Kaka Michuzi,
Kwa jina naitwa Jovinata Kileo. Natokea mkoa wa Kilimanjaro. Nina miaka 28, niko single, sina mtoto, na wala sijawahi kuolewa. Baba ni Mchaga ila Mama Mjerumani. Mimi ni mtoto wa pili katika familia. ninaye Kaka ambaye ameshaoa na anaishi zake Afrika Kusini. Mama ni marehemu ila baba anaishi Moshi
Elimu ya msingi nimesomea Moshi, na baadae kujiunga na shule ya International School of Tanganyika, Kabla ya kuendelea na masomo ya Juu Afrika kusini. Nilipata shaada ya kwanza ya biashara na hatimaye ya pili ya maswala ya utawala mwaka 2005.
Kwa sasa nafanya kazi katika shirika la kuhudumia wakimbizi lililopo Juba Sudan. Ingawa ninaweza kusema kwamba nimejaliwa kazi nzuri, na maisha mazuri, ninaona upungufu Fulani maishani mwangu, kwani kila mwanamke inabidi awe na familia yake, na Muda unavyozidi kwenda, naona uzee unaninyemelea bila matumaini ya kumpata mchumba.
Nilishauriwa kwenda kwa waganga wa kienyeji ili nipata usaidizi, lakini haijasaidia. Niliyempata akawa balaa, tapeli wa kutupwa. Mmoja wa vigogo nchini aliniahidi uchumba matokeo yake nikaja kugundua ningekua mke wa tatu. Sikuwa tayari kuwa mke wa tatu. na waliokuwa wakinishauri mambo ya waganga ndo kabisa wamezalishwa na kutelekezwa.
Namtafuta kijana mcha Mungu ambaye tutakuwa pamoja. Kutokana na familia yangu kuwa ya kidini sana (walutheri) nitafurahi sana kumpata Mkristo wa aina hoyote, na pia mcha Mungu.
Manka alipoweka maombi yake ya kutafuta mchumba, wengi walimuona kama vile kichaa. Ila, katika dunia ya sasa na hali ya sasa, inambidi mwanamke atafute vigezo kwa mwanamme.Sitaki kumparamia mpiga tungi wa siku mbili tatu, wala sitaki mlevi wa ngono. Namtafuta mume ambaye atakuwa baba watoto wangu. Sitafuti makuu, namtafuta mwanamme msomi lazima hawe na masters na hawe na umri chini ya miaka 35 na ambaye hajawahi kuoa.
Mzungu marufuku, wala mtu uchanganyiko sitaki. Asiwe mlevi, au mtumiaji wa kileo cha aina yoyote. Lazima hawe na kazi, Lazima awe na roho safi , mwenye fadhila na mpenda watu atakayenipenda kwa moyo wake wote.
Ulipoiweka picha ya bwana John Mashaka mara ya kwanza, niliguswa sana, ila kwa vile sikuwa na uhakika , nilishindwa na la kufanya ili niweze kuwasiliana naye; Nilikuomba contacts na email zake lakini ukanibania. Nilipokuomba namba za Mshikaji toka Ukraine pia ulinibania, wakati alibainisha wazi kwamba naye ni single nikashindwa kukuelewa.
Ulipoibandika picha ya Mashaka hapo jana, sikuwa na budi kuchunguza zaidi ili kufahamu hali yake ya ndoa. Inshallah, hajaoa. Sitaki kujua saizi yake ya viatu, sitaki kujua ana hela ngapi au magari mangapi, simtaki kwa vile yupo Marekani . Sitaki maisha yake mazuri, ninachohitaji ni roho yake safi. Naomba kwa hisani ya mbingu unipe namna ya kuwasiliana naye ili tujuane.
Ukiona kuna ugumu, basi niunganishe na yeyote mwenye wasifu wake. Nipo Tayari kununua tiketi na hela zangu na kwenda kukutana naye popote pale alipo.
Au kama atakuja Tanzania mwaka huu, naomba unijulishe ni lini ili nikutane naye bwana Mashaka kwa ajili ya maongezi ya kawaida. Ukininyima contacts, zake, basi naomba uchapishe conctacts zangu ili kaka yeyote wa kitanzania mwenye hizo sifa anitafute kupitia
jovinatakileo@yahoo.comWAKO MTIIFU
Jovin-Grusdin- KILEO
mdada hongera kwa hatua hiyo!! ila naomba kuuliza kwani MITHUPU aliandika mashaka anataka mtu wa kuoa???
ReplyDeletehutaki mzungu wala mtu mchanganyiko!!!while na ww ni mchanganyiko!!wa2 wakikukataa je utapata m2??
hiyo elim yako na wasiwasi nayo lkn mh may b mana hizo msomi lazima HAWE na na masters na HAWE ..!KAZI IPO
mm nakutakia kila la kheri na ninakukaribisha saaaaaaaaaaaaana kwenye klab ya wanandoa! ina raha yake ati!!
Mdau XXXL
MDOGO WANGU KAMA WEWE NI MCHA MUNGU NI KWAMBA MWANAUME HATAFUTWI KWA NJIA HIYO UNAYOIFUATA. KWA USHAURI WANGU OMBA KWA MWENYEZI MUNGU NA UTAFANIKIWA. TATIZO BINADAMU NI MVIVU WA KUSALI CHOCHOTE UOMBACHO UTAFANIKIWA SASA USIJALI MUDA KWANI KWA MUNGU HAKUNA MUDA. WAWEZA KUOMBA SASA NA KUPATA MUDA HUO AU BAADAE. ILA UNAPOCHELEWESHWA KUPATA UNAKATA TAMAA NA UKIKATA TAMAA NA OMBI LAKO LINAFUTWA.MIMI NILIOMBA NA KUPATA MKE BAADA YA MIAKA KUMI. SASA WEWE UNAMONA MTU KTK NET UNAMTAMANI ANAWEZA KUWA AMESHAPATA MWEZI WAKE.
ReplyDeletedu msichana mzuri kama huyu hajaolewa na anatafuta mwanaume?michuzi ungekua hujaoa hapo si fresh sana tu mpango mzima?omba mungu utajaaliwa riziki yako bado haijafika tu,mungu ndie anajua kakupangia lini..lakini swala la humu utapata waosha vinywa,inamaana huko hujapata ile mishefa ya umoja wa mataifa kwenye kambi za wakimbizi?na labda nikuambie siku hizi wanaume wachache wanawake wengi,sasa ukitaka wa peke yako pia unaweza usimpate ungekubali kua mke wa tatu tu..wenzio tunabanana siku hizi hata wakristo wanaoa wake wawili kisirisiri
ReplyDeleteNjia fupi ya kupita ni kuzunguka zunguka kwenye Bar naimani utapata mchiumba kila lenye mafanikio kwani kule utaweza kuchaguwa ni yupi unae hisi kuwa anaweza kuwa baba watoto wako
ReplyDeletePole sana Jovinata na hongera kwa ujasiri wako.
ReplyDeleteWewe mshukuru Mungu wako kwa kukujaalia uzuri, elimu na kazi nzuri.
Mie nimekumaindi kinoma ila natatizwa na vigezo vyako viwili, kwanza elimu yangu ni ndogo (shahada mbili lakini zote ni undergraduate siyo masters) na pia dini.
Hata hivyo nakutakia kila la kheri na nakuombea umpate atakayekufaa....
MKR(dar)
Mi bwana kwa wanawake katika yoooote, mi hua naangaliaga taarabu tu,
ReplyDeleteYaan ni mgonjwa sana katika mambo ya taarabu,
sasa dada yangu hapo nkikuangalia taarabu huna,
Anyway, watapatikana wengine tu
Baby you are cute,
ReplyDeleteBut the standards you have set (Masters degree and be a Lutheran) will automatically preclude a good number of would-be-fiancees
Wimbo ulioandika una maneno ya kweli. Nakutakia kheri, mtu ana haki ya kusema kilichopo moyoni.
ReplyDeleteLakini mashaka ni mkulya(mwanageshi) sasa utamuweza?
Haya Jovinata, nitafute ktk anuani hii: mbalamoon@yahoo.com. Kuna mambo machache tu inabidi nikwambie. Mimi sina masters bali na diploma ya juu, mcha mungu, miaka 28 na niko nje ya bongo. Niko tayari kuwa baba watoto wako!
ReplyDeleteMichuzi.
ReplyDeleteHivi mbona wote wanaojinadi wanaonekana kuwa na lugha zinazofana katika kuwatafuta wachumba?
Dada jovin pole sana.Hivi unadhani kuna mwanaume aliyekamilika?Uyo uliyempata usingemwacha ulipaswa umtengeneza awe unavyotaka.
Wanawake wanafanya kosa moja ambalo linawagharimu kila siku kwamba wanapenda mwanamme wa aina fulani bila wao kuandaa mazingira ya uyo mwanaume (Kwani mmezaliwa tumbo moja?).Umejiandaaje kuzikubali changamoto za anaetaka kukuoa au unafikiri ni Yesu?. Kwa taarifa yako nyie wanawake kila mwanaume ana mapungufu yake jambo la muhimu ni ridhika na unayempata na kumpata mwanaume wa kuishi naye ni suala la muda lialohitaji kusubiri na kuvumilia.Muda ukiwadia unapewa na Mungu na bahati nzuri we unamwamini Mungu so omba atakusaidia.Kwanza haina haja kujinadi na kujishebedua(jiangalie picha uliotuwekea) kiasi hicho kweny net otherwise unayo matatizo yanayokupelekea husijiamini hadi kuweweseka kiasi hicho.Sikukatishi tamaa nafahamu unaweza kumpata ila una uwezekano mdogo saana kumpata umtakae kwa kupitia njia hii ulioichagua na sanasana unaweza kumpata kinyume chake.Ushauri kwako ni hivi:Makanisani,makazini,Mashuleni,Maeneo unayoishi ni maeneo mazuri unayoweza kumpata mtu ukamuelewa in and out na mka-oana na eneo hili la(internet)ndilo eneo baya zaidi la kumpata mchumba(Kwa mjibu wa utafiti).Hata ivyo hujachelewa sana Omba Mungu na jitunze zaidi pia uwe na adabu miongoni mwa watu kwani huyo unaemtafuta nae anatafuta mke mwema.
Mwenye dhamila ufanikiwa.
Pole
Kwa umri na uzuri huo kama mpaka leo huna mshikaji basi lazima una matatizo. Lakini mbona hiyo picha ukutani inaonyesha umebeba mtoto? Halafu kwa mandhari ya hicho chumba hapo ni Juba kweli? Danganya toto hii! Waosha vinywa wanachokozwa...
