Na.Khadija Seif, Michuzi TV.
 
WABUNIFU Wa Kizanzibar wameahidi kutumia fursa ya jukwaa la Mavazi ya Kiasili kusaidia Serikali ya Zanzibar kutangaza na kukuza pato la Taifa.

Akizungumza na Michuzi, Mbunifu Mkongwe kutoka Visiwani Zanzibar ambae pia ni Muasisi wa jukwaa la ubunifu (Zanzibar fashion island) Waiz Shelukindo  amesema Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi julai mwaka huu likiwa na lengo la kutangaza utalii visiwani na Mavazi ya Kiasili.

"Sanaa ya Ubunifu wa Mavazi lazima ikue hivyo lazima kuwepo Kwa Matamasha ambayo yanakumbusha na Kuonyesha vitu vipya hivyo tumeamua kutangaza utalii kwenye jukwaa la ubunifu wa Mavazi linalotarajiwa kufanyika julai 29 Hadi 30 mwaka huu katika ukumbi wa front ocean Visiwani Zanzibar."

Aidha ameeleza kuwa jukwaa hilo litakuwa la wazi Ili kuwapa fursa watu kuhudhuria Kwa wingi na kuona Kwa jinsi gani Kuna baadhi ya Mavazi ya Kiasili na kitamaduni hayapewi nafasi Kwa Sasa kutokana na utandawazi na tamaduni za kizungu.

"Kuna baadhi ya Mavazi mara nyingi yamekua hayaonekani lakini wabunifu kutokana na kazi zao wamekuwa wakitengeneza hivyo jukwaa hilo litaweza kuwapa fursa wabunifu kuonyesha Mavazi hayo."

Pia Waiz amesema kupitia jukwaa hilo litashirikisha wabunifu wa ndani na nje ya nchi ikiwemo Visiwa vya Comoro,Kenya, Uganda na nchi zingine nyingi Visiwani Zanzibar.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...