Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na Viongozi wa Gereza la Isupilo Wilayani Mufindi, Mkoani Iringa, leo Disemba 4, 2022. Amelitaka Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza (SHIMA) kuhakikisha linatumia Ardhi ya Gereza hilo kuongeza kasi ya uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akisalimiana na Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza katika Gereza la Isupilo Wilayani Mufindi wakati alipokuwa anawasili katika Gereza hilo kukagua utendaji kazi, leo Disemba 4, 2022. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Taasisi zake wa Mkoa wa Iringa, wakati alipokuwa anawasili Mkoani humo kwa ziara ya kikazi, leo Disemba 4, 2022. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Taasisi zake wa Mkoa wa Njombe, wakati alipokuwa anawasili Mkoani humo kwa ziara ya kikazi, leo Disemba 4, 2022. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Na Mwandishi Wetu, Iringa
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amelitaka Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza (SHIMA) kuhakikisha linatumia Ardhi ya Gereza la Isupilo Wilayani Mufindi Mkoani Iringa pamoja na magereza mengine nchini kuongeza kasi ya uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.

Akizungumza wakati wa ziara yake katika gereza la Isupilo, leo, Masauni amesema kuwa mbali ya kuanza kazi kwa SHIMA ila amefarijika na mapokeo makubwa ya mabadiliko ndani ya Jeshi la Magereza hasa katika Mkoa wa Iringa kutokana na jinsi walivyopokea mabadiliko hayo mapya.

Aliongeza kuwa, uwepo wa SHIMA ni fursa kubwa kwa magereza kutimiza majukumu yao pia kunufaika zaidi ya shirika hilo kiuchumi kama gereza na wafungwa wanaomaliza muda wao .

Alisema jambo kubwa la shirika ni kusimamia shughuli za kibiashara zitakazotokana na kilimo huku magereza wao watafanya shughuli za kusimamia wafungwa kwa kuripoti wa kamishana wa magereza Tanzania huo shirika msimamizi wake atakuwa mkurugenzi mkuu wa shirika .

Hivyo alisema makubaliano kati ya shirika na Jeshi la Magereza kwa wafungwa yatakuwa ya kibiashara kati ya pande hizo mbili na itasaidia magereza na wafungwa kupata faida ya nguvu wanazotumia.

"Sioni ubaya wowote kwa Jeshi la Magereza kuwalipa wafungwa watakaomaliza vifungo vyao kwa nguvu watakayoitumia "

Waziri Masauni aliizindua Bodi SHIMA Novemba 3, 2022, ambalo litakuwa na maono ya kibiashara na utekelezaji wa azma ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambapo moja ya kipaumbele chake ni kuboresha Jeshi na mifumo yake.

Masauni alisema katika kutekeleza mipango hiyo, Rais aliongeza Bajeti ya jeshi hilo, ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ipasavyo kwa ufanisi na weledi.

Alisema kutoka na wajumbe wa bodi hiyo aliowateua kwa sifa na weledi wao, serikali ina matumaini makubwa kuwa watatekeleza majukumu yao kwa uzalendo wa kusaidia Taifa katika Jeshi la Magereza kusonga mbele zaidi.

"Lengo kuu la SHIMA ni kusaidia Jeshi la Magereza kutenganisha majukumu ya kijeshi na biashara bila muingiliano wowote, ili kuwepo kwa mafanikio makubwa yakujiendesha na kuchangia pato la Taifa, hivyo ni matumaini yangu makubwa kuwa bodi hii itasaidia shirika hili kutimiza malengo hayo na kusonga mbele zaidi," alisema Masauni.

Aidha, Waziri Masauni aliitaka Bodi hiyo aliyoizindua kutatua changamoto zilizopo, ambazo ni nikutokuwepo mfumo maalumu wa kujiendesha, kutozingatia kanuni na taratibu, kutokuwa na maono na nia ya dhati ya kujiendesha kibiashara na kutatua baadhi ya migogoro iliyopo.

Masauni alifanya ziara ya siku moja moja katika mikoa ya Ruvuma, Njombe na Iringa akiwa na lengo ya kukagua utendaji kazi wa taasisi zake zilizopo katika mikoa hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...