ReplyDeletenimependa email ya huyu dada, ni muwazi na mkweli, anastahili mume mwenye roho nzuri kweli!! Mungu atakujalia Inshallah! Nakutakia kila la heri.
ReplyDeletePS/lakini kwa nini hutaki wazungu!! walikutenda dada!! sorry
Dear Maelezo yako ni mazuri. Ila the way ulivyovaa na ulivyosimama si dhani kama utapata mchumba maana mtu anakujaji jinsi ulivyovaa sasa wewe unaonekana kama changu. Wanaume tunataka binti aliyetulia sio mapepe kama wewe siku mbili ugomvi. oka try your best.
ReplyDeleteMamaa na uzuri wote huo! nakujia huko hukosudan siwajali hawo janjawid wanaoua! i will die wit u~!
ReplyDeleteSHUK TEXAS.
basi zoezi lako limefanikiwa nina sifa zote ulizotaka na ninaongezea moja kwamba mie pia ni baba wa mtoto mmoja so ninajua uchungu wa mwana tuwasiliane kupitia siasa_zangu@yahoo.com
ReplyDeletedada wewe ni mzuri kwa sura ingawaje sijui tabia zako. cha muhimu dada nakushauri muombe mungu atakupa mume mzuri kulingana na sifa unazohitaji. umri wako bado haujaenda sana kuna watu wanaolewa wakiwa na umri wa miaka 35.hujachelewa dada tulia tu utapata mume.
ReplyDeleteJovin pole sana kwa kufika hadi kwa waganga kwa kweli umepitia mengi!nakutakia kila la kheri na ujaliwe kumpata mme mwema!kama wewe ulivyosema umempenda mashaka nakutakia kila jema ili naye akubaliane na wewe!wasukuma tunasema FUJAGA NDIMU ALIYO UTIZOFUJA NHOLA!maana yake bora ukosee kulenga mnyama porini kuliko kukosea kupata mwenza maana ndoa yako itakuwa na matatizo tu!keep it up i wish all the best
ReplyDeleteWewe kweli una matatizo na mbaguzi mno.Kwa nini hutaki wazungu wakati mama yako ni mzungu?
ReplyDeleteKama una dini hujafundishwa kuwa Mungu hana upendeleo wala ubaguzi. Mungu aweza kuwa kakuandalia mzungu au chotara lakini kwa kuwa huwataki basi utaishi bila mume milele.
Acha kubagua watu kwa misingi ya rangi mimi nakuona wewe ni kaburu wa kike sijui ukaburu wa ubaguzi wa rangi ulijifunzia Afrika ya kusini ulikosomea hizo digrii! Sijui.
Nilitaka kukuoa lakini sasa sitaki tena katafute mbele.Mtu mzima lakini hovyo!
Very interesting resume.
ReplyDeleteYou seems smart enough to smarten the boys. I will be interested to know who is going to step on your toes.
My suggest to you is that, need to relax and let the affection take its course, you seems tense individual who lacks relaxation.
I am sure there are lots of individuals/hustlers who will fall onto your trap, and that will make things worse. And that will make heard enough for you to choose, there are lot of sincere words out there.
Good LUCK!.
Last but not least get outreach hand to your nephews, cousins back in GERMANY, I understand you must had very bad hard hitting experience coming from mixed marriage, and that is affecting your personality, and sometimes making you fall victims on your love life as you had already highlighted on your resume.
By Mchangiaji
kazi ipo mithupu kweli kazi ipo,haya bwana mi sina hayo ma master elimu yangu darasa la saba lakini nimejiendeleza hapa kiwanja ila bado nabeba box mi yangu macho,kweli wahenga walisema usione chaelea hicho kimeundwa.
ReplyDeleteWE DADA INAMAANA UNAMTAFUTA HUYO JOHN MASHAKA AU UNATAFUTA MCHUMBA?MBONA MI SIKUELEWI?HATARI KWELIKWELI,KWA MPANGO HUO HUTAMPATA MCHUMBA WA KWELI,MICHZI MPE MAIL YA MASHAKA KUMBE TAYARI MTU ANAYEMTAKA YUPO,ANATUZINGUA HUYU ANAUZA SURA TU HUMU KWENYE BLOG YETU,WACHAGA BWANA DUH!
ReplyDeletenimeisoma hii post kwa umakini mkubwa. inaonekana huyu dada yupo serious kupita mpaka. ameongea kwa hisia na ujasiri kubwa. mimi nipo married hivyo sina nia ya kuwasiliana nae lakini nawaomba wadau kuwa wawe serious na haya mambo.
ReplyDeletetabia ya kutukana au kukejeli kutafuta wachumba kwa kupitia internet inaonekana kushamiri katika blog hii. sio tabia nzuri hata kidogo. kama huna interest na njia hii tafuta blog nyengine au kaa kimya.
si sahihi hata kidogo kumuona mtu anaetafuta mchumba kwa net kuwa malaya au nungayembe au hana mvuto au kumhukumu kuwa ana tabia mbaya nk. hii ni njia ya kawaida kama njia nyengine na inabidi watanzania waikubali.
mdau,
dar es salaam
haya ndo macomfo kudadeki mwananawe.Uko juu sistery.
ReplyDeleteNiko interested..niko UN .kama wewe..lakini Mashariki ya Mbali..tuweke kando mambo ya kazi na elimu ..lakini Hiyo picha ya mtoto unayembusu hapo jikoni ni ya nani??
ReplyDeleteMie nina sifa zote kasoro moja tu, mimi ni mlevi wa ngono. Hata hivyo ni mwaminifu kwa mpenzi mmoja kama anapatikana.
ReplyDeleteHebu toa maelezo kuhusu "ulevi wa ngono"
Mashaka changamkia tenda hiyo.
Ignorant
Jeremani
Safi sana dada, tafuta kitu roho inapenda!!!!!!!!!!!!!!!!
ReplyDeleteInshallah! Utapata.
Du e bwana nimekubali dada Jovin kweli inaonekana wewe uko serious na hili swala maana umeweka hata picha yako, halafu vigezo venyewe ni ni vya kawaida tu, kwa hiyo hope utapata mtu unaye mhitaji.
ReplyDeleteHongera pia kwa kuwa muwazi kiasi hicho. Umedisclose mambo yako ya ndani sana, Iam very much impressed with you ingawaje kuna kigezo kimoja ambacho sina (Masters Degree), ambacho kinanifanya nishindwe hata kuingia kwenye mchakato.
Ila wasiwasi wangu ni kwamba, angalia kuna hatari ya kupata tapeli vilevile. Maanake ni rahisi mtu kujifanya ni mpole, si mlevi wa ngono, si mpiga tungi wa siku mbili, tatu kama ulivyosema, kumbe anapretend tu, akishapata kile anachokihitaji then anaishia, it will be another disappointment to you. Mi ningekushauri umwombe sana Mungu atakupatia mwenza wako anayekufaa katika muda mwafaka, you are still young and you have got much of the qualities that a woman deserves to have )especially visble ones) ingawaje hatujui tabia za ndani kama utu wa ndani, wema, upendo, uvumilivu, etc.
All the best,
Big Sam-onetwofo21@yahoo.com
Nimeona dada una tamaa sana, na hii ndo sababu iliyokufanya usifanikiwe hata baada ya kuzunguka kwa kalumanzila.
ReplyDeleteEti oooh kigogo aliniahidi uchumba.. na sasa unamtaka Mashaka, mmmh unapenda wanaume wenye umaarufu na mipesa sio? Inaelekea hata huyo aliyekuchezea alikua sampuli hii.
Kwa taarifa yako, hivyo vigezo mnavyoweka huwa vinafifia au kuboreka. Kama ikitokea vikapungua, baada ya muda mfupi tu utagundua kua mwanaume uliedhani ni chaguo lako hakufai tena. Na kama ikitokea jamaa akaboresha vigezo vyake mf masters to phd, nae atagundua kua wewe si mwanamke wa viwango vyake. Kazi kwelikweli
Best wishes
VIVA Jovinata VIVA!!!!
ReplyDeleteMimi ni mama mwenye watoto nimekufurahia sana kwa mambo ma3
1. u-mzuri, 2. jasiri. 3Muwazina mwangalifu, kutokana na maelezo yako, hongera sana mdogo wangu Mungu akujaalie akupe haja ya moyo wako.
Be blessed
MUNGU WANGU, DUNIA IMEKWISHA KAMA MAMBO YENYEWE NDIO HAYA. WAKO WENGI TUU WANAJIZEEKEA WENYEWE
ReplyDeletemie la kusema sina maana mtoto kamwaga kila kitu sio kama manka, wadau wenyewe nadhani mtathaminisha mie nishaoa mlio singo kazi kwenu, ila mama kwenye hicho kigezo cha mtu mpaka uwe na masta hapo sasa kasheshe wengi wetu wenye mapenzi ya dhati na moyo kama huo wa huruma tumeishia darasa la 12.
ReplyDeletemama wewe sema tu moja kwa moja unatafuta fisadi... eeh ndio maana waliosoma ndio wasio na moyo wa huruma hata kidogo si unaona mabilioni yetu yanavyoliwa na wenye masta? haya mie mawazo yangu tu kila la heri
makubwaaaaa mchumbaaaa
ReplyDeleteYangu macho!!!!!!
Pole sana binti, na hongera sana kwa ujasiri wako uliouonyesha, na tunakuombea mungu akujalie umpate umtakaye, na awe ana vigezo ulivyovitaka. Kama ningekuwa sijaoa, ningejaribu kutupa karata yangu kwani sifa zote za `mrembo' unazo.
ReplyDeleteLakini pamoja na hayo, nimeshituka kidogo, sio kana kwamba ulichofanya ni kibaya, hapana, ulichofanya ni sahihi, kwani `blogi hii ya michuzi' ni ya wanajamii, na wanajamii ni kusaidiana hasa pale unapokwazwa na matatizo, pamoja na mengineyo.
Ila nikajiuliza, Manka anatokea mitandao ya Moshi, na wewe pia unatokea hukohuko. Mnisamehe sana watani wa watu fulani, lakini hapa kuna kaukweli ndani yake. Sisi kama binadamu tunapoishi kuna vitu vinakwaza, na kila mmoja anajaribi kuvikwepa kama sio kuviogopa na anaomba asikutane navyo, kwani katika maisa haya magumu hasa ya ndoa vinahitajika sana vitu hivi adimu kam vile `upendo, subira na amani'
Sasa kwangu mimi tabia kama `majivuno', `dharau' na `kupenda mali au uchoyo-uchoyo'ni mojawapo ya vikwazo vya `mapenzi ya dhati'
Unakutana na binti unamsalimia, (nazungumza kwa mfano tu), badala ya kukujibu unakukagua kutoka utosini hadi nyayoni, halafu anabenu mdomo kwa dharau. Je binti kama huyo ataolewa? Unafika ukweni unaanza kuulizwa maswala ya `gari, nyumba nk haya ni mapenzi kweli? Sijui wajamani..
