WAZIRI anayeshughulikia Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Singida kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi na katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Angelina Lutambi

WAZIRI anayeshughulikia Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Singida kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi na katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Angelina Lutambi

Kikundi cha Ngoma Asili cha Sarakasi wakitumbuiza wakati wa uzinduzi wa Mwongozo huo


Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi mwenye kilemba cheupe akishiriki kucheza ngoma ya asilina wadau mbalimbali

WAZIRI wa Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo akikagua baadhi bidhaa zilizoletwa na wadau mbalimbali

Kwaya ya Chuo cha Utumishi Singida wakitumbuiza wakati wa tukio hilo
Na John Mapepele, Singida

Waziri kuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassimu Majaliwa amezitaka Mamlaka zote za Mikoa kujipanga kikamilifu kutangaza fursa za uwekezaji zinapatikana kwenye mikoa yao kwa kushirikiana Kituo cha Taifa cha Uwezekezaji ili kuhakikisha kuwa fursa zote zilizoainishwa kwenye miongozo ya uwekezaji zinapata wawekezaji makini ili kuongeza mapato na ajira kwa wananchi

Akisoma hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwenye tukio la uzinduzi wa Mwongozo wa Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Singida, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo amesema kwa mujibu wa Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano(5) Serikali imedhamilia kuimarisha ustawi wa wananchi wake kwa kuzalisha ajira milioni nane na kukuza uchumi wake kwa asilimia nane hivyo uwekezaji makini unatakiwa ili kufanikisha azma hiyo.

Amesema ili kuwapata wawekezaji makaini watendaji wote wa Serikali hawana budi kutoa taarifa sahihi za fursa zinazopatikana katika maeneo yao na utaratibu wote wa namna ya kuufuata ili kuweza kuwekeza.

“Ndugu zangu ni muhimu sana tubadilike taarifa za uwekekezaji tunazozitoa ziwe sahihi na ziwe zinafanana, ukienda kwa Mkuu wa Mkoa upate taarifa sawa na ukichukua taarifa hiyo kwa Katibu Tawala wa Mkoa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hapo tutakuwa tumefanikiwa” amesisitiza Profesa Mkumbo.

Amezitaka mamlaka hizo kutowakwamisha wawekezaji kwa kuhakikisha maeneo ya uwekezaji yanapatikana mara moja ili pindi Wawekezaji wanapofika wanapatiwa maeneo hayo na wanahudumiwa kikamilifu ikiwa ni pamoja na kuondoa changamoto zozote zinazojitokeza.

Amesema balozi namba moja anayeweza kuleta au kutoleta wawekezazi katika nchi yoyote duniani ni Muwekezaji aliye ndani ya nchi husika hivyo ni muhimu kuwapa huduma bora ili waweze kutuletea wawekezaji wengi zaidi ambapo amesisitiza uwekezaji ufanywe kwa kuzingatia sheria, taratibu na miongozo ya Serikali ili nchi yetu iweze kunufaika.

Amekemea tabia ya kupenda kutoa lawama baada ya kuingia mikataba mibovu na wawekezaji na badala yake amewataka watendaji kuwa makini katika mchakato mzima wa majadiliano na kufunga mikataba hiyo na wawekezaji.

Aidha, ameitaka kila Mkoa kuangalia kuangalia maeneo machache ya kipekee ili kufanya uwekezaji wenye tija badala ya kwenda na maeneo mengi ambayo hayana tija.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi ameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa kubuni mikkakati kabambe ya uwekezaji ambayotayari katika kipindi kifupi imeleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi na kijamii kwenye nchi yetu.

Amesema Mkoa wa Singida ni miongoni mwa mikoa ambayo ilikuwa ikionekana kama mikoa masikini lakini sasa umekuwa ni miongoni mwa mikoa ambayo inaweza kuongoza kuleta mapato makubwa kwa nchi kutokana na kuboreshwa kwa mazingira na fursa nyingi zilizopo.

Ametaja baadhi ya fursa za uwekezaji zinazopatikana kuwa ni pamoja na madini, kilimo cha Alizeti na Korosho, mafuta asilina na gesi pia elimu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...