Kaimu Katibu Mtendaji wa THBUB akiongea katika kikao kazi kilichofanyika mkoani Morogoro kuanzia Februari 3 – 4, 2020 kwa lengo la kuandaa muongozo utakaotumika kufanya ufuatiliaji na ukaguzi wa Magereza na maeneo mengine walipozuiliwa watu. Kulia ni Kalliopi Kambanella, Mwanasheria kutoka Dignity. Wa kwanza kushoto ni Mkurugunzi kutoka THBUB, Alexander S. Hassan, wa pili kushoto ni Una Marquards-Busk, Meneja  Mradi kutoka DIGNITY na wa tatu ni Kamishna Dkt, Fatuma Rashid Khalfan.
Kamishna Dkt, Fatuma Rashid Khalfan akiongea wakati akifungua kikao kazi kilichofanyika mkoani Morogoro kuanzia Februari 3 – 4, 2020 kwa lengo la kuandaa muongozo utakaotumika kufanya ufuatiliaji na ukaguzi wa Magereza na maeneo mengine walipozuiliwa watu.
Una Marquards-Busk, Meneja  Mradi kutoka DIGNITY akitoa maelezo mafupi kuhusu taasisi ya DIGNITY na lengo la kikao kazi hicho.
Kamishna Dkt, Fatuma Rashid Khalfan (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao kazi pamoja na maafisa kutoka taasisi ya Dignity.
……………………………………………………………………………………

Na Mbaraka Kambona,

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) kwa kushirikiana na taasisi ya DIGNITY kutoka Denmark wamekutana na wadau mbalimbali wa haki za binadamu  kuandaa muongozo wa ukaguzi na ufuatiliaji wa Magereza nchini.

Wadau hao wamekutana katika kikao kazi kinachofanyika mkoani Morogoro kuanzia Februari 3 – 4, 2020 kwa lengo la kuandaa muongozo utakaotumika kufanya ufuatiliaji na ukaguzi wa Magereza ili kuboresha maeneo hayo.
Kikao kazi hicho kilichojumuisha wadau mbalimbali wa masuala ya haki za binadamu kimelenga pia kubadilishana uzoefu katika masuala ya ukaguzi na ufuatiliaji wa maeneo wanapozuiliwa watu ikiwemo magerezani, mahabusu na vituo vya polisi kwa lengo la kujenga uelewa wa pamoja.

Akiongea wakati wa ufunguzi wa kikao kazi hicho, Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Fatuma Rashid Khalfan alisema kuwa kikao kazi hicho ni fursa nzuri kwa tume na wadau wengine kuboresha mbinu utendaji wao wa ukaguzi na ufuatiliaji wa maeneo wanapozuiliwa watu.

“Kikao kazi hiki ni fursa nzuri kwetu sote kama wadau kubadilishana uzoefu katika hatua za msingi za kufanya ufuatiliaji na ukaguzi na kukubaliana namna nzuri ya uandaaji wa muongozo wa ufuatiliaji na ukaguzi wa maeneo wanapozuiliwa watu”, alisema Dkt. Fatuma  

Aliendelea kusema kuwa kikao kazi hicho kinaenda sambamba na jukumu la kikatiba la tume la kutembelea magereza na maeneo walimozuiliwa watu na  kutoa mapendekezo mahususi kwa serikali ili kuboresha maeneo hayo.
Dkt. Fatuma alieleza kuwa kikao kazi hicho kimefanyika wakati muafaka ambapo Wizara na Taasisi mbalimbali za serikali na binafsi zikiwa katika juhudi kubwa ya kuboresha mazingira na maisha ya wafungwa nchini.
“Katika jitihada hizo, siku ya Maadhimisho ya Uhuru, Disemba 9, 2019 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli alitoa msamaha kwa wafungwa 5533 kwa lengo la kupunguza msongamano magerezani”, aliongeza Dkt. Fatuma

“Tume inaendelea kupongeza maamuzi hayo ya Rais, hivyo ni mategemeo yetu kuwa taasisi nyingine za serikali na zisizo za serikali zitaendelea kushirikiana na tume katika utatuzi wa changamoto zinazokabili Magereza na maeneo mengine wanapozuiliwa watu”, alisisitiza Dkt. Fatuma
Aliongeza kuwa kikao kazi hicho kitaleta matokeo ambayo yatapelekea kuimarika kwa uhamasishaji na ulinzi wa haki za watu walioshikiliwa kulingana na miongozo ya kimataifa, kikanda na kitaifa ya haki za binadamu.

Aidha, Dkt. Fatuma aliishukuru taasisi ya DIGNITY ya Denmark kwa kuwezesha kikao kazi hicho na kuwataka washiriki kutumia kikao kazi hicho kujifunza na kubadilishana uzoefu kwa lengo la kuboresha maeneo walipozuliwa watu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...