Na MWAMVUA MWINYI,PWANI
MKUU
wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo ametoa miezi mitatu kwa
,mmiliki wa Kampuni ya Mafubilo General Supplies iliyopo Kibaha
kuwalipa wakulima wa korosho deni wanalodai la zaidi ya sh.milioni.
356.156.3.
Fedha
hizo wanadai wakulima wa Kibaha baada ya korosho zao kilo 282,306.5
zilizokuwa kwenye vyama vya ushirika (Amcos) vitano kuuzwa kwa Kampuni
hiyo.
Ndikilo alitoa agizo hilo ,Mjini Kibaha wakati wa kikao maalum na wakulima ambao waliingiia mkataba na muwekezaji huyo.
Aidha ,alimpa muda huo kuhakikisha analipa deni hilo na akishindwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Mkuu
huyo wa Mkoa ,alielekeza mmiliki wa Kampuni hiyo kulipa fedha hizo kwa
awamu tatu kila awamu ahakikishe analipa kwa awamu milioni milion 118.
Pamoja na hilo, alitoa muda mfupi kwa muwekezaji huyo kukiri kuwa atalipa deni hilo pindi atakapopata barua ya kumtaka alipe.
Kwa
mujibu wa mkataba uliosainiwa mwezi Februari, mwaka 2020 kati ya
Kampuni ya Mafubilo na vyama hivyo vya ushirika ni kwamba mnunuzi
alitakiwa kulipa fedha hizo kwa muda wa siku 63.
Amcos
zilizoshiriki kusaini mkataba huo ni Kongowe ( kilo 168,982.50),
Mwendapole (kilo 2,279) na Misugusugu (kilo 72,314), Visiga (kilo
36,244) na Mkombozi ( kilo 2,487) na kwamba kilo zote za Korosho zina
thamani ya Shilingi 394,156,335.30 hadi sasa ni Shilingi Milion 40 tu
ambazo zimelipwa na Kampuni hiyo.
Wakulima
hao walieleza,wamekuwa wakisumbuka kwa muda mrefu kufatilia jambo hilo
na kwamba sasa wameanza kuona muelekeo wa kupata haki zao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...