Sisemi kwako wewe au kwa Manka, huenda nyote wawili mna tabia zenu nzuri kabisa, ila ni bahati mbaya watu hawajawaelewa. Lakini ili tufanikiwe kuwapata wachumba tuwapendao, lazima na sisi tujishushe tulingane na jamii zetu, hata kama hatuwezi tujaribu angalau kidogo hata kwa kujificha. Upendo wa dhati si mali, au uwezo.
Ni kweli upo `mfumo dume' ambao wanaume wanataka kila kitu wafanye wenyewe, wanapenda wawaone wanawake ni dhaifu, na wanapotokea wanawake wanye kauwezo/uwezo fulani, basi kwa uzaifu wetu wa `mfumo dume' tunatokea `kuwaogopa'
Ni ukweli usiopingika, `kutawaliwa' ni hali `nyonge sana' na jaribu kufiria wewe ulikuwa `kidume' sasa wewe ndio `kidume-njaa' umuoe, mwanamke mwenye elimu kama ile, uwezo kama ule...inakuwa taabu kidogo. Huu ni ukweli kwani wote tunaishi kwenye jamii, sio mbinguni au uzunguni.
Kwahiyo ninachotaka kusema (mimi)ni kuwa, heri yenu mumejaliwa kupata elimu kubwa, kipato kizuri na maisha bora kwa waliojaliwa. Sio lazima kuwa, maisha bora ya ndoa utayapata tu kwa mtu wa aina yako, mwenye elimu kama yako, au zaidi , mwenye kipatao kama chako au zaidi nk. Maisha ya ndoa bora ni pale unapompata mume/mke mtakayependana na kukubaliana kwa hali yoyote.
Ahsate, na nazidi kukuombea ujaliwe kumpata mume umtakaye, na mpendane na muishi kwa amani.
mimi emu-three
Michu,
ReplyDeleteYou are in the wrong business man, this should be a dating sight, where people meet and hook up. This lady is damn fine, too bad I am happily married!!!
Dada mzuri umejieleza vizuri ila poleee mchumba anapatika kwa Mungu piga magoti kwa huyo muumba wako muombe mume mwema nae atakupa kwani kwake kuna kila kitu ila eti kujitangaza mwanamke unatafuta mchumba haipendezi kabisa kwani we unaoa au unaolewa? kichwa ch nyumba atakuwa nani? mmmmm haipendezi kabisa mi nakereka sana !!!!! hivi akitokea siku mwanaume anatafuta mchumba hapa itakuaje? mmm pole dada
ReplyDeleteHaya vijana,Jovin kaweka na picha kabisa,na anaita kiuhakika.
ReplyDeleteKazi kwenu,msitoane macho tu!!
Way to go sis' Jovin,goodluck on your mission.Usife moyo kwani kuponda watu wataponda tu,haijalishi unafanya jema au baya.
mmmhh! haya mambo sasa kumekucha, aliyedhani ya kina manka ni yakupita basi ndio kwanza. Lakini ngoja! nikijipima hapo nafit vigezo viwili vitatu, sijui nijitose?! Ahaa ngoja nisubiri lala salama.
ReplyDeleteHapo Vipi?
ReplyDeleteMi nangoja ageuke!
Mwache Ageuke Uone Muziki Wake.....
haya bwana!
kazi kweli kweli,kitu kimetulia ila hayo masharti mmh.
ReplyDeletemmhhhhh, yangu macho tu...wadau; hii post ukiisoma btn the lines imemlenga mashaka...kila la heri dada...
ReplyDeletemimi nina sifa zote mcha mungu ,nina masters na nina umri chini ya miaka 35,nina kazi naishi mwenyewe,nitafute katika anuani hii tumainit@hotmail.com
ReplyDeleteMY X-GFRIEND UMECHOKA MPAKA UNATAFUTA MCHUMBA KWENYE BLOG HII....POLE,I USED TO LOVE U.TATIZO UNATAMAA SANA
ReplyDeletemmhhhhh, mashalaah mtoto weye ntakukaribisha kwa home japo hatujaonana
ReplyDeleteila nicheki kwa email yangu tuongee zaidi email yangu ni robsson1@yahoo.com
Michuzi sasa blog yako umeibadilisha na kua ya wauza sura?maana naona siku hizi si mchezo wauza sura wanapewa nafasi kubwa sana kuliko vitu vya msingi,Wahenga walisema ukistaajabu ya musa utayaona ya firauni pia nimeamini ya kua biashara ni matangazo my self najiuliza kwanini huyo binti kwa uzuri huo alokua nao akose mchumba??bt later nimegundua si bure kuna kitu hapo nahisi huyu binti ni matatizo.utaishia kuzalishwa tu...haya kazi kwenu wadau wa mambo yetu yaleeeeeeee
ReplyDeleteJovinata,
ReplyDeleteSifa zote hizo ulizozitaja mimi ninazo na nyingine za ziada ya hapo. Ni Masters ya Sheria kutoka Havard, nina kazi nzuri sana, tena nzuri mno.
Lakini na mimi ninahitaji msichana aliyesoma mwisho darasa la saba tu, au kama utakubali nikuweke ndani sitaki ufanye kazi yeyote.
Biashara ni maelewano
MICHUZI KAZI UNAYO KWELIKWELI MWAKA HUU, WATANI ZANGU WAMECHARUKA WANATAFUTA 'FITO' KWA BIDII.
ReplyDeleteway to go girl...
ReplyDeletehongera sana kwa ujasiri wako jovinata..
bwana asikwambie mtu,hao wanaume wanaoponda hapa wapo pia wanaosota kupata mwandani...hawajapata tu courage kama uliyopata wewe ya kuanika hadharani...
mimi nimeolewa na nilipata mume kupitia internet,ilianza kama urafiki tu wa kuchat, na wala hakuwa tanzania,alivyorudi tz tukameet,tukapendana,tukapima.. tumeoana na sasa ni mjamzito wa mtoto wa 2..tumeshakaa pamoja miaka 4 sasa,hatujapata tatizo lolote. so sikukatishi tamaa.
muhimu ni ukishampata,na kufamiana kwa muda..muongeze kigezo kingine... mkapime ukimwi.
all the best.
mdau,
mama to be.
Jovinata, kwanza nikupe HONGERA kwa moyo wa kijasiri, kuelezea NIA yako ya kutafuta mwenza. Wengi hapa wanashangaa mtu tena wa kike kutafuta mchumba kwa njia hii ya internet. Binafsi naona hamna tatizo, kwani hata mtu akipatikana, siamini kama binti MAKINI kama Jovi, anaweza kuparamia, bado ana vigezo vyake atatumia kujiridhisha kuwa aliyepatikana ni mtu aliyemhitaji!
ReplyDeleteSasa, mimi binafsi, najiona kama nina vigezo vyote ulivyotaja, Sijao, nina shule ya kiwango cha Masters, ni mcha mungu wa kiwango cha kutosha(mkiristo), nina ajira ambayo naamimi ni nzuri tu, huko Bongo japokuwa kwa sasa nipo kikazi kidogo nje ya nchi na pengine nitarudi bongo mapema mwakani! Na cha muhimu sana NIMEVUTIWA na wewe! Sasa kabla sijawasilisha RASMI maombi yangu, ningeomba unijibu maswali yangu mawili! Mosi, pengine utapata watu zaidi ya mmoja wenye sifa ulizotaja, je utatumia vigezo gani ili kumpata mmoja?? Pili, umeonekana kuvutiwa sana na Mashaka, sasa unanihakikishiaje kuwa hata nikibahatika kuteuliwa na wewe... Mashaka akitia timu, usalama wangu utakuwepo?? Naomba majibu ya maswali hayo mawili kabla sijatia timu... Na mimi kabla hata sijatuma maombi kwako nakuhakikishia ukinipata hutajutia... Ni mimi KubwaLao
huo ni uhuni dada alikwambia masters inaoa ni nani kam unataka mum huwezi kuwa so critical kam ivyo nway inaonekan una infatuation mana umri wako umesonga sana isipokuwa unaonekan kuwa huna msimamo kwani ndani ya maelezo yako unaoneka wewe ni lifesit sana no one kwa wanaume wa kitanzania atakae kuoa kwani watoto wadogo kibao halafu wew unajifanya kuwa upo so clitical sana pole sana,
ReplyDeletekwanza mpaka hapo wewe ni mbaguzi sana huwezi kuwa mcha Mungu halafu uaktoa maoni kam hayo,wewe ni mbaguzi vinginevyo uende uakatafute mume kwa saiz yako man upo siliazi sana wakati vijan wa kibongo hawaoi watoto walio nje kam wewe,
pole
jamani, dada amesema mkiristo yoyote anafaa, hakusema lazima awe lutheran, tusome vizuri jamani
ReplyDeleteHaha haha WAJINGA NDIO WALIWAO JAMANI HUYU DADA KAOLEWA NA ANA MTOTO NA MUMUE> HEBU ANGALIENI KWA MAKINI HIYO PICHA KWA JUU KUNA PICHA NDOGO MBILI, MOHA AMEBEBA MTOTO NA NYINGINE KWA PEMBENI YAKE NI YA MUMEWE. Michuzi siku ya wajinga si ilishapita au umeamua kufurahisha genge? By the way vi vyema mkatupa ukatu[pa feedback ya kina Manka na wengineo je wamefanikiwa???
ReplyDeleteJAMANI JOVI, HIYO PICHA NI YAKO AU YA RACHEL TEMU? anyways duniani wawili wawili...umefanana sana na Rachel Temu
ReplyDeleteDada, picha imetulia na wewe ni mzuri. Na elimu pia unayo. Hapo unastahili pongezi. Usiwe na wasi wasi na waosha vinywa; kila mtu ana 'choices' kwenye maisha na wewe una haki ya kufanya unachotaka. Nadhani ulitegemea baadhi ya responses za watu.
ReplyDeleteAnyway, mimi nilitaka kukupa mawazo na ushauri wangu. Kwanza, unaonekana your "first target" ni Mzee Mashaka, nothing wrong with that and go for it. Lakini jua kwamba wanaume pia wana wivu na pride. Sasa ukikosa "first target", itakuwaje. Mimi kama mwanaume sitakubali to go out with a lady ambaye mimi ninajua fika kuwa I am not her first choice. Hii huleta matatizo mengi baadae. Na nina uhakika ninaongea kwa niaba ya wanaume wa Kiafrika wengi.
