Na Mwandishi wetu Mihambwe
Afisa
Tarafa Mihambwe Emmanuel Shilatu ameagiza kukamatwa mara moja kwa
Wazazi wanaowazuia ama kutokuwapeleka Watoto wao shule wale ambao
wamefaulu kujiunga na kidato cha kwanza.
Gavana
Shilatu ameyasema hayo wakati akizungumza na Wanafunzi wa shule ya
Sekondari ya Mweminaki iliyopo kata ya Kitama wakati wa ziara yake ya
kutembelea shule zote za Sekondari zilizopo Tarafa ya Mihambwe ambapo
hakuridhishwa na kiwango cha kuripoti shuleni kwa Wanafunzi waliofaulu
kidato cha kwanza.
"Nazungumza
nanyi Wanafunzi ambao mnawajua Wanafunzi wenzenu waliofaulu kidato cha
kwanza na wapo nyumbani. Nendeni mkawaambie Wazazi wao watakaokaidi
kuwapeleka shuleni Watoto wao Serikali itatumia vyombo vyake kuwakamata
wote. Usalama wao wawalete Watoto shule mara moja." Alisema Gavana
Shilatu
Akizungumza na
Mwandishi wetu mara baada ya ziara hiyo Gavana Shilatu alisema sababu
wanazotoa Wazazi za kushindwa kuwapeleka Watoto shule hazina mashiko ni
za kuishi kwa mazoea kutokana na mwamko mdogo uliopo licha ya Serikali
kutoa Elimu bure.
"Mwaka
jana walisema hawana hela hata ya kununua sare za shule kutokana na
malipo ya Korosho kuchelewa, mwaka huu wamelipwa fedha za Korosho kwa
wakati lakini bado hawawapeleki Watoto shule, hapa tatizo si fedha. Sasa
mwendo ni ule ule tutawakamata wote wasiowaleta Watoto shule."
Alisisita Gavana Shilatu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...