliyasema hayo wakati wa mafunzo ya Siku moja kwa wazee wa mila pamoja
na viongozi wa dini yaliyoandaliwa na Wizara ya Afya Idara Kuu
Maendelepo ya Jamii kwa lengo la kuwafundisha kuhusu ukubwa watatizo la
UKIMWI kwa vijana na kuwataka kusaidia kupambana na tatizo hilo katika
jamii kupitia nafasi zao.
Mzee Mohamed
Hussein Kola akitoa maoni yake katika kikao hicho alisema hata Siku
mmoja hakuna mtu aliyefikishwa mbele ya sheria kwa mtu kuambukiza
mwenzake UKIMWI kwa makusudi pamoja na uwepo wa sheria ya UKIMWI hapa
Nchini.
Mzee Kola
anaangazia pia suala la malezi na kusema kwamba vijana hawaeshimu tena
mawazo ya wazee na kudai kuwa kila mzee akitoa maoni yake vijana
wanasema mawazo ya mzee nayo yamepitwa na wakati na kudai kuwa hata kwa
baadhi ya mafunzo ya magonjwa mbalimbali yanapotolewa wazee wamekuwa
hawashirikishwi.
Mzee Haruna
Ramadhani Dodi pia aliongeza kuwa vijana wadanganyana kupuuza uwepo wa
maambukizi ya UKIMWI na kudai kuwa watakufa kishujaa uku akiwataka
kupuuza mawazo haya kwani hakuna mtu aliyewai kufa kishujaa na kuonya
pia juu ya uwepo wa maeneo ya biashara za kumbi za starehe kuwa
zinachangia uwepo wa maambukizi.
Taarifa hizi kwa
wazee hao zilikuwa za kushtua kwani idadi ya maambukizi kwa vijana
inazidi kupaa na hii ilizibitishwa na Afisa Maendeleo Mkuu kutoka Wizara
ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Matias Haule aliyesema kuwa
watanzania 200 wanapata maambukizi mapya kwa siku.
Aidha Bw. Haule
alitoa takwimu hizo na kuongeza kuwa maabukizi haya kwa mwaka ni kiasi
cha watu elfu 72 akiitaja idadi ya watu inayoambukizwa kwa mwezi kuwa
watu elfu 6,000 na kushangaza wazee hao kwa kusema kwa vijana wenye umri
kati ya miaka 15-24 maambukizi mapya kwao 79 na kati yao wasichana
wanaombukizwa ni 63 hivyo idadi kubwa ya wasichana inaambukizwa
ukilinganisha na wavulana.
Wizara ya Afya
Maendealeo ya Jamii kwa Kushirikiana na TACAIDS pamoja na Shirika la
TASAF wako Mkoani Dodoma kutembelea wasichana barehe na wanawake vijana
pamoja na Shule mbalimbali Mkoani humo kwa lengo la kuhamasisha vijana
juu yatishio jipya la maambukizi ya UKIMWI kwa vijana na zoezi hili
litaendelea kwa Mkoa wa Morogoro na baadae Nchi Nzima.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...