Kwasababu bado haujaanza kuwasiliana na "first target", nadhani hujachelewa to retract (Obama anasaidia ku-improve vocabulary..msipime!..LOL) the request or whatever you want to call it.
Halafu, kwa binti zetu wengine, wakati mna-pursue degrees muwe macho pia. Kule ndio pa kupata watu kama mkiwa macho. Msiwe too focused on careers tu. Your jobs will NEVER make you happy.
Lakini usiwe na wasi kwasababu 28 bado mdogo tu. Tulia na mtu atapatikana tu. Bahati mbaya watu kama kina Mashaka huwa wameshakamatwa, na kama haitoshi huwa wametulia. Kwahiyo inakuwa ngumu, lakini kila kitu kinawezekana.
Du e bwana nimekubali dada Jovin kweli inaonekana wewe uko serious na hili swala maana umeweka hata picha yako, halafu vigezo venyewe ni ni vya kawaida tu, kwa hiyo hope utapata mtu unaye mhitaji.
ReplyDeleteHongera pia kwa kuwa muwazi kiasi hicho. Umedisclose mambo yako ya ndani sana, Iam very much impressed with you ingawaje kuna kigezo kimoja ambacho sina (Masters Degree), ambacho kinanifanya nishindwe hata kuingia kwenye mchakato.
Ila wasiwasi wangu ni kwamba, angalia kuna hatari ya kupata tapeli vilevile. Maanake ni rahisi mtu kujifanya ni mpole, si mlevi wa ngono, si mpiga tungi wa siku mbili, tatu kama ulivyosema, kumbe anapretend tu, akishapata kile anachokihitaji then anaishia, it will be another disappointment to you. Mi ningekushauri umwombe sana Mungu atakupatia mwenza wako anayekufaa katika muda mwafaka, you are still young and you have got much of the qualities that a woman deserves to have )especially visble ones) ingawaje hatujui tabia za ndani kama utu wa ndani, wema, upendo, uvumilivu, etc.
All the best,
Big Sam
onetwofo21@yahoo.com
Dada maelezo yako ni mazuri kuliko ya Manka na nakutakia kila la heri umpate Mchumba na hatimaye MUME. Kikwazo kikubwa kinaweza kuwa kazi yako na wanaume wengi huogopa kuoa mtu mwenye kipato kikubwa (Umesema unafanya kazi Shirika la Kuhudumia Wakimbizi-Nadhani ni UNHCR). Utafiti pia unaonyesha kuwa kwa wanandoa ambapo mmojawapo anafanya kazi UN, "divorce rate" ni kubwa. Lakini kwa kuwa unaonekana una busara na mzuri, utapata MCHUMBA karibuni. Inshallah.
ReplyDeleteWACHA KUTONGOZA AU KUTAFUTA MWENZA LIVE HUA AWAWEZI SO HII NI HALI HALISI MAANA KILA TUONAPO MAOMBI HAYA HUWA NI WACHAGA SASA TATIZO NINI??TUJIULIZE WAUNGWANA??HIZO MASTERS NA KAZI SIO TATIZO ILA MAISHA WANAYAWEZA YA KITANDANI HASA??NA SIO KUJALI KAZI TU NA PESA MAANA NDIO MILA ZA KICHAGA PESA MBELE.SO NI MANKA MWINGINE TENA.....UMESAHAU VIATU SIZE NGAPI AWE ANAVAA??
ReplyDeletesifa zote ninazo ila kwa kuwa wewe mchaga hata kwa bunduki na hata kama ni millionea nenda mama......utapata mtu ila sio mimi kazi hamwezi.
ReplyDeleteha hahahahahahahahahhahahahahahahahahahahahahaha !! Yaani I can not stop laughing from Joanita's post to the comments made! Thank you all for making my day ! WABONGO KWELI TUMEDATA BIG TIME .......... !!
ReplyDeleteJAMANI HUKO K'NJARO KUNANI????????!
ReplyDeleteMAKE TOKA HAYA MAMBO YAANZE NAONA WADADA WA HUKO WANAHAHA KWENYE MTANDAO KUTAFUTA WANAUME KWANI KAMA WAKO SAFI NA MAMBO WANAYAEZA SI WATULIE TU WATAFUATWA? NA CHA AJABU MTU ANAYEMTUMAINI MUNGU ANATAFUTA MTANDAONI? JAMANI KINA MANKA PUNGUZENI SPEED GOVERNER ZENU MAMBO HAYAENDI HIVYO MNATUAIBISHA WAKILIMANJARO WOTE.
Kwanini watu tunakua wanafiki kiasi hiki. Jovina una diriki kudai familia yako ni ya kidini na huku unaeleza kua ulishakwenda kwa kalumanzila... Ukweli uko wapi hapa?
ReplyDeleteNa dhambi ya kwenda kwa kalumanzila huwa haiishi, kwa hiyo yeyote atakae kupata atarajie utamlisha madudu (kuna mauchafu sana katika sanaa hii ya limbwata.
Haingii akilini kudai una masters degree halaf ni mteja wa kalumanzila.
Unatia kichefuchefu na hayo maelezo yako. Sijaoa na nina sifa zote unazozitaka ila naogopa kulishwa mauchafu.. Hunipati ng'o
Mimi bwana furaha yangu ni kwamba sasa wanaume tunagombaniwa,,hii iwe onyo kwa wanawake ambao wanaacha kutoa service za uhakika kwa jamaa zao,,inaleta changamoto kubwa kuona sisi wanaume wenye maisha yetu yaliyoonjooka ni deal sana..Bahati mbaya dada yangu mimi sipendi wabongo na mamixed kama nyie..mi nakula weupe tu,,makaratasi,,hamna majungu ya kina mwajuma na waganga,,wazungu wako juu hata kama mtakataa,,lakini ni ukweli ambao mioyoni mwenu mnaujua..aaaaaaaisee dada kwaheri.
ReplyDeletePole sana na hangaiko hilo.Husiwe na wasiwasi dada-wee.Wakati utafika na mchumba atapatikana nawe utashangaa.Hauko peke yako,ambaye anatafuta,na bado uko mchanga,hivyo jipe moyo tu na Mungu atakusaidia.Husikate tamaa,wewe vumilia na jinoe katika tabia na jinsi unavyoonekana,na wala husipende makuu ili wanaume waweze kukufuata.Jilinde hasa katika Tabia,mavazi,na huwe simple atapatikana.Ulizaliwa ili uwe na mme,hivyo jipe moyo.
ReplyDeleteWako,
Mwanakijiji
hivi ninyi wanawake akili zenu ziko wapi mnadayi mmesoma nyinyi mnashidwa kujuwa kama hiyo elimu iliyo nayo imekupa tu ujuzi wakutafutia liziki nawala haijakufanya kuwa bora kuliko wanawake wegine ambao wameishia la saba. sasa mimi kama mwanaume nina master au sina hiyo elimu yako itanisaidie nini katika kunipa haki zangu ambazo mwanamke anatakiwa kumpa mwanaume na wanaumeanatakiwa kumpa mke wake?
ReplyDeleteNIMEGUNDUA KITU, NA NASISITIZA TENA, kwa mwendo huu NCHI haitafika Popote, maana mmelalamika mafisadi wamekula ela ya mayatima na barabara, leo wewe usiye fisadi unamsikia mwenzio amepata shida au anashida unapondea, unasaidia nini sasa? isitoshe ametoa anuani yake, si wastaarabu tunajua cha kufanya, we unatoa tena anuani yako hap ili iweje, unamtangazia nani km unataka akuemail? Mi naona km WOOOOOOOOOTE kasoro wachache hamjajua maana ya shida na HAMTAFUNGUKA MACHO MPAKA MTAPOKUA NA AKILI
ReplyDelete(kwa ufupi mimi niliijua blog hii kwa kuambiwa nimeandikwa fisadi na sasa kila siku naifuatilia, naona upuuzi wa niliowaibia unavyoendelea, huwezi kumsaidia dada mwenye shida hata kwa mawazo, utaweza kuisaidia nchi yako kwa lipi? na kwa taarifa yenu, mtaishia hivyo hivyo, tuacheni wenye contacts za kina Bill Gates tule nchi, allllalalawaaah
Mwanahawa Ally anasema "..si bure iko namna..." Namimi nasema kizuri cha jiuza kibaya cha jitembeza! Mwanaume unaemtaka huwezi kumpata wewe, sababu huna sifa ya kuwa na mwanaume mwenye sifa hizo, picha na mkao uliotundika hapo, ian reflect tabia flan ambazo mwanaume sirias alie tayari kuwa mume hawezi kuzikubali, labda uwe demu wake wakuzugia, mwanaume mstaaab, mwenye elimu na kazi yake anataka mwanamke mstaarab, mwenye adabu na heshima zake, mtulivu na msikivu. Mwanaume gani mstaarabu anaetaka "sadaka lawe", umechezewa mpaka kushachoka ndo aje ajitwishe yeye balaa lako, ungetulia, ukajitunza chenza hilo huyo alolila mwanzo hakika angelichukuwa jumla, sababu kwa sura una sura mzuri, hivyo kama na tabia zako zingekuwa njema nna hakika huyo alomega chenza ange beba jumla, lakini sasa wataka utuuzie chungwa! Kunkula huuu..! Yaguju....!
ReplyDeleteDada unadai huna mtoto....hizo picha hapo ukutani sio wewe na mwanao huyo? Na hiyo ya pembeni sio Baba wa mtoto? Na hapo kwenye kutoa wanywa pombe, umewakosa wengi. Wamebaki wachache sana utakaowapata.....ila nahisi kama vile huu ni mtego. Hakuna ukweli wowote hapa. Hilo Carpet sio la Sudan.
ReplyDeleteKuna maswali kama vile 'Huyu mkeo kabla ya kuoana mlikutana wapi?'jibu: Oh hatukukutana ila alijitangaza kwenye blog ya michuzi alafu tukatuma maombi akanichagua mimi kwani nilikuwa na vigezo alivyohitaji.
ReplyDeleteAu:wakati wanamtoto wa kiume anaanza kuuliza swali ivi 'mama ulikutanaje na baba? Jov anajibu: kuwa uyaone mwanangu nilianzia kumtafuta baba yako kwa waganga wa kienyeji na nikamalizia kujinadi kwenye internet'.ooooops teh teheeeeeeee.madnes
koh koh koh kwanza nabanja ili nipate kuzungumza vizuri,hv dada huko kote ulikopita hujapata mwanaume wa kukuowa hadi umthumbue bwana mithupu?au unataka kuudha thura kama MANKA?Kama kweli ni mcha mungu funga na usali kwa ajili ya issue hiyo utapata na siyo lazima utuletee utumbo kwa blog yetu.Faza mdemi.
