Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya watu wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa akizungumza mara baada ya kutembelea vivutio vya Magofu ya Kale yaliyopo mji Mkongwe, Bagamoyo -Pwani huku akiwa ameongozana na wabunge wenzake wenye ulemavu ziara iliyokuwa imeratibiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).
Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Mashariki Bi. Caroline Malundo akiwakaribisha wabunge wenye ulemavu mara baada ya kutembelea katika eneo la Mji Mkongwe, Bagamoyo ambapo kuna vivutio vya magofu ya kale. Wabunge hao walikuwa kwenye ziara iliyokuwa imeratibiwa na TFS. Wengine katika picha ni wafanyakazi wa TFS.
Wabunge wenye Ulemavu wakipatiwa maelezo ya historia ya Mji Mkongwe mara baada ya kuwasili kujionea vivutio vya eneo hilo.
Katibu wa Chama cha Wabunge wenye Ulemavu Mhe. Amina Mollel akitoa machache.
Mbunge wa Ulyankulu, Tabora Mhe. John Kadutu (kulia) akizungumza neno mara baada ya kukaribishwa na na Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mhe. Amina Mollel wakati wa ziara yao ya utalii mjini Bagamoyo - Pwani.
Wafanyakazi wa TFS wakifuatilia.
Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge wenye Ulemavu Mhe. Riziki Lulida ambaye ni mmoja ya mabalozi wa Utalii akitoa shukrani zake kwa TFS kwa namna ilivyoweza kuwapokea na kuwakarimu wakati wa ziara yao ya utalii mjini Bagamoyo - Pwani.
Muongoza watalii Bw. Cathbert akitoa maelezo kwa wabunge waliofika kutembelea vivutio vya mji mkongwe Bagamoyo - Pwani.
Muongoza watalii Bw. Cathbert akitoa maelezo juu ya vivutio vya mji mkongwe Bagamoyo - Pwani.
Moja ya kibao.
Boma ya Wajerumani iliyojengwa mwaka 1897 katika mji Mkongwe Bagamoyo - Pwani.
Boti zikisubiri mzigo kuelekea Zanzibar kutokea mji wa Bagamoyo - Pwani.
Wavuvi wakielekea kuvua samaki katika Bahari ya Hindi.
Shughuli za kuandaa chombo zikiendelea.
Wachuuzi wa vinyago wakionyesha biashara zao.
Mbunge wa Ulyankulu, Tabora Mhe. John Kadutu (kushoto) na Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mhe. Amina Mollel akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili katika eneo la Magofu ya Kale yaliyopo mji mkongwe, Bagamoyo - Pwani.
Meneja wa Wakala wa Huduma za Misiti Tanzania (TFS) Kanda ya Mashariki Bi. Caroline Malundo akizungumza na wanahabari.
Bango linaloelezea kwa ufupi mji wa Kaole, Bagamoyo - Pwani.
Wageni kutoka mataifa mbali mbali wakipata maelezo mara baada ya kutembelea mji wa Kaole, Bagamoyo - Pwani.
Meneja wa Wakala wa Huduma za Misiti Tanzania (TFS) Kanda ya Mashariki Bi. Caroline Malundo (kushoto) akizungumza na wageni aliwakuta eneo la Kaole Bagamoyo-Pwani.
Muongoza watalii akitoa maelezo kwa wageni.
Moja ya msikiti ambao ni kivutio katika mji wa Kaole, Bagamoyo - Pwani.
Makaburi.
Moja ya kaburi lenye mnara refu kuliko yote.
Mbunge wa Ulyankulu, Tabora Mhe. John Kadutu akinawa maji ya baraka katika kisima kilichopo mji wa Kaole ambapo kisima hicho hutoa maji kwa mwaka mzima bila kukata. Inasemakana maji hayo huondoa mikosi na kuwapatia watu baraka.
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mhe. Amina Mollel (mwenye kilemba) akinawa maji ya baraka.
Wabunge wenye ulemavu wakiongozwa na Naibu Waziri Stella Ikupa wakipita kujionea vivutio katika mji wa Kaole, Bagamoyo - Pwani.
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mhe. Amina Mollel akifanya sala katika makaburi ya Kaole, Bagamoyo - Pwani.
Moja ya Bango lililopo katika eneo la Bandari ya Zamani iliyopo Kaole, Bagamoyo - Pwani.
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) akiwa katika kaburi la Sharifu, kaburi hili hutumika katika matambiko mbali mbali ikiwemo kutoa mikosi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...