Na Abdullatif Yunus

Naibu Waziri wa Nishati na Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini Advocate Stephen Byabato amewasilisha Kilio cha Wapiga kura wa Jimbo la Bukoba Mjini kuhusu adha kubwa wanayokumbana nayo wakati wanapohitaji Kuunganisha Huduma ya Maji nyumbani kwao, ambapo hutakiwa Kulipia Shilingi laki moja na Nusu pesa ambayo ni gharama kubwa.

Naibu Waziri Byabato amewasilisha Kilio hicho kwa Naibu Waziri wa Maji Mhe. MaryPrisca ambaye yupo Ziarani Mkoani Kagera, wakati wa Mazungumzo yaliyofanyika Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa Kagera, mapema Machi Mosi alipofika katika Ofisi hizo.

Mhe. Byabato ameomba Serikali kupitia Wizara ya Maji kutizama upya gharama hizo na ikibidi gharama zipunguzwe kwakuwa Jimbo la Bukoba Lina Maji ya Kutosha, na pengine gharama hizo zilipwe kidogo kidogo.

Akijibu ombi Hilo Naibu Waziri wa Maji MaryPrisca ameeleza kuwa changamoto hiyo kwa Sasa ipo Mikoa mingi Nchini na kwamba tayari ushauri na maombi hayo yamekwishaanza kufanyiwa kazi na Wananchi watarajie Huduma hiyo kuwafikia nyumbani.

Kwa upande mwingine Naibu MaryPrisca amewashukuru Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Bukoba (BUWASA) kwa namna ambavyo wameendelea kutekeleza Miradi mbalimbali ya Maji Jimboni humo, na kuongeza kuwa amefurahishwa na kauli Mbiu yao Mpya ya Maji inayosema MAJI BOMBANI,BOMBA LIPI , BOMBA LA NYUMBANI na kwamba anaichukua itumike Nchi nzima















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...