Msanii Nyota wa muziki wa kizazi kipya a.k.a BongoFleva Nasibu Abdul almaarufu Diamond Platnumz, amesema kuwa atachangia ‘kodi ya pango’ kwa kaya 500 nchini kwa ajili ya kupunguza makali ya kiuchumi wakati huu ambapo Watanzania wanapambana dhidi ya virusi vya Corona (Covid-19).

''Najua katika kipindi hiki cha Corona, mambo mengi hayajakaa sawa, hususani upande wa biashara, nyingi zimeshuka na kupelekea hali ya kifedha kuyumba na mambo kuwa kidogo magumu kwa wengi wetu... na mimi ni miongoni mwa walio ndani ya janga hili,'' ameeleza Diamond kwenye ukurasa wake Instargram

Kupitia ukurasa wake wa  Instagram,Msanii huyo ambaye amejizolea sifa lukuki ndani na je ya nchi ,Diamond amebainisha kuwa katika kulifanikia zoezi hilo utaratibu zaidi utatangazwa siku ya Jumatatu ya namna kaya hizo 500 zitakavyopatikana na kuweza kupata msaada huo.

Diamond Platnumz anakuwa msanii wa kwanza nchini kujitokeza hadharani na kuweka bayana kuwa atasaidia chochote wakati huu wa janga la mlipuko wa virusi vya corona vyenye kusababisha homa kali ya mapafu yaani #COVID-19.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...