Kwa masikitiko makubwa tunawatangazia kifo cha Mzee wetu Robert Jaka wa Forest Hill- Morogoro (pichani), kilichotokea katika hospitali ya Regency mchana huu wa Jumapili ya tarehe 22/01/2012 Dar-es-salaam-Tanzania.
Marehemu katika uhai wake alifanya kazi katika vyuo vikuu vya Sokoine na baadae chuo kikuu cha Dar-es-salaam kabla ya kustaafu na kurejea Morogoro. Msiba upo Dar-es-salaam Mtoni-Kijichi (nyumba za maafisa wa Magereza)
Mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa kwenda Morogoro siku ya Jumanne na Mazishi yanatarajiwa kufanyika Morogoro siku ya Jumatano tarehe 25.01.2012.
Kwa taarifa zaidi za msiba unaweza kuwasiliana na Kizito Jaka (+255 762 583740 begin_of_the_skype_highlighting +255 762 583740 end_of_the_skype_highlighting) Paschal Kunambi () au Exupelius Kunambi (+255 767 201098 begin_of_the_skype_highlighting +255 767 201098 end_of_the_skype_highlighting)
R.I.P mzee Jaka ulikuwa mtu wa aina yake ulipokuwa unafanya kazi UDSM mwenyezi mungu akurehemu .amen
ReplyDeletePoleni sana akina Kizito. Mzee Jaka ni jirani yangu pale Forest Hill Morogoro. Ukapumzike kwa amani.
ReplyDeletepoleni sana wana familia,poleni sana wanamji kasoro bahari,mungu ailaze mahala pema peponi roho ya mzee jaka.
ReplyDeleteMzee Jaka nimefanya kazi nae pale UDSM ni mtu mwema sana. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, amin.
ReplyDeleteR.I.P my dear father.
ReplyDeleteNatoa pole sana kwa Familia ya Mzee Jaka. Nawaombea familia yake ipate faraja katika kipindi hiki kigumu.
ReplyDeleteRIP Mzee Jaka
Mzee Jaka alikuwa jirani yetu pale Simba Road karibu kabisa na UDASA. Taifa limepoteza mmoja wa wazee ambao walikuwa mfano mkubwa kwa wasomi wa kizazi chetu.
ReplyDeletePole sana wapendwa wetu Jaka and Kunambi's family Mwenyezi Mungu awatie nguvu. RIP baba mpendwa
ReplyDelete