Na Mwandishi wetu, Simanjiro
KATIBU
Tawala (DAS) wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Zuwena Omary Jiri
amewataka viongozi wa Tarafa, kata, vijiji na wananchi mbalimbali
kutotegemea nyaraka pekee katika kutatua migogoro ya ardhi.
Zuwena
ameyasema hayo wakati akielezea miongozo tofauti ya utatuzi wa migogoro
mbalimbali ya ardhi iliyopo kwenye maeneo tofauti ya kata na vijiji vya
eneo hilo.
Amesema
viongozi wasijikite kwenye nyaraka pekee kwani siyo sifa ya kumiliki
ardhi ili hali nyingine huwa siyo halali japokuwa nyaraka ni kielelezo
kimojawapo cha umiliki wa ardhi.
"Tunapaswa
kwenda mbali zaidi ya kumiliki nyaraka na kudhibitisha kuwa anamiliki
eneo la ardhi hiyo japokuwa hatupingi kuwa na nyaraka ndiyo kutokuwa na
ardhi ila siyo kigezo cha udhibitisho pekee," amesema Zuwena.
Amesema
jambo limefanyika vijijini kisha mtu anakimbilia wilayani kuwa ana
nyaraka za umiliki wa ardhi hivyo jamii inapaswa kushirikishwa ili mtu
asinyang'anywe ardhi yake kwa nyaraka za kughushi.
Amesema
mambo mengi yanatokea kwenye vitongoji na vijiji kisha watu wanafika
makao makuu ya wilaya na kulalamikia kuwa wamenyang'anywa ardhi ili hali
wananchi ndiyo wanatambua hali halisi ilivyo.
"Kuna
watu wameishi miaka mingi kwenye vitongoji na vijiji hao wanapaswa
kushirikishwa ili waeleze wanachotambua juu ya hilo na siyo kutegemea
nyaraka pekee," amesema Zuwena.
Amesema
wazee wa kimila au watu walioishi miaka mingi wanafahamu wamiliki
halisi wa ardhi kwenye vijiji vyao tofauti na mtu akiwa na nyaraka zake
ambazo amezipata kwa ujanja ujanja.
Mkazi
wa kata ya Naberera, John Peter amesema ni ushauri mzuri umetolewa na
kiongozi huyo hivyo viongozi wa ngazi hizo na wananchi kwa ujumla
wanapaswa kutekeleza hayo.
Amesema
viongozi na wananchi walioishi muda mrefu wakishirikishwa kutakuwa na
tija zaidi tofauti na kutegemea nyaraka pekee ambayo imekuwa inachochea
migogoro ya ardhi.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara,
Zuwena Omary Jiri akizungumza kwenye kikao cha Baraza la madiwani wa
Halmashauri ya Wilaya hiyo, katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri hiyo, Yefred Myenzi na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo,
Baraka Kanunga Laizer.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...