Na Amiri Kilagalila,Njombe

Halmashauri ya mji wa Njombe imewaagiza watendaji na maafisa ugani katika ngazi za kata kuhakikisha inatoa elimu ya kutosha kwa wananchi kuzingatia kanuni za kilimo bora kisichoathiri mazingira kwa kuwa ndio msingi wa maisha ya binadamu.

Agizo hilo limetolewa na kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bwana Thadei Luoga wakati akifungua kikao kazi cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi ya awamu ya pili iliyotekelezwa na shirika la Highland Hope Umbrella kwa ufadhili wa The Foundation for Civil Society kwenye kilimo katika kata tano za halmashauri hiyo,hatua iliyoambatana upokeaji wa mradi awamu ya tatu.

“Tuzingatie,tuhakikishe tunawaelimisha wananchi wetu kuzingatia kanuni za kilimo bora na kisichoathiri mazingira kwasababu mazingira ndio mwarobaini wa kila kitu kwasababu pamoja na jitihada za jamii za kupanda miti na kuhifadhi mazingira zinatufanya Njombe tuendelee kuwa na hali ya hewa inayotuwezesha kuzalisha mazao ya mboga mboga nay ale ya nafaka”alisema Bwana Luoga

Bathseba Barnaba Liduke ni mkurugenzi wa asasi hiyo,amesema wamekuwa wakifanya miradi mbali mbali ikiwemo ya elimu,afya,watoto pamoja na kilimo ambapo katika kilimo wamefanikiwa kutekeleza kwa awamu mbili na sasa wakielekea awamu ya tatu katika tarafa ya Igominyi  kwa lengo la kuelimisha jamii kuelewa wajibu wao kwenye kilimo.

“Lengo kubwa ni kuhamasisha jamii iweze kuelewa kama ina wajibu gani katika kufuatilia maswala ya kilimo na kuangalia namna kilimo kinavyoendesha katika halmashauri yao na sio kupiga kelele tu”alisema Liduke

Vile vile Bi,Liduke amesema zaidi ya wakulima 300 katika kata tano lengwa za halmashauri hiyo wameweza kunufaika na utekelezwaji wa mradi.

Kwa upande wake afisa kilimo wa halmashauri hiyo alisema licha ya halmashauri hiyo kuendelea kupambana na kuendeleza kilimo lakini wanakumbwa na uhaba mkubwa wa maafisa ugani huku akishukuru shirika hilo kwa msaada ambao wamekuwa wakiutoa katika maswala ya kilimo.

“Halamsahuri yetu ya mji wa Njombe ina upungufu mkubwa sana wa wataalamu wa kilimo ukilinganisha na idadi ya vijiji,halmashauri ina maafisa ugani 23 na ukijumlisha vijiji na mitaa unapata 72 na kwa kweli changamoto hii ni kubwa sana unaweza kukuta kuna wakati afisa mgani mmoja ana fanya kazi katika kata zaidi ya mbili.Niombe serikali itufikirie kwasababu halmashauri ya mji Njombe ni tofauti na halmashauri zingine kwa kuwa ina mitaa 28 halafu ina vijiji 44”alisema afisa kilimo.

Aliongeza kuwa “Taasisi hii ya HHU inajitahidi sana kushirikiana na halmashauri na kufuatilia utendaji kazi wa maafisa ugani wao,wanasema maswala ya uwajibikaji”alitoa pongezi afisa kilimo

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa kikao kazi hicho,diwani wa kata ya Luponde bwana Urlick Msemwa amesema taasisi hiyo imekuwa ikifanya kazi nzuri na kuongeza uwajibikaji kwenye kilimo katika kata tano za mradi.

“Kufanya kazi na sisi kumeongeza uazalishaji na uwajibikaji kwenye kilimo,tunaendelea kuwaona kama wadau muhimu sana na tunaendelea kuwaunga mkono wakati wowote ili kuwezesha kilimo kwenye halmashauri yetu”alisema Urlick Msemwa

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Njombe  Bwana Thadei Luoga akifungua kikao cha kupokea taarifa ya utekelezwaji wa mradi pamoja na kupongeza shughuli mbali mbali zilizofanywa na shirika la HHU mjini Njombe.



 
:Mmoja wa watumishi kutoka shirika la HHU akieleza namna mradi awamu ya pili ulivyotekelezwa na kutambulisha mradi awamu ya tatu utakavyotekelezwa katika halmashauri hiyo


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...