TUME
ya Taifa ya Uchaguzi ,tayari imekamilisha maandalizi ya zoezi la
uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura ,katika kundi la mkoa wa
Dar es salaam na Pwani .
Aidha, kwasasa Tume hiyo inaendelea na zoezi la kuhamasisha wadau kwa kutoa semina katika ngazi za mkoa,Jimbo na kata.
Akifungua
mkutano wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na wadau wa uchaguzi, Makamu
Mwenyekiti wa Tume ,Jaji Mbarouk Mbarouk, huko Kibaha Mkoani Pwani
,alifafanua ,zoezi la majaribio lilifanyika katika mikoa ya Pwani na
Morogoro kama sehemu ya maandalizi ya uboreshaji daftari .
"Katika
mkoa wa Pwani uandikishaji huo ulifanyika katika kata ya Kibuta
wilayani Kisarawe na Morogoro ulifanyika kata ya Kihonda Manispaa ya
Morogoro.":
Hata hivyo,uboreshaji unaendelea katika halmashauri saba za mkoa wa Morogoro.
":Lengo
la uandikishaji wa majaribio ulifanyika kwa siku saba kuanzia machi
29 mwaka jana hadi april 4 ,lilikuwa ni kupima uwezo wa mfumo wa
uandikishaji na utendaji kazi wa vipuri vipya vilivyofungwa kwenye
mashine za kielektroniki za BVR.:"alibainisha Mbarouk.
Mbarouk
aliwashukuru wananchi wa Kibuta ,na kuwaomba wajitokeze tena kwa wingi
katika kipindi hiki cha zoezi la uboreshaji daftari la kudumu la wapiga
kura.
Pamoja
na hayo ,alisema kwamba uboreshaji umeshakamilika pia mikoa 23 ya
Tanzania Bara,halmashauri mbili za mkoa wa Morogoro na mikoa yote mitano
ya Tanzania Zanzibar.
Alieleza
Mbarouk ,Tume ya Taifa imepewa jukumu la kikatiba la kusimamia na
kuratibu uandikishaji wa wapiga kura katika uchaguzi wa Rais na
wabunge na madiwani ikiwa ni kwa mujibu wa ibara ya 74(6) (a) na (d)
ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977.
Pia
alisema ,Tume inatambua umuhimu wa kuwashirikisha wadau katika
michakato ya uchaguzi kwa lengo la kuwa karibu nao,kujenga imani kwa
jamii na kuweka uwazi katika utekelezaji wa majukumu yake.
Mada
kuhusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura ,iliyoandaliwa na
mkurugenzi wa uchaguzi ,dkt Wilson Mahera ilielezea ,zoezi la uhakiki
wa vituo vya kuandikisha wapiga kura nchi nzima lilifanyika 2018,Lengo
lilikuwa kuona kama vituo hivyo bado vipo na kama bado vina sifa na
hadhi kwa mujibu wa sheria na kanuni za uchaguzi.
"Kutokana
na uhakiki huo vituo vya kuandikisha wapiga kura kwa nchi nzima
viliongezeka kutoka 36,549 hadi 37,407 lakini kwa mkoa wa Pwani vituo
hivyo 1,734 vya kuandikishia wapiga kura vilivyokuwepo mwaka 2015 na
havijaongezeka kwa mwaka huu"alisema
Katika
hatua nyingine, Mahera alieleza ,uboreshaji huu unahusisha waliofikisha
miaka 18 mwaka huu, waliohama kuhamia maeneo mengine na waliopoteza
kadi na kupoteza sifa.
Kwa
upande wake ,ofisa uhamiaji ,kamishna msaidizi Wilfred Minja akieleza
elimu ya uraia ,alisema masharti ya mpiga kura lazima awe raia wa
Tanzania ,ambae amezaliwa na wazazi aidha mmoja awe Mtanzania au
kazaliwa Zanzibar.
Alisema,
ambae amezaliwa na wazazi ambao sio raia wa Tanzania awezi kuwa raia
mfano ,wakimbizi hata kama watoto wao wamesoma Tanzania lakini watakuwa
hawana sifa ya kuwa raia wa Tanzania .
Zoezi la uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura ,linatarajia kuanza februari 14- na kukamilika februari 20 mwaka huu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...