Serikali imemteua Hajaat Kijakazi R. Mtengwa kuwa Mwenyekiti mpya ya bodi ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa), zamani Chuo Cha Sanaa Bagamoyo.
Taarifa toka wizara ya habari, utamaduni na michezo iliyosainiwa na msemaji wa wizara hiyo mzee Jacob Tesha, kwa mujibu wa sheria za wakala wa serikali namba 9 ya mwaka 1997, waziri Mh. Kapt. Goeroge Mkuchika pia amewateua wajumbe wanane wa bodi hio.
Taarifa imewataja wajumbe hao kuwa ni pamoja na Bi. Rose Sayore, Katibu Mtendaji wa Mfuko wa Utamaduni, Mkurugenzi wa Utamaduni Mstaafu, Dk Daniel Kyaruzi Ndagala, Dk Herbert Francis Makoye ambaye ni mhadhiri Chuo Kikuu Dar na Profesa Hermes J. Mwansoko, Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni.
Waajumbe wengine wa bodi hiyo ni Bi Judica Haikase Kida Omari, ambaye ni mchumi mwandamizi, Mh. Ramadhani A. Maneno, Mbunge wa Jimbo la Chalinze na Profesa Elias Elieza Jengo, Mhadhiri UDSM na gwiji la sanaa.
Taarifa toka wizara ya habari, utamaduni na michezo iliyosainiwa na msemaji wa wizara hiyo mzee Jacob Tesha, kwa mujibu wa sheria za wakala wa serikali namba 9 ya mwaka 1997, waziri Mh. Kapt. Goeroge Mkuchika pia amewateua wajumbe wanane wa bodi hio.
Taarifa imewataja wajumbe hao kuwa ni pamoja na Bi. Rose Sayore, Katibu Mtendaji wa Mfuko wa Utamaduni, Mkurugenzi wa Utamaduni Mstaafu, Dk Daniel Kyaruzi Ndagala, Dk Herbert Francis Makoye ambaye ni mhadhiri Chuo Kikuu Dar na Profesa Hermes J. Mwansoko, Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni.
Waajumbe wengine wa bodi hiyo ni Bi Judica Haikase Kida Omari, ambaye ni mchumi mwandamizi, Mh. Ramadhani A. Maneno, Mbunge wa Jimbo la Chalinze na Profesa Elias Elieza Jengo, Mhadhiri UDSM na gwiji la sanaa.
HONGERA MAMA MTENGWA!! TUNAKUTAKIA MAFANIKIO MEMA KTK MAJUKUMU MAPYA ULIYOPEWA!!!
ReplyDeleteNDEMA MAPUNDA, THESSALONIKI, GREECE
hivi neno HAJAAT ni jina au ni cheo? ajuaye anijibu please.
ReplyDeleteNeno HAJAAT ni sawa na ALHAJ yaani mtu aliyewahi kwenda MAKKAH kuhiji.
ReplyDeletehuyu mama Mchapa kazi sana.
ReplyDelete