Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Samuel Sitta akimpatia taarifa juu ya mwenendo wa Bunge Maalum la katiba na ulipofikia, Rais Wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mheshimiwa Dkt. Ali Mohammed Shein, alipomtembelea nyumbani Ikulu ya Migombani Zanzibar. Mhe Sitta alikuwa Visiwani Zanzibar kwa lengo la kuonana na Mhe. Shein kumpatia taarifa kamili ya shughuli za Bunge Maalum la Katiba. Picha na Owen Mwandumbya - Bunge Maalum
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Samuel Sitta jana amefanya ziara ya kikazi Visiwani Zanzibar na kutana na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mheshimiwa Dkt. Ali Mohammed Shein, kumpatia taarifa juu ya mwenendo wa Bunge Maalum la katiba na hatua lilipofikia. Mhe. Sitta amekutana na Dkt. Shein katika Ikulu Ndogo Ya Migombani, Zanzibar ambapo aliweza kumpatia picha halisi ya maendeleo ya Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba unaoendelea Mjini Dodoma, Rais wa Zanzibra.
Akizungumzia mchakato wa Utungaji Kanuni, Mhe. Sitta amemwambia Dkt. Shein jinsi hatua hiyo ilivyokuwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na jinsi Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo Mhe. Pandu Ameri Kificho alivyoweza kufanikisha zoezi hilo kwa kuunda kamati ya watu 20 kuongoza utungaji wa Kanuni hizo ikiongozwa na Mheshimiwa Profesa Costa Ricky Mahalu, ambapo alisema matarajio utungaji wa Kanuni ulikadiriwa kukamilika ndani ya muda wa siku tatu, hata hivyo, kutokana na umuhimu wa jambo lenyewe na haja ya kuwa na Kanuni makini kwa ajili ya kuendesha Bunge, muda huo haukutosha na badala yake Bunge lilichukuwa wiki tatu kukamilisha kazi ya kutunga Kanuni hizo.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Samuel Sitta jana amefanya ziara ya kikazi Visiwani Zanzibar na kutana na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mheshimiwa Dkt. Ali Mohammed Shein, kumpatia taarifa juu ya mwenendo wa Bunge Maalum la katiba na hatua lilipofikia. Mhe. Sitta amekutana na Dkt. Shein katika Ikulu Ndogo Ya Migombani, Zanzibar ambapo aliweza kumpatia picha halisi ya maendeleo ya Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba unaoendelea Mjini Dodoma, Rais wa Zanzibra.
Akizungumzia mchakato wa Utungaji Kanuni, Mhe. Sitta amemwambia Dkt. Shein jinsi hatua hiyo ilivyokuwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na jinsi Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo Mhe. Pandu Ameri Kificho alivyoweza kufanikisha zoezi hilo kwa kuunda kamati ya watu 20 kuongoza utungaji wa Kanuni hizo ikiongozwa na Mheshimiwa Profesa Costa Ricky Mahalu, ambapo alisema matarajio utungaji wa Kanuni ulikadiriwa kukamilika ndani ya muda wa siku tatu, hata hivyo, kutokana na umuhimu wa jambo lenyewe na haja ya kuwa na Kanuni makini kwa ajili ya kuendesha Bunge, muda huo haukutosha na badala yake Bunge lilichukuwa wiki tatu kukamilisha kazi ya kutunga Kanuni hizo.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
aseme kama kawata ukawa
ReplyDelete