ReplyDeletehaaaa,jamani hako kademu nakajua vizuri sanaaaa kalikuwa ni kapenzi kangu mwaka 92 pale kishumundu ila tulipotezana mimi niko US nabeba box ila nilipata taarifa zake 2006 kwamba alishalambwalambwa sana na mzungu mmoja wa arusha ndo kamuunganishia UN, ni kakicheche mwitu hako ingia uonje msumari wa moto.
ReplyDeletebaba ubaya.
Well well
ReplyDeleteConsider me as a wild card
Your bit of rough as they say
Kwanza mimi ni mzee na kibogoyo na nina makengeza,na kiziwi kidogo tu, elimu ya dunia ninayo niliwahi kuwa porter kwenye soko la samaki, na dini sijua kwani. Je would you consider me and make my day
PS send me a few dollars I would like to arrange them arround your downloaded photo
Mdau
Nyie mnashangaa eti ni Wachagga tu ndo wanatokea humu! wanaangalia vigezo baba! hivihivi wametoa FIRST LADY! na mtabaki vinywa wazi wakitoa mama wa kwanza mwingine! Akina Dada wa makabila mengine mpo???? Nyie lazeni damu tu!
ReplyDeleteTatizo ni kwama unachagua mno! any way, ninachoweza kukushauri ni kwamba ungeelekeza nguvu kwa Mashaka, cause inaonekana wazi kwama ameuteka moyo wako kwa kuangalia tu picha yake.
ReplyDeleteThen be frank inamaana kwa uzuri woooooote huo huko UN hujapa mtu? au siyo handsome?????
Ok, vigezo ninavyo na nipo Dar, lakini mimi mlevi mno wa pombe, siwezi kulala bila kunywa.
Any way, best wishies for your seach!
Habari yako dada Jovinata, kama wewe mwamini Mungu kwanini uwe mbaguzi hutaki wazungu? Naomba nikuulize hilo, halafu cha kushangaza wewe mwenyewe ni jamii hiyo, kwanini sasa? Duniani wanajitahidi kuutokomeza upanguzi wa rangi na dini, wewe unatuletea sera hizo. Pia kwanini uende kwa waganga? Wakati unajua kabisa dini hairuhusu mambo hayo, wewe sio mkweli kuna lako jambo. Kama unamwamini Mungu, na mwanadini mzuri huwezi kufanya hivi. Nakushauri uwe mvumilivu utapata tu wako wa moyo. Ninakusalimu sana na kukutakia kila lakheri nyingi kumpata huyo unae mtaka. Ni Mdau wa siku zote hapa ndani,
ReplyDeleteCHIBIRITI.
mie nina sifa zoote, nitakuandikia lakini kabla ya yoote nataka kujua afya yako, je? umepima ukimwi? maana ulivyohangaika na wanaume hadi mume wa mtu aliyetaka kukufanya mke wa 3, mhhh! inabidi ucheki ngoma dada yangu...na wagangakibao? naambiwa waganga huwa wanaonja wao kwanza ilik kuweka dawa zao...je wewe ulikuwa wangapi kwa waganga? pima ngoma kwanza dada...
ReplyDeleteHapo ndipo tunaposema kuwa Uislaam unafaa maana umeamrisha kuowa mke zaidi ya mmoja unaona wanawake sasa wanatafuta wanaume wa kuwaowa na kila wanapopata wanakuta ni tayari mume wamtu
ReplyDeleteKijana wa Apr 3, 12:12 KubwaLao Unaonekana uko makini na unawasiwasi wakati unajiamini ulishasema akikupata hatajuta sasa nini tena, Mimi nijuavyo, ukiwa msichana unakuwa unapata maombi mengi na mpaka pale unaporidhishwa ndipo unakubali sasa wewe usiwe na hofu juu ya kumtaja Mashaka hapa yeye kama wasichana wengine anahaki ya kuvutiwa na kijana yoyote na kutamani moyoni kuwa huyu ningependa awe mume wangu, kama wewe unavyomtamani msichana na kumpigia speed, sasa ninachotaka kukwambia we onyesha juhudi yako tu kama umemaanisha kweli,kama sikosei mapenzi hayafichiki atapambanua yupi anampenda kwa dhati na yupi anajikongoja, na kama utampenda kikwelikwelii utaonyesha umahiri wako na utakaza uzi na Jovinata anachohitaji upendo wa dhati ambao hautakua na yale mambo ya ulevi uhuni na ukorofi kama alivyoainisha hapo juu.
ReplyDeleteSijui kwamba dada unakasoro gani kwani elimu nzuri unayo, kazi nzuri je? nini kinakusumbua? au unashindwa kutoa service nzuri kwa jamaa zako?
ReplyDeleteElewa kwamba unaweza ukawa ni mwanamke mwenye kila kitu lakini ukashindwa kutoa service ya maana kwa jamaa yako na matokeo yake unamegwa kisha mtu anaingia mitini.
Jaribu kurekebisha udhaufui huo unaweza utatoka katika dimbwi la kutoswa na mabwana.
Aisee Jovinata,hivi makasisi wa Kilutheri si wanaruhusiwa kuoa??
ReplyDeleteMi-nakushauri uangaliye uwezekano huo, angalau utaambulia UPENDO na AMANI ndani ya NDOA yako, kwani hawa Wanaume wa kawaida wa S.hizi waigizaji watupu,hawachelewi ku-fodge C.Vs.
**You Glow Girl!!
michuuuu mi nafkir ungeanzisha kasehemu kwenye blog yako ya watu wanaotafuta waume au sijui wachumba maana sasa ishakuwa tabu lakin inaonekama huyu demu nae ni mtu wa kushobokea watu ndio maana mijamaa inafanyiza inatembea ok au kuna watu wanatuzingua blogin? kama kweli kaumia aende makanisan akatangaze asituzingue sisi kama wasomi tushaona sana kama wenye kaz nzur ndo usiseme sasa kipi kipya,HATUTAK VIZEE
ReplyDeleteI will tell you this my dear sister, when my wife and I met, I wasnot the same person I am today, but she saw a potential in me, the reason why I was the way she met me, it was result of previous relationship, she took time to bring out the person she knew I was, the men you are looking for, they are all married or about to get married and it because somebody took time to work their men, Look for potential and not the best, God has blessed us with beautiful family, and succefull life, in foreign land. I ask you repent for reaching out to witch doctors instead of God, then ask God to bring a Man that He has for you! Keep God first, He is Alpha and Omega
ReplyDeleteMademu wa kibongo wana nyodo, yaani wanajiona masista do. Wale mabwana walioona ndo bab kubwaa wameshawachezea na kuchukua totoz umri mdogo zaidi. Sasa unajiona unazeeka, unatafuta mwanaume. Ulikuwa unafikiria nini wakati wanaume wazuri walivyokuwa wanakufuata, na wewe kuwatolea nje. Ndo maana mimi nimeamua sasa kutafuta demu kutoka nchi zingine za Afrika. Nyie kaeni na u-much know wenu tuu!
ReplyDeleteDon't judge a book by it's cover!
Nipe Mwaka 1 na nusu nipate Masters ya Telecommunication Engineering.Vigezo vingine safi,ingawa pia kuna kufanya adjustment kidogooo ile niwe mkamilifu kwako.
ReplyDeletekaygee_@boni@hotmail.com
Wadau mimi nanachokiona hapo katika hiyo msg ya huyo mwana dada anabagua wachumba ndio maana anakutana na wahuni kila mara kwa sababu haiwezekana kwamba alipotoka mpaka alipofika hajawai kuwa na mwanaume au wanaume labda hikcho kikazi chake kinamfanya awe na nyodo na sikufichi unayetafuta mume kwenye internet nvigumu kupata mkweli kama huamini ww endelea kutafuta wastarehe na ww kisha wanakuacha
ReplyDeletekatochi)
EBWANA HILI BONGE LA ALUTA CONTINYUA NA SHANGAA WATU WANAMWAMBIA HII SIO SEHEMU YA UCHUMBA AKATI ISSA MUHIDINI MICHUZI KASEMA VIZURI WAWEKE PICHA ZAO.KAZI KWENU MASELA WA KIKRISTO KAMA UNA MASTERS CHUKUA JIKO TOTO LA KICHAGA SEMA MTAFUTE BACKGROUND YAKE PIA MAANAKE SIO KILA KINACHONG'AA NI DHAABU.ALAFU KITU KIMOJA DADA KANIKATISHA STIMU NA KITENDO CHAKE CHA KWENDA KWA MGANGA,MCHA MUNGU GANI ANAENDA KWA MGANGA? KWA NINI USINGEOMBA MUNGU NA INSHALLAH DUA ZAKO SIKU MOJA ZITAJIBIWA NA ATAKULETEA MCHUMBA AMBAE UNAMTAKA? NAKUASHAURI ENDELEA KUMUOMBA MUNGU SANA NA SIKU DUA YAKO ITAJIBIWA NA ATAKULETEA MCHUMBA.
ReplyDeletemichuzi ni kuwadi mzuri sana.
ReplyDeleteJamani wewe dada hapa sio mahali pa kutafuta mchumba.utatoka na matusi hapa mpaka ukome,,,hivi umekosa kabisa mchumba?ebu wasiliana na mimi email yangu ni rnkaisiswe@yahoo.com mimi ni mchagga mwenzako nitakusaidia.
ReplyDeletekyekue
Dunia ya sasa si kama ile ya mwaka 47 hata mademu sasa wanajiuza mtandaonix2 fanya utakalo michuzi atakurusha mamen utapa mademu hutakosax2 wo wowow!!!!
ReplyDeletewabongo bwana mwenzenu akwia na shid abadala mumsaidie maneno na wivu hata nje ya nchi, ndio maana hatuendelei unakuta mtu ana shida, watu wanafurahi, sasa wewe dada umekosa kabisa hata wasudani uko uliko???
ReplyDeleteHaaaaaaaahaaaaaaaa..nimechecka mpaka nikaachia kabomu kadogo na jirani niliyekuwa nimekaa nae ikabidi apane pua....
ReplyDeletewewe una ubini mzuri KILEO...a.k.a kinywaji halafu kwenye term of reference (TOR) hutaki mwanamume anayechukua KILEO...
naona hutaki kuolewa!!
kwani ungetaka aanayechukua KILEO ungepata wengi na kwa vile nawe upo kwenye kundi hilo ungebahatika...au nimekosea!ALL THE BEST!!
