Trekta 4 zilizonunuliwa kupitia Mpango wa kuendeleza kilimo wilayani(DADPS) Kabla ya kukadhiwa kwa
vijiji vya  Litama,Nachinyimba,Chilangalile na Michenga Wilayani Ruangwa
 .Mkurugenzi  mtendaji wa Halmashauri hiyo Bw Reubern Mfune akiweka saini mkataba wa makabidhiano na Mwenyekiti wa kijiji cha kijiji cha Nachinyimba Bw Hassan Saidi Mchaka 
 .Mkuu wa wilaya ya Ruangwa Bi Agness Hokororo(Mb) akijaribu kabla ya kukabidhi trekta na mkataba wa umiliki wa Trekta hiyo kwa Mwenyekiti wa kijiji cha Chilangalile kata ya Makanjiro,Bw Juma saidi Nangolingo huku ikishuhudiwa na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Bw Reubern Mfune katika hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika mbele ya ofisi ya Idara ya Kilimo Wilayani Ruangwa
Wananchi wakishuhudia makabidhiano hayo. 

Picha na habhari na Abdulaziz Video, Ruangwa

 Jumla ya hekta 14960 zinatarajiwa kulimwa wilayani Ruangwa  Msimu huu wa kilimo 2012/13 kufuatia upatikananji wa matrekta makubwa yaliyotolewa na Halmashauri hiyo  na kukabidhiwa kwa vijiji Vinne vilivyopo Wilayani Humo.

Hayo yalielezwa na Mkuu wa wilaya ya Ruangwa,Bi Agness Hokororo(Mb)alipokuwa akikabidhi trekta 4 aina ya  Farmtrac (70E 60 HP 2WD)zilizonunuliwa Kupitia  Mpango wa Maendeleo na Uendelezaji Kilimo wilayani(DADPS)Yenye thamani ya Tshs 160 Milioni ikiwa ni gharama ya Ununuzi na Usafirishaji hadi kufika wilayani humo.


Akiongea na Wakulima hao baada ya Taarifa fupi ya makabidhiano iliyosomwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bw Reubern Mfune,Mkuu wa wilaya aliwataka wakulima hao kuanzisha akaunti maalum
ya kuyatunza matrekta hayo na mapato yote kuwekwa katika akaunti hizo ili kusaidia kumudu kujiendesha ikiwa pamoja na kuchangia asilimia 20 kwa ajili ya marejesho ya ununuzi wa trekta hizo ili kijiji kiweze
kumilikishwa.



Aidha Bi Hokororo aliitaka halmashauri hiyo kupitia maafisa Ugani kuhakikisha wanasaidia uendeshaji wa miradi hiyo huku wakiamasisha Jamii kuandaa mashamba yao ili yasiwe na Visiki ikiwa pamoja na kuhakikisha trekta hizo zinabeba mzigo uliolingana na uwezo uliopangwa kubebwa na trekta hizo.



‘’Nataka muhakikishe kuwa trekta hizo ninazowakabidhi leo zinatumika kwa misingi ya kilimo na ziendeshwe na dereva mwenye leseni na aliepatiwa Mafunzo na si Vinginevyo’’’Alimalizia Hokororo.



Vijiji vilivyonufaika na Mpango huo ni Litama,Nachinyimba,Chilangalile na Michenga ambazo ziliwezeshwa kuibua miradi ya Kilimo na kupatiwa
Mafunzo




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Ruangwa sio RWANGWA

    ReplyDelete
  2. Mkuu wa Wilaya na Mbunge wa Ruangwa.

    Hivi jamani Wasomi wanao hitimu kila mwaka Elimu ya Juu wakafanye kazi wapi kama ndio hivi mwenendo ndio huu mtu mmoja Kofia mbili?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...