Huyu demu mzushi
ReplyDelete1. Anamtaka Mashaka, bila kujua Mashaka kuwa bachelor haimaanishi kwanza hana mchumba... anyway lets assume that hana mchumba, inamaana hata akikukubalia, Mashaka siku akija anachukua kama mzaha.
2. Anataka mtu ambae atamzalia watoto wake (sijui kama mmegundua amesema hivyo). Hatafuti mume ila mashine ya kumzalisha watoto. Inamaana utakuwa huna lako hapo...
Anyway, all the best....japo nina qualify... though am a RC with masters.... n' planning kurudi ku-settle Bongo later this year... Ukirekebisha hayo 2 juu tunaenza anza....ila nimesahau pombe nakunywa sana
SASA NIMESTUKIA KITU KIMOJA HAPA BWANA MISUPU...YULE MASHAKA KUMTOA HAPA NI KUJITANGAZA KIAINA KWA WAREMBO....SEMA KAINGIA NA MKWARA WA KUTOA MISAADA NA KUISHI MAREKANI,,,NA WEWE NANI UNAITWA TAMAA ITAKUPONZA KWANINI UJAMTAKA KIBILITI NA KILA SIKU YUMO HUMU????KISA HANA TV??????TULIA MTOTO UTAPATA HUKO HUKO SUDANI...MDAU 00316
ReplyDeleteBRO MICHUZ SHUKRAN KWA KUJIBU MAOMBI YANGU KWANI NILIOMBA MMUNGU ANIPE BIBIE COLOURED NA MPENDA MUNGU, MIE MMASAI BWANA LAKINI NAAMINI HATUTOSHINDWANA DADA. MPATIE EMAIL YANGU ANIBIP.
ReplyDeletemeleji@yahoo>co>uk
hahaha, it aint getting no better than this aisee inabidi nisifanye haraka kumbe sasa hivi soko letu liko juu
ReplyDeletekwa jovinata dada naona ume-base sana kwa mashaka kwa hiyo goodluck siwezi kuwa second/just another choice
halafu haya mambo yako ya sangoma yanarusha stimu kiaina usije lisha mtu limbwata akawa zezeta hiyo haijasimama kwenye mstari
halafu mitungi wakaka wengi tunasukuma kiaina occassionaly ila hatujabobea(sio chaulevi)
goodluck with mashaka
NIMESOMA COMMENT ZOTE WAKATI NAKARIBIA KUMALIZA NIKAONA KUNA MMOJA TU NDIO KAONGEA POINT>>> BIG UP ANON HUYU>> Tarehe Thursday, April 3, 2008 2:02:00 PM EAT, SIJUI KAPATA WAPI AKILI HIZI.. BIG UP SANA.. HIVI BAADAE BAADA YA HAYO MTAKAYOYAITA ,MAPENZI KUKOLEA WATU WAKIWAULIZA MLIKUTANA WAPI MTAJIBUJE.?? LETS MAKE IT U R KID ASKS.. HAPO SI NDIO DIZASTA?? MAMA ,MIA..
ReplyDeleteAND LET IT BE A WORNING TO ALL THEM GALS WHO TREAT THEIR MEN WRONG.. JAMANI MTAKE MSITAKE.. NYIE MLIO KWENYE NDOA NA UHUSIANO.. MNAONA WENZENU WANAVYOTAPATAPA? KUWASAKA WANAUME.. HEBU KUWENI NA ADABU ZA KUTOSHA NA KUTIMIZA YALE MUME ANATAKA AS WEL AS NA YEYE APROVIDE FULL SERVICE..
MI KWENYE WANGU NISHAWAHI KUAMBIWA HII SIYO 'ONE SIDE GAME MI NA WEWE TUKO SAWA.' MKE ANAMWAMBIA MUME HUYO. NIKAMUANGALIAAAAAA HALAF KIMOYO MOYO NIKASEMA HIVI NIKUACHA ATAKUOA NANI WAKATI NISHAKUTOA DOA???? POLEEE.. NA KWELI NAMUACHA..
Du mtoto nimekumaindi!sifa karibu zote ninazo, nina-hold Masters degree, mimi ni mlutheri, nina miaka 30 na sijawahi kuoa. Ila tatizo ni moja tu Baba yangu Muingereza na mama ni mchagga!Nimekulia pale Moshi shanty!Nilifikiri ubaguzi nakutana nao Ulaya tu, kumbe Bongo ubaguzi upo wazi hivyo mpaka kwa maandishi? Basi bwana isiwe taabu maana familia yangu ipo diverse kama ya Obama naona ingekuwa matatizo tu, maana nina ndugu wazungu na wengine .5 vile vile na wewe watu hao unawabagua. Lakini no sweaty, all the best.
ReplyDeleteAm Confused, puzzled and befuddled
ReplyDeleteChakunishangaza ni hoja za watu kwa mlimbwende huyu, firstly, I would like to complement on this discussion by asserting that “Globalisation is not optional” haya ndiyo manufafaa ya utandawazi.Sisi tuendelee kushangaa tu na kustaajabu kwamba mwanamke hawezi kuchangua mwenziye, ha ha ha ha!!! Ninachodai hapa ni kwamba kasi ya mabadiliko duniani ni kubwa na lazima iathiri mifumo yote, kwani hamshangai hata idadi kubwa ya wamasai wametupa rubega, siku hizi ni mwendo mdundo tu kama ndivyo mwacheni binti achague kwa taste yake.
Ni kama mimi ninamalizia PhD in two months time, lakini mke wangu niliyemuoa aliishia darasa la Tano, watu hunishangaa lakini mimi ninampenda na familia yangu wote wanamuenzi, kwa upendo,ukarimu,ubinadamu,hekima na busara.This is neither a joke nor a trump up story.Ni ukweli halisia na wala sijawahi kuyajutia maamuzi yangu kuchagua ni kupanga.
Perception ya mapenzi ni pan asana sina haja ya kutundika gazeti zima.Sasa naona mada za kumshambulia binti ya watu, hata nyie mnaruhusiwa kama unataka kuoa amaunatafuta mchumba wa pili kama mzee Maulid wa Kitenge.Kwani watu huoana wanapounganishikanika na kukutania, ndiyo maana hata wanakwaya huanza kuchumbiana,padiri na muumini, daktari na nurse ama mgonjwa, polisi kwa polisi ama mtuhumiwa.Hivyo blogu hii ndiyo makutano ya huyu binti na wanajamii.
Tunaomba mawazo endelevu muache kunyanyapaa na kukandya.
Dr. Confusion
Tarehe Thursday, April 3, 2008 2:02:00 PM EAT, Mtoa Maoni: Anonymous
ReplyDeleteKuna maswali kama vile 'Huyu mkeo kabla ya kuoana mlikutana wapi?'jibu: Oh hatukukutana ila alijitangaza kwenye blog ya michuzi alafu tukatuma maombi akanichagua mimi kwani nilikuwa na vigezo alivyohitaji.
Au:wakati wanamtoto wa kiume anaanza kuuliza swali ivi 'mama ulikutanaje na baba? Jov anajibu: kuwa uyaone mwanangu nilianzia kumtafuta baba yako kwa waganga wa kienyeji na nikamalizia kujinadi kwenye internet'.ooooops teh teheeeeeeee.madnes
Huyu mshikaji kanifurahisha sana...
"LMAO"
kwanini uulisema umevutiwa na mashaka wakati hata humjui umeona tu picha yake na kijana hodari ndio umevutiwa nae? kama yeye hana sifa kati ya hizo ulizozitaja hapo juu inamaana hana neno utamkubali tu?inaonekana wewe unaangalia umarufu na elimu tu hayo mengine wala huyazingatii kuwa makini dada usivamie tu.jaribu kushauriana na wazee wako kwanza kuwa unatafuta mchumba awe wa aina fulani sasa wao watakusaidia kukutafutia kwa njia nzuri sana na ya utulivu ikiwa ni jamaa au makanisani au maofisini,wazee ni watu wa hekma
ReplyDeleteKuna MBWIKO mbili zimetoa toa mail zao hapa duh....
ReplyDeleteEee bwana wazee mlioacha email zenu kweli mnapenda vya kunyonga vya kuchinja nyie hamtaki kabisa duh... Haya jitahidini labda mtabahatika na ufinyu wenu wa fikra
CHIBIRITI UPO WAPI MCHUMBA HOYOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
ReplyDeleteNA WE DADA UNA MASHARTI NAFIKIRI UNATAFUTA MTUMWA NA SI MCHUMBA UTAKUFA SINGLE AU MTAFUTE CHIBILITI
DEAR WOMAN, DO NOT WORRY JUST BECAUSE YOU ARE 28YRS OF AGE IT DOES NOT MEAN YOU ARE OLD AT ALL AM 34 AND BEAUTIFUL NEVER MARRIED AND NO KIDS BUT AM NOT DESPERATE AT ALL, WHEN YOU ARE DESPERATE YOU END UP WITH CRAZY MEN OUT THERE. KUMBUKA KUNA MAUKIMWI KILA KONI UKANYAGAPO..SASA NA WEWE LAKINI EBU TUONGEE KWANINI UNAJITAFUTIA BOYFRIEND HADHARANI HIVYO,?? MUOMBE MUNGU ATAKUSHINDIA MPENZI WANGU USIWE NA PAPARA AU PUPA... I WILL PRAY FOR YOU AND YOU WILL GET THE ONE.... KEEP YOUR HEAD HIGH..
ReplyDeletekaka misupu hii blog sasa ni kichekesho kushinda ze comedy maana maoni na sura tunazoona na akili zao na size za viatu basi mbavu sina maana,sasa huyu msichana anazungumzia wagaganga then anataka mcha mungu mbona mashaka matupu na kuwa sudan ndio kwenda sehemu yoyote maana mikwara mingi kwa misupu hapa uwezi pata mtu ila soma maoni kuna mengi ya kujenga sana kama utatumia akili
ReplyDeleteWanawake wa Kichaga miyayusho. I have dated one, waaaay too much pride and control freaks, eventually I couldn't keep up with them and I wanted out ASAP.
ReplyDeleteNow, we are seeing a trend of wachaga kutafuta ndoa humu ndani because none of us want nothing to do with them. Ila I know few wachaga ladies ambao wako down to earth, so am not generalizing, but the few that I encountered ni noma.
Mdau mmoja alisema Obama anaimprove vocabulary, ebwana I second u kichizi, Look, "folks" are using bigger words straight from Obama stump speeches to vehemently reject and denounce all these cynics rhetoric kuhusu kutafuta mchumba kwa michuzi. Usipime influence ya Obama, ni soo.
Back to huyu mdada, Goodluck, mi am single ila malaya flani. I don't qualify, besides am not ready "kuwowa"..either way kila la kheri
Tumekona dada! Biashara matnagazo eti siku hizi!!!! Taarabu imo?
ReplyDeletehayaaweee kunani huko maranguu jamani mtoto wa manka huyu jamani wabeba maboksi mwaibiwa mwaka huu wachaga wataka madume.
ReplyDeleteUnatafuta mchumba au unamtaka john mashaka, we mdada yatakushinda kama kuona picha ya mwanauume mwenye mafanikio ya kizushi "promote by wanahabari" unababaika je ukikutana live na mapedejee si watakusukuma kizazi the same day, angalia.....!
ReplyDeleteMichuzi ushauri wa bure, wazungu wanasema "free consultation", hebu anzisha dating website ya wabongo, halafu unalipisha watu kuwa members (initial thirty days free), inaonekana wateja wapo wengi tu...
ReplyDeleteDili hilo mwanangu...
Dada kajifungie ndani kwa siku ka mia hivi, sali, fanya kazi, fanya mazoezi, saidia wenye shida. Halafu ndio uanze kusoma e-mails utazopata, au utoke na staili nyingine...
ReplyDeleteWarning: FRAUD on African/black Dating sites
ReplyDeleteSeveral dating sites (including many aimed directly at the African/black community) has a high percentage of FAKE profiles posted. Many users are not aware that the person writing love letters to them through dating sites is not always what he/she appears to be.
From what I haven been told by several users, the fake profiles are probably made only for one purpose: to cheat naive men into sending money to the person hiding behind a false name and picture. The excuses used are money for an airline ticket, hospital treatments, school fees or similar. The love-seeking men will never see their money again and surely never see the person they thought to be mailing with. The profiles are hiding behind fake pictures and who knows... often the beautiful young woman is in fact a man. There is some patterns to see in the way the false profiles are used and it gives the impression that these are pretty well-organised frauds.
These people are just looking for easy cash, so.... be VERY much alert and aware if you are using online dating sites. It is very easy to be fooled on the net and pictures doesn't always tell the truth.
Fake photos
I was made aware of this problem after users telling me that some of my portraits of African women has been stolen and abused on dating sites and online forums. This was obviously never the aim of my photographs or the wish of the models posing. In most cases the fake profiles was deleted promptly by the administrators after I contacted them. But sadly they often pop up again later under a new profile name. The problem is extending and I get new reports of abused pictures almost EVERY DAY! My photos are obviously not the only photos being abused online so watch out on the dating sites.
CHEMA HUJIUUZA KIBAYA HUJITEMBEZA.KILA KINACHONGARA SI DHAHABU.JAZENI WENYEWE
ReplyDeleteWe Michuzi hebu acha Utani APril Fool Ishapita!!! niunganishe mimi nataka kuja bongo kuoa!!
ReplyDeleteJovin
ReplyDeleteI wish you all the best, usiwasikilize wanaosema sali tu alafu ukae chini usubiri mtu ashuke kutoka angani, as a christian you pray, seek and you shall find, so usali and continue looking, continue making your efforts kila siku, too bad uko sudan ungekuwa bongo ningekushauri ku-socialize more, that way ungekuwa na bigger chances za kukutana na watu, all the best.
Mie nishakutana na watoto wazuri kama huyo lakini kitu kimoja najua kwamba; mchagua mabucha nyama ile ile.
ReplyDeleteHuyu keshaenda kwa waganga, ushirikina tayari sasa mie na 'Mashaka' ukimpata huyu limbwata juu.
Abiria chunga mzigo wako.
Mwanafunzi mganga asilia,
K.T
hongera sana dada kwa kutambua hali yako na kuwa tayari kupmbana nayo. naamini utapata unachotafuta.
ReplyDeletejamani msimshangae huyu dada kwani huko alipo sio rahisi kupata mchumba. wote huwa ni wapita njia. lakini waweza kuchukua haohao na kuwaweka unavyotaka. najua huko ni non family duty station ila kabana nao.
kuwa makini vile vile wachumba wa mitandao ni hatatri. mfano waweza kukaribiswa huku hata ukae mwezi huwezi kumjua kwa kina. mfano mie nafanya kazi ubelgiji kwa mwaka sasa na sijaenda nyumbani. unaweza kudhani sina mke kumbe.....
haya utafutaji mwema. kumbuka hizo pesa zako ndicho chanzo cha tatizo lako.
I never thought i will be doing this. I give you a big thumbs up for doing this.Mimi naomba tuwasiliane kwa email and tuone mambo yatakavyokua na labda tutakuwa marafiki. Mimi ni mtanzania ninaye ishi USA na kufanya kazi huku na pia ni raia wa huku sasa. Natafuta mtanzania maana hawa wazungu hawana cha maana. I always want to post my add at Isaa michuzi blog but afraid.
ReplyDeletelets keep in touch na unaweza ukanitumia email kwa raphymoss@yahoo.com
i hope we can be friends. By the way napenda sana unachokifanya huko Sudan. Nilikuwa nasoma kitabu cha angelina Jolie kuhusu refugees na pia niko active na save darfur coalition.
Anyway keep in touch and i will tell you more about me and what i do and exchage photos.
Hi,
ReplyDeletei give you a big thumbs up for doing this. Mimi siwezi kuamini kuwa ninaandika hapa. Nilizaliwa Tanzania lakini ninaishi America na pia ni raia hapa. Nina umri wa miaka 31 na ninakazi, sina mtoto bado na this time natafuta mtanzania.
I really like that your in Sudan and help refugees and i am active with Save Darfur coalition. Let keep in touch and you can email me at raphymoss@yahoo.com na labda tutakuwa marafiki.
i really like kuona strong women kutoka Tanzania.
Hii picha nina uhakika itakuwa imeibiwa somewhere kutoka kwa mtu ambaye si Mtizii.Comments zote hakuna aliyemtambua binti kuwa ni nani, anakaa wapi?alisoma wapi?alifanya kazi wapi , kabla ya kwenda huko aliko.
ReplyDeleteMdau, mtoni kijichi.
we binti tafuta hata wasudani kwanza, ukikosa ndo tafuta kaka zako wa kitanzania. lakini usife moyo endelea tu utampata mwenzako.
ReplyDeleteHuuyo aliyeandika I can bet a hundred pounds si yeye...si kazi mtu ame copy and paste picture ya mtu mwingine toka internet halafu katuma..
ReplyDeleteHongera huyu ni shujaa mwingine tena aliyeweza kujitokeza, and you look good on your photo. Husband or wife sometimes hawapatiakani kwa urahisi, just that person you can share hapiness and sadness with. Please keep doing what you are doing and also be positive, and when you meet me please say goodmorning or just make mylife easier, I will respond. Some mila zimepitwa na wakati and there is nothing wrong to search for your husband. Aliyeko juu mpandie huko huko! na aliye chini inabidi sometimes umshukie. xuma70@yahoo.com
ReplyDeletepole sana jovin,najua ulienda kwa mganga kwa kuwa ulikuwa umekata tamaa ya maisha,hiyo nakusifu kwa kuwa umegundua tatizo lako,always mume hatafutwi kwa waganga wa kienyeji,na ukimpata ni balaa huyo hawezi kuwa mwema mume uliemtafuta kwa shetani hata siku moja.ushauri wangu kwanza tubu kwa Mungu kutokana na kitendo ulichokifanya cha kwenda kwa mganga,maana hata biblia inasema na alaaniwe yule amtegemeaye mwanadamu.nenda kwenye maombi omba Mungu tubu kabisa hiyo dhambi na uache kabisa.Mungu atakupatia jovin ila mweleze Mungu hitaji lako kwa huyo mchumba umtakaye naamini atatenda tu.
ReplyDeleteNikupe mfano mimi mwenyewe nilienda kwenye maombi kuombewa nikamwomba Mungu anipatie mwanamme mwenye vigezi vipendavyo then nikangia kwenye internet kuweka profile yangu.nilipata interest nyingi sana toka kwa wanaume kila kona ya dunia,wala sikukurupuka kwa kuona interest kibao ila niliamini yule ambae Mungu amenichagulia nitamjua tu,na kweli kati ya hao wote akatokea mmoja mwenye sifa ambazo nilimwomba Mungu.tukameet nae tukadumisha urafiki zaidi baada ya mwaka na nusu kufahamiana vizur tukaamua tuoane,nakupa moyo dada maombi ni silaha ya kila kitu.tumeoana na tunapenda sana ukimwamini Mungu anafanya jovin.achana na waganga kabisa ni waongo na hawawezi kukupa mume hao.
umenigusa sana jovin hongera kwa ujasiri,nakuombea utafanikiwa
by Ms BEN
HONGERA SANA JOVINA KWA UJASIRI WAKO HUU ILA NAOMBA NIKUAMBIE KITU DADA YANGU MCHUMBA AU MUME HAPATIKANI KWA NJIA HIYO ILA KWA KUSALI NA KUMUOMBA MUNGU MAANA MKE MZURI AU MUME MZURI HUTOKA KWA MUNGU WEWE NI MKRISTO NAAMINI UNAFAHAMU MANENO HAYO TOKA KTK BIBLIA SO NINACHOKUSHAURI NI KWAMBA PIGA GOTI OMBA MUNGU KWA BIDII NAMINI MUNGU WETU NI MWEMA NA ANASIKIA HITAJI LA KILA MMOJA WETU NAAMINI ATAKUJIBU NA UTAPATA MUME MZURI NA UTAFURAHIA MAISHA YA NDOA ILA NAOMBA UJUE KWAMBA KAMA UMEKOSA MUME SEHEMU ZOTE UNAZOPITIA( NAMANISHA MITAANI , OFISINI,SHULENI) KUPATA MUME KWENYE NET SIO RAHISI NA VINGINEVYO UTAOPOA MATAPELI PILI NAOMBA UELEWE KWAMBA KILA BINADAMU ANAMAPUNGUFU YAKE HATA WEWE UNAMAPUNGUFU YAKO AMBAYO YATAMKWAZA HUYO MUME UNAYEMTAFUTA. JARIBU KUWA MVUMILIVU .
ReplyDeleteNajua Brother Michuzi bado hujatimiza nguzo za kiislam kwa kuoa mke wa nne, tafadhali bro chukua huyu mtoto wa kike hata kama huna Masters atakufaa kutimiza nguzo.
ReplyDeleteHuyu hana tatizo la mwenza(MUME) kwani vigezo alivyoweka ni vigumu kwa binadamu wa Kitanzania wa maisha haya. Namshauri hapunguze hivyo vigezo visivyo vya lazima.Hongera sana kwa kumsaidia huyu Mrembo.
ReplyDeleteplayer haters mnachuja maoni haya tunawapa link za info alafu mnabana posts na dating sight yenu haya
ReplyDeleteUSIKATE TAMAA, WATU WENGI TU WAMEPATA WAUME KUPITIA NJIA HII, NA WEWE UNA HAKI YA KUTOA SIFA YA MWANAMME UNAYEMTAKA, WALA USIWASIKILIZE WANAOKUPONDA HAPA, WAMEPITWA NA WAKATI, HATA WANAWAKE WANA HAKI YA KUCHAGUA, KWA NINI WAO WACHAGULIWE TU! KOSA LAKO KUONYESHA WAZI KUWA UMEMPENDA MASHAKA, HAPO UMEFANYA KOSA, WEWE UNGEACHA NA KAMA MASHAKA ANGEONA UNAMFAA ANGEKUTAFUTA MWENYEWE, HAPO UMEWAKATISHA TAMAA WALIO WENGI,PIA HAKUNA MWANAMME ALIYE PAFECT KILA MMOJA ANA KASORO ZAKE, KUNA ZINAZOREKEBIKA, SWALA LA KWENDA KWA WAGANGA ACHANA NAYO KABISA,MAPENZI YA DAWA HAYADUMU, NI MUDA TU, USIRUDIYE TENA, SUDANI9 NAKO KUNA WAGANGA KUMBE!DA, NAKUSHAURI UACHE MDOGO WANGU, PIA UMRI WAKO BADO KABISA, WASICHANA WA KICHAGA HUWA HAWAPENDI KUOLEWA MAPEMA SIJUI KWA NINI WEWE UMEKUWA TOFAUTI NA WALIO WENGI HUKO MOSHI. BADO MTOTO WALA USIJALI.
ReplyDeletewewe anoy unaesema hawezi pata mume kwenye net unakosea mie nimepata humo humo kwenye net na tunaishi vizur na mume wangu hatujui kitu kinaitwa ugomvi kwenye ndoa yetu,acha kumkatisha tamaa mwenzako,kama anaomba Mungu na Mungu ndie wa kumsaidia apate mume kwanini isiwekezane?ndio ile mtu unaomba alafu una imani haba huna uhakika na unachokiomba kama itakuwa kweli au?tuache tumbip Mungu,kama unaomba kuwa na imani. Mungu anaweza kujibu ndani ya siku 1,mwezi au mwaka,dada we mwombe Mungu huku ukiendelea kutafuta naamini utapata either hapa kwa michuzi au kokote kule amabpo Mungu amekupangia utakutana nae.all the luck my dear sister
ReplyDeleteby MRS INTERNET
swala ya kupunguza vigezo mimi siliungi mkono sana ila naweza tu kushauri tumia busara zaidi kwenye maswala ya shule unaweza pata mwanamme mwenye vigezo utakavyo lkn akawa labda na degree 1,sio kwamba hataki kufanya masters lkn labda kuna kitu anafanya kwa sasa lkn ana mpango wa kuendelea na masomo tena.hata mimi mwanzoni wakati natafuta mchumba nilipenda wa masters ila nilimpata tulieendana ambae alikuwa na degree 1 na mimi degree 2 ila alikuwa na ambitions za kuendelea kusoma zaidi.tukaoana na baadae akaendelea tena na masters.kwaiyo nashauri usikomae sana na masters dada yangu kama ukipata mnaendana ana degree 1, masters sio tatizo ataipata tu.mafanikio mema
ReplyDeleteMichu kama nikipitwa na hii na bila kukandamiza maoni basi naacha kutembelea blogger nimeamini siku hizi muwidwa huwinda haya jovinata nakutakia mawindo mema.
ReplyDeletesamahani dada kwenye ndoa halisi hakuna masters unless otherwise unatafuta show off. watu wote waliofanikiwa katika maisha ya ndoa wakuona wakiwa nahizo masters unazotaka please grow up
ReplyDeletemichu!!!!sasa ndoto zangu zimekamilika,mdada mzuri kajireta mwenyewe!!!sasa basi,sifa alizo sema zote ninazo!!!ila moja tuu!ndio sina!!yani dini)sasa sijui itakuwaje!!ila kwa kweli mtoto yuko bomba sana anafaa kuwa my wife wangu,sasa basi kama kweli unasoma hii cmmnt yangu chukua nambar yangu ya simu ok 821086802140,tuwasiliane???
ReplyDeletehataki wazungu kwa sababu wemepoa, wamepooza kwa kweli. si unajua rangi nyeusi oyeeeeeeeee. joto.
ReplyDeletekwa reaha zako dada.
jamni mwacheni aseme yaliyoko moyoni mwake. Cute and beuty mmeona? cute yule brother aako vipi hana master?
ReplyDeletemhh bora fulani aliondoka sudan angeanza bure kumtolea macho.
cute and beuty did u see it. kazi kwenu.
ReplyDeleteJamani kumbe tuko wengi...
ReplyDeleteIla mimi naamini Mungu ndo atatusaidia, kila kitu kwa mda wake, kusoma sana maandhara yake mengine ndo haya. Dada Jovina, to be honest nakupongeza kwa ujasiri, unaonekana kweli you have nothing else to loose.
Ila be patient, inshallah Mwenyezi Mungu atakusadia, pia
a) Usijachague sana (shule na roho nzuri vinatosha)
b) Vuta subira, mda nao una matter mno
c) Tuliza moyo wako na chunguza vizuri waliokuwa karibu yako bila kuweka zile judgments zetu (anafaa..hafai..mlevi..hajatuliaa..ana mwanamke mwingine...hajasoma..hanielewiii..etc.)
Wewe ndo utakuwa LEADER YA GAME,WEWE NDO WA KUMBADILI NA KUMFANYA AWE THE BEST EVER!
Usisahau kuwa Nyuma ya Kila Mwanaume Bora ni Mwanamke...sisi ndo wapishi jikoni!
Nakuelewa sana kwasababu niko katika position yako, nimesoma, na kazi nzuri ila hupati kile unachotaka kweli kweli.
Sala na Subira ndo mali mda huu dada Jovina!!
Hi ndo advice yangu!
Wanaume mpoooooooo ... ???
POLE SANA DADA JOVINATA KWA WATU AMBAO HAWAKUTAKII MEMA, NAPENDA HAO WATU WANAKUTUMIA SMS ZA MATUSI WAACHE KWANI NAWE UNATANGAZA BIASHARA YAKO KAMA WANANYOOFANYA(TIGO,VODA, ZANTEL..) WAJUE KWAMBA BIASHARA NI MATANGAZO. NINAMPA SHUKRUNI NYINGI BROTHER MICHUZI KWA KUKUTANGAZA.
ReplyDeletePole sana dada jovin, wewe umri wako bado mdogo sana lakini kwa nini umekata tamaa hivyo? Mimi nakushauri vuta subira na kama unataka mtu wa kukuoa basi usichague sana vigezo ulivyoweka ni vingi sana na kamwe huwezi pata kwani watu hakuna aliye kamilika,
ReplyDeletewahenga walisema mchagua jembe si mkulima. na hata kama unamtaka huyo mashaka basi ujue ata ku undergrade kwani ataona umembabaikia,
Anyway mimi nakutakia kila la kheri na kuwa mwenye subira.
Nakukukaribisha kwenye kambi ya wanandoa ila inahitaji uvumilivu na subira si pakukimbilia.
Mtanzania
S Farahani
wanaume hawatafutwi kupitia huku tafuta njia nyingine dada yangu huku utakua unatafuta matusi na maneno kutoka kwa watu...mimi john is mine na kutokea kwake kote huko si kwamba anatafuta wanawake hapana tafuta njia nyingine ya kutafuta wanawake sio hii.....
ReplyDeletejovin dear we koma naye michuzi tu misupu poa sana huyu au cute boy kikwete utapata raha ya dunia.usiwafuate wenginew wababishaji wasio wasomi hawa wawilli nakupa gurantee watakutunza utuzike kimwana kama wewe take my advice dear please.
ReplyDeleteWee dada, kwa ushauri wangu. Hachana na watu maarufu kama Mashaka, hauwawezi. Rudi kijijini Moshi utampata mume. Hebu fikiria kufukuzana na mademu wa kibongo waliovyo wajanja, huyo mashaka wako siku moja tu kashaopolewa hivi hivi unaona. Kila la kheli
ReplyDeleteMochiro
Kwanza Hongera Dada kwa Mengi.....
ReplyDeletePili Nadhani ungetafuta tu mchumba mwenye akili na busara anaweza kupewa sifa ya Mume, Elimu na Mengine Mtaangalia baadae.
Tatu,Watoa maoni mmmejuaje kama hiyo picha ni ya huyo dada J? na je ni lazima kila mtu anapopigia picha kuwe KWAKE? nyie hamna picha mlizopiga kwa watu au sehemu nyingine tofauti?
TAFADHALI the gal is dead serious,Mnaoweza kuwa WAGOMBEA,Take action,Yaliyowashinda Kaeni Kimya.
Mhhhh yaani hapo tu ndio Missupu anaponipata maana saa zingine nakaa nafurahi sana mpaka machozi yananitoka sasa wewe uliyeandika hii unataka kuumiza watu vichwa au unataka kufurahisha baraza yaani picha za hi5 ndio mnaturetea hapa.Yaani kwanza huko uliko hujaona wanaume mpaka umekuja kutafuta online kwa michuzo?hahaha yaani kutembea kote hujapata mvulana basi wewe sio halali na kama upo halali basi nahisi unamatatizo ya akili yaani mtu unakaa kwa akili zako unakaa kwenye computer saa zima na kuandika huo uchafu kweli maisha sasa yanakwisha ok bwana wacha sisi tuinjoy mazeru zeru huko haya wewe kazi kwako unatafuta wanaume online
ReplyDeleteMdau
kutoka
Liverpool.
JIFUNZE KUPANGA NGUO NA CHUMBA VIZURI THEN UTAMPATA MWENZI ACHA UCHAFU WA MWILI NA ROHO!!!
ReplyDeleteSasa michuzi hao machangudoa wa GARDEN BISRTO wameshaona hii ndio sehemu ya kutafutia mabwana ..wanajua wakitoa picha tu lazima mijitu ilivyona uchu itaanza kufuatilia .. kuliko akikaa baa.. kujiuza .. hebu angalia hiyo picha ukutani anambusu mtoto aliyezaa na mzungu ...
ReplyDeleteIVI AYA MAMBO BADO YAPO UMU BLOGUN?SIKU NYINGI NIMEPOTEA LEO NARUDI NAKUTANA FIRST PAGE "MUME"
ReplyDeleteweee dada sio ivo ata kidogo